Watanzania: Udaku na Nadharia za Njama

Watanzania: Udaku na Nadharia za Njama

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Naona kama kuna idadi kubwa sana ya watanzania wanaopenda vitu hivyo, yaani Udaku (habari za kuhusu mambo ya watu wengine) na Nadharia za Njama (kuwa kuna jambo la njama linafichwa na serikali au taasisi yoyote). Ukitaka kula hela ya watanzania, jikite katika biashara ya kuuza udaku na nadharia za njama; utachuma kweli kweli kweli.

Mkapa alitututakana kuwa tuna uvivu wa kufikiri, maneno ambayo aliyakopi kwa mgriki mmoja wa zamani sana nadhani Alistotle, lakini ndio ukweli kuwa hatutaki kufikiri badala kupokea habari nyepesi kama hizo. La ajabu ni kuwa hiyo ni hulka ya watu wengi sana duniani, siyo watanzania tu.

Wanasiasa kadhaa wa upinzani wameona malipo ya nadharia za njama, na ndiyo imekuwa sera yao. Vyombo vingi vya habari vinegudundua malipo ya udaku, na vimekuwa vinaweka udaku sana kwenye habari zao.

Swali: Je kuna uwezekano wa kuvunja hii cycle ya udaku na nadharia ya njama, na badala yake kukuza ukweli unaohusu maisha yetu sote.
 
Wachache wanalifahamu hilo na ndio maana viongozi wanaweza peleka jamii waonavyo!
Kutoka hapo itachukua kipindi kirefu Kuna kiongozi mmoja alishawahi kusema Sera zake ya kwanza hadi ya tatu itakuwa ni Elimu,Elimu,Elimu!
Nafikiri kuna kitu aliona..

Mtu hawezi kutoka huko Kama bongo yake haijakaa sawa,chakufanya nawe ukigundua hilo watumie tu maana wanayataka wenyewe!
 
Huo uwezekano wa kuvunja cycle ya udaku na nadharia ya njama kwa dunia ya Sasa na kizazi Cha vijana kilichopo ni ngumu sana.

Ila tunaweza kupunguza madhara yake kwa kujikita kwenye kuboresha kiwango cha elimu kwa wanachopata vijana huko mashuleni na vyuoni.
 
Kwa hiyo na wewe unaamini kweli vifo vya Corona ni watu 16.

Unaonyeshwa video na picha pia huoni.

You must be stupid.

Sent using Jamii Forums mobile app

Matusi yako yanaonyesha kuwa wewe ni mmoja wa watanzania hao; hujaleta ukweli bali unasema zile zile nadharaia za njama (Conspiracy Theories). Ninaishi katikati ya ugonjwa wa Korona duniani (marekani), na ninaomba sana nisipatwe na kadhia hiyo. Hizo picha na video unazosema wewe hazina uhusiano na uathirikaji wa ugonjwa wa korona kama tunavyoufahamu.
 
Watanzania ukiwasikiliza watakutoa kwenye reli
Wengi ni wapiga majungu na umbeya
 
Hata kwenye huu uzi tumekuja baada ya kuona neno "udaku".

Sisi ndio waTZ wewee.
 
Serikali kuficha ukweli ni vitu vya kawaida sana. Serikali ingependa muiamini kwa 100% kwasababu ndiyo siasa zenyewe hizo.
Serikali wanataka wakisema walimpigia Mungu simu na walikubaliana na Mungu 123, na ABC wananchi mshangilie na msihoji wala msifikiri na kujiuliza uhalisia wa kilichosemwa. Serikali ziko hivyo, zinapenda akina " ndiyo mzee" .
Uongo ndio sifa za wanasiasa wote, wanapotaka wapigiwe kura na kuendelea kutawala hawajali wanasema nini na matokeo ya wanachosema kina athari gani, ilimradi kina muweka madarakani, hilo ndilo wao wanajali.
Ndio maana hawataki mgombea huru, na hata vyama vingi hawataki kwasababu hawataki kukosolewa kwa lolote.
Binadamu wako curious kujua ukweli wa mambo mengi, wanapofanya hivyo kwa kuhoji wewe unasema wanapenda conspiracy na udaku, nadhani unakosea kuwaona watanzania ni waongo na wambeya. Ikiwa ndivyo tulivyo basi na watawala nao ni waongo na ni wambeya pia.
Sasa kama umbeya na uongo ndiyo sifa zetu na kupenda udaku, unashangaa nini tukifanya tunachokipenda?!
Watanzania tunapenda ugali, tunapenda pombe , je hilo ni tatizo tukila ugali na kunywa pombe?!
Wewe uko marekani lakini ni mtanzania, je na huko una practice mambo ya kitanzania kupenda udaku na conspiracy au wewe umeshakuwa mmarekani hivyo vitabia vyetu vya kitanzania umeviacha?!
Siyo kwamba mtu akikataa usemacho ni mdaku, au akileta mawazo yake ni conspiracy, yafanyie kazi uweze ku prove otherwise siyo ku generalize kwamba tunapenda udaku na conspiracy.
Wewe unamapenzi na Magufuli hivyo kila asemacho yeye ndicho sahihi na kila wafanyacho wengine siyo sahihi, lakini huo ni mtizamo wako na mapenzi yako. Waache walioamua kutoja nje ya box waulize na wapate majibu yenye kuridhisha nadharia zao.
Kuna watu they trust nothing and question everything, ndivyo walivyo, usiwaite wadaku na conspiracy mongers.
 
Kiwango cha Elimu hakihusiani na kuamini conspiracy. Kuna Ph.Ds na Maprofesa kutoka vyuo vikubwa kama Havard wanaamini conspiracy theories za kijinga kabisa.
Huo uwezekano wa kuvunja cycle ya udaku na nadharia ya njama kwa dunia ya Sasa na kizazi Cha vijana kilichopo ni ngumu sana.

Ila tunaweza kupunguza madhara yake kwa kujikita kwenye kuboresha kiwango cha elimu kwa wanachopata vijana huko mashuleni na vyuoni.
 
Back
Top Bottom