Humorous Junior
JF-Expert Member
- Jul 19, 2018
- 1,598
- 1,410
KWANINI USIWATAFUTE? NANI KAKUZUIA MPAKA UNAMTAKA LISSU?Jiwe alikuwa hajawahi kuwa hata kiranja wa darasa, hata wa chekechea, leo eti ni Rais......
Tunawataka Ben, Azory, Mawazo, Akwilina and many others...... hatusikii lolote katu
Vyombo hivyo hivyo vya dola ushindwa kuzilinda mamlaka zinazokengeuka na kuacha misingi ya kuongoza watu kwa kutumia kanuni za kuongozea wanyama kuongozea watu dola ilishindwa kuziokoa na zilianguka na kufutika kabisa,soma history ya rise and fall of kingdoms au mwambie yeriko akupe shule zaidi kuhusu dola na mamlaka.Usije ukatuambia hata manabii walifanikiwa kwa sababu walikuwa kwenye kipindi cha Giza, hahahahahaha.
Kijana ukishajua kutumia kompyuta na smart phones pamoja na ku-download na ku-upload unajiona upo kwenye zama za Nuru hahahahahaha..
Tunamfahamu sasa vilivyo kuliko zamani. Alichowafanyia Watanzania, wengi wanafahamu. Yale tuliyoyategemea, sina haja ya kuyataja maana ni ya kawaida, na yalifanywa na watangulizi wake. Lakini yafuatayo yamekuwa dhahiri chini ya utawala wake:Habari za muda huu ndugu wanabodi wenzangu? Leo nimerudi tena baada ya takribani siku kadha zilizopita kuwa na majukumu mengine na hasa ya kiuchumi pamoja na ya kisiasa..
We peleka ujinga wako Lumumba!! Uongozi uongozi!! nilini jiwe aliwahi hata kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa?? Kama ni ubunge Lisu nae amekuwa mbunge!! Mwanasheria msomi!! mtu wa haki!! amekuwa akitetea watu kabla hata hajawa mbunge!! ni jinsi gani anaupendo na watu!! sio mnafiki Kama walivyo viongozi wenu!Habari za muda huu ndugu wanabodi wenzangu? Leo nimerudi tena baada ya takribani siku kadha zilizopita kuwa na majukumu mengine na hasa ya kiuchumi pamoja na ya kisiasa...
Usitake kutuaminisha kwamba mchakato wote huu wa uchaguzi ni danganya Toto, Kama kuchagua chadema na lissu ni kuhatarisha utulivu na amani ya nchi, kosa si la lissu wala chadema ball ni kosa la walioitisha uchaguzi, lissu ana kura nyingi kuliko babu yenu na uchaguzi huu lissu atamshinda babu yenu kwa kishindo.Ni kweli kuwa wewe na wenzako ninshemu ya watanzania ambao mmeamua kuwajaribu wakina Lissu na CHADEMA. Lakini huna budi kufahamu kuwa amani na utulivu katika nchi huletwa na walio wengi. Watanzania walio wengi kwa idadi wataenda kumpa Rais John Pombe Magufuli miaka mitano Tena ya uongozi.
Anasema chagua mgombea wa ccmAliyeisoma tafadhali naomba atufupishie kwa neno moja au mawili.
Mkuu. mleta mada ni ushamba tu ndio unamsumbua!! achana nae! uwezo wake wa kufikiri umeishia hapo!!Wazungu wa Marekani walisema hivyohivyo wakati wa Obama. Uraisi haujaribiwi. Eti nweusi kutawala ni kujaribu kana kwamba uraisi ni kwa weupe tu. Akishinda wa Chadema ni kujaribu uraisi kana kwamba umewekwa kwa ajili ya ccm tu. Acheni hizo!!! Tukimchagua Jiwe akionekana kuburuza Watz, tunabadilisha.
Lissu ndiye hitaji kubwa la Wtz kwa sasa atakayeirudisha nchi katika misingi ya utawala wa sheria badala ya huu wa kiimla. Leo jiwe akiwa Same aliagiza ziletwe milioni 100 kukarabati Zahanati. Aibu. Hivi Uraisi sio taasisi? Hivi hakuna mfumo on place wa kufanya hivyo? Tumechoka na ujinga. Kura zote kwa Lissu.
