Uchaguzi 2020 Watanzania, uongozi haujaribiwi. Chagua kwa ajili ya Uhuru na Amani ya Watanzania

Thibitisha jinsi Lissu na chadema watskavyo ondoa amani.
Lkn pia kipindi chote cha Magufuli amani imepotea, tumeshuhudia watu kutekwa na kuptezwa, maiti kuokotwa hovyo. Ni kwamba hatuko salama.
Kama Mo aweza kutekwa kirahisi namna hile, mimi wakinitaka si ni sekunde tu??.
 
Hao majambazi wataiba nakupora nini wakati kila mtu yuko hoi kifedha.Kilichobadilika ni mfumo wa maisha kutokana na ugumu wa maisha ila sio kwamba kuna jitihada zozote zimefanyika.labda uniambie jitihada zakufukarisha wananchi.Hayo ya uvuvi hebu yaache maana huyajui kabisa.
 
Umeandika jambo lile lile kwa viswahili vingi vyakuchengesha chengesha ukweli.ndugu hii dunia yaleo sio wote wakudanganya hivyo.
 
BABA YAKO asingejaribiwa na mama yako sidhani kama ungezaliwa . kuna mtu amezaliwa na cheo?
 
Matendo ya kijambazi yameongezeka sana awamu ya magufuli: Lissu kupigwa risasi, Akwilina kuuwawa kwa risasi, Ben saanane kupotea, Azori kupotea, Mo Dewji kutekwa, Zakari kutekwa (jaribio lilifeli), Bureau de change kuporwa, Kimara kubomolewa nyumba, maiti kwenye viroba kuokotwa ufukweni, wakulima kudhulumiwa korosho, n.o. Ni mengi sana. Tunataka UHURU HAKI NA MAENDELEO YA WATU.
LISSU NDIYE RAIS atakae tupatia UHURU HAKI NA MAENDELEO YA WATU.
 
Rojo ya pumba.
 
rubbish.

ingekuwa hivyo basi kina nyerere na wenzake wasingepambana kuwatoa wakoloni wa kizungu.

safari hii tunamtoa mkoloni wa kijani.
 
Jiwe alikuwa hajawahi kuwa hata kiranja wa darasa, hata wa chekechea, leo eti ni Rais......
Tunawataka Ben, Azory, Mawazo, Akwilina and many others...... hatusikii lolote katu
Nawaza tu (yaani kuwaza kwa sauti) kwamba ule uzoefu wa uwaziri waweza kuwa umembeba kidogo.
 
Tunaenda kumchagua Tundu Antiphas Lissu kwa ajili ya Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu.
Hatutaki tena kupigwa risasi, kutekwa na kubsmbikiwa makesi!
Nadhani wewe si mmojawapo wa waliopigwa risasi. Kwa hiyo ni kosa kujijumlisha. Idadi itakuwa ya uongo.
 
Huwa najiuliza hivi mtu unapata muda wapi kukaa na kuchonga uwongo mrefu na mweupe kiasi hiki!
Hizo tafiti za kura za ushindi wa 90% aikosi ni polepole ndo kazifanya?

Pamoja na kufanya siasa za kampeni pekeake miaka 5, Lakini kila siku tunazisikia hujuma za kutengenezwa, mara karatasi za kura zimetengenezwa na kampuni ya makada wa ccm! Mara karatasi zimechapwa mgombea wa CCM juu kabisa, wa Upinzani chini kabisa! Mara tume iengue wagombea wa upinzani huku wenye speed wakisimamishwa! Mara huku jeshi la polisi likitumika kutisha na kukamata wafuasi wa upinzani!

Pamoja na hayo yote lakini bado moto wa Lissu ni palepale, CCM wameshapoteana, Sasa mnakimbilia kutangaza matokeo ya kuchakachua!

Mtashindana sana, lakini hamtashinda! Tarehe 28.10.2020 Watanzania watawafunza adabu!
 
Nikweli unacho kisema lakini nitofauti kidogo namadai yangu mm siupendi uvuvi haram uvuvi nilikuwa navua mm ni uvuvi wakipe ziwatanganyika ni uvuvi ambao unafanyika kwenyekina kikubwa sana chamaji nyavu yake huvua dagaa wakigoma na tunakata leseni yauvuvi huo lakini walipo fika hao wachomaji walituomba tuwaonyeshe zana tunazotumia sisi kwakujiamini tuliwaonyesha waliangalia nawakasema zipo sawa lakini wakasema tumetumwa pesa kama hakuna pesa tunazichoma kwahiyo hazikuchomwa kwasababu nyingine yoyote nikwasababu hatukua napesa zakuwapa ipohivyo kifupi kiletulifanyiwa unyama embu angalia tunasalimisha iliupime naunasema ziposawa unaomba pesa unakosa unaamua kuchoma napia unateka engeine unatuambia tuzikomboe kwapesa nyavu umechoma nipigokubwa nyavu halali yenye leseni kwakuonyesha umefata pesa unateka na engeine unasema tuzikomboe inauma sana mpaka sasa wanazo
 
Aliyeisoma tafadhali naomba atufupishie kwa neno moja au mawili.
Eti uongozi haujaribiwi, hivyo watanzania walikosea kumpa uongozi mwl Nyerere kwa kuwa alikuwa hajapata hata uhead Master.
.
 
Unaandika mambo meengi lakini mshachelewa. Wananchi wameshachoka na ahadi hewa.

Mashirika ya pensheni yanakufa hayana pesa nyie mnanunua ndege kwa cash money.

Wacha tuwaweke hawa ambao tutawamudu. Mgombea wa CCM ameshasema yeye hapangiwi ni rais anayejiamini. Sisi tunamchagua mwananchi mwenzetu Tundu Lissu ili tukae chini tushauriane kwa pamoja tujenge nchi yetu.
 
Upende usipende Lissu hana uwezo wa kuongoza na hatakuja kuwa Rais wa nchi hii. Na hata huko kwenye chama chake hana uwezo wa kuwa Mwenyekiti wa hiko chama. Ni suala la muda tu, ila siku moja tutaongea lugha moja na tutaelewena vizuri.
 
Tatizo lako ni mchanganyo mchanganyo, kwa hiyo ni rahisi kuyachanganya yale uliyojifunza. Lugha mbili ndani ya Aya moja, mimi sijakuelewa bado!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…