Huyu ni mshamba Kama walivyo waliomtuma!!Mimi nmeishia kusoma heading tu nikajua huyu ataegemea wapi na lengo lake ni nini, Nipo kusoma comments tu...
Sikiliza video ya Bashiru. ameungana na Lisu kunadi sera zake!!Chagua : Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu
Kishajichokea lakini anang’ang’ania tu. Alidhani Urais ni lelemama na udhalimu wake ungetufanya Watanzania tukae kimya.
Na walivyogoma kujiandikisha na kuhakiki taarifa eti sababu Lowasa alishindwa sasa😁😁😁View attachment 1606888
Lissu for Life
Kule wamefata maslai lkn hata nafsi zao zinawasuta hasa ukiwa msomi,unajua hakuna Uhuru wa watu Hakuna maendeleo ya watu.Sikiliza video ya Bashiru. ameungana na Lisu kunadi sera zake!!
Hayo aliyoyaleta ameleta kwa wachache but wengi ameshindwa kuwagusa thus unaona upepo ulivyoNimejitahidi kukuelewa kiasi. Ni kweli waafrika ni waoga wa mabadiriko, ni kwa sababu hawajayajua hasa yanalengo gani kwao maana ni msamiati mpya.
Lakini waafrika hawahawa wapo tayari kundilika na hawayaogopi mabadiliko. Ambayo yatakuwa na msingi wa kuleta maendeleo ya watu wote na sio kwenye kundi la watu fulani wa nchi. Waafrika wanataka wafikie uwezo wa kupata huduma za muhimu za jamii uwe no uwezo wa kila mtu. Ikiwa n huduma ya maji safi na salama, elimu Bor, afya bora, lishe bora n.k kama ambavyo yametekelezwa vema na Rais Magufuli kwa miaka mitano ya kwanza. Hakika #MagufuliNiMafanikio.
#magufuli5tena
Wakati Magufuli akituburuza kwa miaka 5 inaonekana wewe ulikuwa kwenye fungate.Habari za muda huu ndugu wanabodi wenzangu? Leo nimerudi tena baada ya takribani siku kadha zilizopita kuwa na majukumu mengine na hasa ya kiuchumi pamoja na ya kisiasa.
Tumetafuta kura za kutosha na kwa tathimini ya haraka tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuweza kuwafahamisha watanzania wengi nchini, kuhusu ilani yao pendwa na ahadi za kiongozi wao mpenzi. Na kutegemeana na matokeo ya tafiti ndogo zilizofanyika ni kwamba mgombea wetu na ilani ya chama chetu imefanikiwa kueleweka na kupokelewa vema, na hivyo upo uwezekano mkubwa wakupata idadi ya kura zaidi ya 90% ya wapiga kura watakaojitokeza.
Leo nimekuja kuendeleza kazi ile ya kutafuta kura ya ushindi wa kishindo kwa chama chetu pendwa na mgombea wetu mpendwa, chaguo la watanzania wazalendo.
Inafahamika kuwa historia ya binadamu haiwezi abadani kujitenga na historia ya amani, ya utulivu na ya uchumi. Binadamu amekuwa akitafuta amani, utulivu na uchumi tangu alipoanza kupata ufahamu kuhusu Dunia hii. Na kwa jinsi hiyo Binadamu huyu amejikuta akikutana na usaliti na utumwa wa namna zote katika akili na hali ya maisha. Waliofanikiwa katika utumwa walishindwa katika uaminifu, vivyo waliofanikiwa katika uaminifu waliushinda utumwa.
Afrika ni bara ambalo watu wake wamepitia historia ya kutisha na kuhuzunisha kwa karne nyingi, hata kabla ya kugawanywa kwake. Inasemekana biashara ya utumwa ndani ya Afrika ilianza katika karne ya 14 huko nyuma. Ni kwa sababu gani hasa..? Ukweli wa historia ya mwafrika kuingia utumwa ni kukosekana kwa uaminifu kwa baadhi ya viongozi wa makabila makubwa, ndio kusema historia ya mwafrika imegubikwa na usaliti. Kundi moja kujiona ni bora zaidi kuliko wenzao, kwamba ni wao pekee wanastahili lakini sio wengine. Hivyo kupelekea kusalitiana. Utashangaa Makaburu kuweza kuitawala Afrika kusini baada ya miaka 100 tu tangu kuingia kwake miaka ya 1400's. Ambapo wakaburu wa kwanza kukanyaga ardhi ya Mzee Madiba Mandela inakadiriwa idadi ya wazee wastaafu wasiozidi 200! Lakini ndio hao waliweza kuwatawala zaidi ya waafrika 100k ya wazawa.
Hivyo kwa sababu ya usaliti, Afrika tulitawaliwa. Lakini kwa kuwa Binadamu ameendelea kutafuta amani na utulivu ni dhahiri kuwa ilitakiwa Uhuru uwepo kwa waafrika ili mwafrika aweze kupata amani na utulivu. Na kwa jinsi hiyo ni katika karne ya 19, waafrika walianza kujitafutia Uhuru wao na kwa kweli ilitakiwa kujenga umoja na kujengeana hali ya kuaminiana kwanza ili kufanikisha kuikomboa Afrika. Hivyo basi, umoja wa waafrika na uongozi wenye uaminifu uliwezesha Afrika kujikomboa na watu wake kuwa huru. Na sasa waafrika wanawajibika na ujenzi wa uchumi wa nchi zao.
Leo Tanzania kama sehemu ya Afrika inatudai uaminifu wetu sisi waafrika watanzania katika kuhakikisha tunayaendeleza yale ambayo Afrika iliyahitaji kwa muda mrefu hata kuweza kujikomboa. Nao ni umoja wa waafrika, ndio kusema kuwa Tanzania, inatudai umoja wetu sisi watanzania.
Sasa tutawezaje kuilipa Tanzania? Kipindi tunaelekea uchaguzi mkuu, wajibu wetu ni kupiga kura kwenda kumchagua kiongozi ambaye atakuwa na misuli imara isiyotetereka katika kuwaunganisha watu pasi na kuwagawa katika misingi ya udini, ukabila wala hali zao kiuchumi. Kiongozi ambaye wajibu wake ni kwa Tanzania na Afrika, kiongozi ambaye kipaumbele chake ni kuendeleza na kukuza siasa zenye kufuata tamaduni za mwafrika na Afrika. Tukachague chama ambacho kinaamini katika ujamaa na kujitegemea kwamba usawa ndani ya jamii ndio msingi wa haki sawa kwa wananchi wote na hivyo huzaa matunda ya amani na utulivu na uaminifu baina ya Watanzania.
Siasa haiwezi kujitenga na Tanzania, na watanzania hawawezi kujitenga na siasa. Hivyo wajibu wetu ni kuwapima wanasiasa na kutambua ni wanasiasa gani wenye malengo ya kudumisha umoja, amani na utulivu wa Afrika! Kushindwa kutambua jambo hilo, ni kuiweka nchi katika hatari ya kurudi kule ilipotoka. Hivyo basi siasa haijaribiwa bali hutekelezwa kwa umakini na uangalifu mkubwa. Kwa miaka mitano sasa, wapo wanasiasa ambao kwa haiba zao, uwezo wao wa misuli, uzalendo wao kwa nchi umefunuliwa kwetu.
Tarehe 28/10/2020 siku ya jumatano, ni siku ambayo inaenda kutoa uelekeo wa Tanzania kwa miaka mitano na zaidi mbeleni. Ewe Mtanzania napenda nikukumbushe kuwa hakuna dalali ambaye aliwahi kumuacha salama mwenye mali. Yeye anasukumwa na faida zake binafsi na sio za mwenye mali. Dalali yeyote atakayeweza kuingia ikulu pale, ni hakika yangu watanzania hawatakuwa salama, Tanzania ni ya watanzania. Chagua mtanzania mzalendo mwenye kuiona Tanzania katika mioyo ya watanzania, na sio mwenye kuiona Tanzania katika mikataba ya madini iliyopo tu. Hiyo ni ishara ya udalali wa wazi kabisa. Amka asubuhi kisha fanya uamuzi wa kwenda kumchagua Rais wa nchi mzalendo na mwenye maamuzi magumu na mwenye kuamini katika misimamo yenye tija kwa ajili ya watanzania, hana msukumo wa uoga bali ni ukweli wa kitafiti, fahari ya Tanzania, kiongozi mfano wa kuigwa na Marais wa mataifa hata ya Ulaya na Asia, si mwingine ni Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI. Leo hii mataifa wanashangaa ni jinsi gani ajabu alivyoweza kidhibiti covid-19 bila lockdown?! Walipogundua kuwa ni maombi, sasa na wao wanaitisha maombi ndani ya nchi zao.
#chaguaMagufuli2020
#chaguaCCM2020
#Magufuli5Tena
Sauti ya Mdodomia
20/10/2020.
Wewe ni idiot of the month.Habari za muda huu ndugu wanabodi wenzangu? Leo nimerudi tena baada ya takribani siku kadha zilizopita kuwa na majukumu mengine na hasa ya kiuchumi pamoja na ya kisiasa.
Tumetafuta kura za kutosha na kwa tathimini ya haraka tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuweza kuwafahamisha watanzania wengi nchini, kuhusu ilani yao pendwa na ahadi za kiongozi wao mpenzi. Na kutegemeana na matokeo ya tafiti ndogo zilizofanyika ni kwamba mgombea wetu na ilani ya chama chetu imefanikiwa kueleweka na kupokelewa vema, na hivyo upo uwezekano mkubwa wakupata idadi ya kura zaidi ya 90% ya wapiga kura watakaojitokeza.
Leo nimekuja kuendeleza kazi ile ya kutafuta kura ya ushindi wa kishindo kwa chama chetu pendwa na mgombea wetu mpendwa, chaguo la watanzania wazalendo.
Inafahamika kuwa historia ya binadamu haiwezi abadani kujitenga na historia ya amani, ya utulivu na ya uchumi. Binadamu amekuwa akitafuta amani, utulivu na uchumi tangu alipoanza kupata ufahamu kuhusu Dunia hii. Na kwa jinsi hiyo Binadamu huyu amejikuta akikutana na usaliti na utumwa wa namna zote katika akili na hali ya maisha. Waliofanikiwa katika utumwa walishindwa katika uaminifu, vivyo waliofanikiwa katika uaminifu waliushinda utumwa.
Afrika ni bara ambalo watu wake wamepitia historia ya kutisha na kuhuzunisha kwa karne nyingi, hata kabla ya kugawanywa kwake. Inasemekana biashara ya utumwa ndani ya Afrika ilianza katika karne ya 14 huko nyuma. Ni kwa sababu gani hasa..? Ukweli wa historia ya mwafrika kuingia utumwa ni kukosekana kwa uaminifu kwa baadhi ya viongozi wa makabila makubwa, ndio kusema historia ya mwafrika imegubikwa na usaliti. Kundi moja kujiona ni bora zaidi kuliko wenzao, kwamba ni wao pekee wanastahili lakini sio wengine. Hivyo kupelekea kusalitiana. Utashangaa Makaburu kuweza kuitawala Afrika kusini baada ya miaka 100 tu tangu kuingia kwake miaka ya 1400's. Ambapo wakaburu wa kwanza kukanyaga ardhi ya Mzee Madiba Mandela inakadiriwa idadi ya wazee wastaafu wasiozidi 200! Lakini ndio hao waliweza kuwatawala zaidi ya waafrika 100k ya wazawa.
Hivyo kwa sababu ya usaliti, Afrika tulitawaliwa. Lakini kwa kuwa Binadamu ameendelea kutafuta amani na utulivu ni dhahiri kuwa ilitakiwa Uhuru uwepo kwa waafrika ili mwafrika aweze kupata amani na utulivu. Na kwa jinsi hiyo ni katika karne ya 19, waafrika walianza kujitafutia Uhuru wao na kwa kweli ilitakiwa kujenga umoja na kujengeana hali ya kuaminiana kwanza ili kufanikisha kuikomboa Afrika. Hivyo basi, umoja wa waafrika na uongozi wenye uaminifu uliwezesha Afrika kujikomboa na watu wake kuwa huru. Na sasa waafrika wanawajibika na ujenzi wa uchumi wa nchi zao.
Leo Tanzania kama sehemu ya Afrika inatudai uaminifu wetu sisi waafrika watanzania katika kuhakikisha tunayaendeleza yale ambayo Afrika iliyahitaji kwa muda mrefu hata kuweza kujikomboa. Nao ni umoja wa waafrika, ndio kusema kuwa Tanzania, inatudai umoja wetu sisi watanzania.
Sasa tutawezaje kuilipa Tanzania? Kipindi tunaelekea uchaguzi mkuu, wajibu wetu ni kupiga kura kwenda kumchagua kiongozi ambaye atakuwa na misuli imara isiyotetereka katika kuwaunganisha watu pasi na kuwagawa katika misingi ya udini, ukabila wala hali zao kiuchumi. Kiongozi ambaye wajibu wake ni kwa Tanzania na Afrika, kiongozi ambaye kipaumbele chake ni kuendeleza na kukuza siasa zenye kufuata tamaduni za mwafrika na Afrika. Tukachague chama ambacho kinaamini katika ujamaa na kujitegemea kwamba usawa ndani ya jamii ndio msingi wa haki sawa kwa wananchi wote na hivyo huzaa matunda ya amani na utulivu na uaminifu baina ya Watanzania.
Siasa haiwezi kujitenga na Tanzania, na watanzania hawawezi kujitenga na siasa. Hivyo wajibu wetu ni kuwapima wanasiasa na kutambua ni wanasiasa gani wenye malengo ya kudumisha umoja, amani na utulivu wa Afrika! Kushindwa kutambua jambo hilo, ni kuiweka nchi katika hatari ya kurudi kule ilipotoka. Hivyo basi siasa haijaribiwa bali hutekelezwa kwa umakini na uangalifu mkubwa. Kwa miaka mitano sasa, wapo wanasiasa ambao kwa haiba zao, uwezo wao wa misuli, uzalendo wao kwa nchi umefunuliwa kwetu.
Tarehe 28/10/2020 siku ya jumatano, ni siku ambayo inaenda kutoa uelekeo wa Tanzania kwa miaka mitano na zaidi mbeleni. Ewe Mtanzania napenda nikukumbushe kuwa hakuna dalali ambaye aliwahi kumuacha salama mwenye mali. Yeye anasukumwa na faida zake binafsi na sio za mwenye mali. Dalali yeyote atakayeweza kuingia ikulu pale, ni hakika yangu watanzania hawatakuwa salama, Tanzania ni ya watanzania. Chagua mtanzania mzalendo mwenye kuiona Tanzania katika mioyo ya watanzania, na sio mwenye kuiona Tanzania katika mikataba ya madini iliyopo tu. Hiyo ni ishara ya udalali wa wazi kabisa. Amka asubuhi kisha fanya uamuzi wa kwenda kumchagua Rais wa nchi mzalendo na mwenye maamuzi magumu na mwenye kuamini katika misimamo yenye tija kwa ajili ya watanzania, hana msukumo wa uoga bali ni ukweli wa kitafiti, fahari ya Tanzania, kiongozi mfano wa kuigwa na Marais wa mataifa hata ya Ulaya na Asia, si mwingine ni Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI. Leo hii mataifa wanashangaa ni jinsi gani ajabu alivyoweza kidhibiti covid-19 bila lockdown?! Walipogundua kuwa ni maombi, sasa na wao wanaitisha maombi ndani ya nchi zao.
#chaguaMagufuli2020
#chaguaCCM2020
#Magufuli5Tena
Sauti ya Mdodomia
20/10/2020.