Watanzania waishio Marekani kwanini wasirudishwe nyumbani wakiwa na pingu mikononi kama wenzao wa Brazil na Mexico

Watanzania waishio Marekani kwanini wasirudishwe nyumbani wakiwa na pingu mikononi kama wenzao wa Brazil na Mexico

Serikali ya Mexico hapo juzi iliikatalia ruhusa ndege ya kijeshi ya Marekani kutua nchini humo ikiwa na abiria wenye asili ya nchi hiyo waishio Marekani. Hatua hiyo ni baada ya kuapishwa kwa raisi Donald Trump japo huko nyuma ilikwishawahi kuwapokea raia hao kwa mikono miwili ikiwaona kama tunu ya kuongeza vipaji nchini mwao.

Kwa upande wa Brazili hapo juzi pia imetoa lawama kali kwa serikali ya Marekani kupitia waziri wake wa mambo ya nje kufuatia abiria 88 kuingizwa nchini humo kinyemela wakiwa na pingu mikononi.

Vyovyote vile itakavyokuwa kwa upande wangu ningependa kujua Watanzania waishio Marekani je, hawana sifa kama hizo kwa utawala wa Donald Trump.

Kwa maneno mengine jee watanzania hao wana sifa gani za kuendelea kubaki Marekani na kukwepa kurudishwa nyumbani kama wenzao wa Marekani ya kusini
Utakuwa una matatizo yako binafsi.

Trump yupo very clear kwamba utawala wake utafanya Forceful Deportations kwa Wahamiaji haramu ambao hawana vibali halali vya kuishi katika nchi hiyo ya Marekani.
 
Kwani zinatakiwa wapeleke wapi mkuu?
Nadhani ni ushamba, 2011 vijana wa Kitanzania walipata fursa za kuwa walimu wa Kiswahili. Kila Jimbo la US alipelekwa kijana mmoja.
Kumbe jamaa walikuwa wanawazoom mienendo yao. Baada ya mwaka mmoja walitimuliwa wote akabakishwa mmoja tu.
Kisa jamaa walikuwa busy na starehe
 
Nadhani ni ushamba, 2011 vijana wa Kitanzania walipata fursa za kuwa walimu wa Kiswahili. Kila Jimbo la US alipelekwa kijana mmoja.
Kumbe jamaa walikuwa wanawazoom mienendo yao. Baada ya mwaka mmoja walitimuliwa wote akabakishwa mmoja tu.
Kisa jamaa walikuwa busy na starehe
Kwani mtu akitumia pesa yake anavyotaka mwenyewe, mwingine inamhusu nini? Yani mtu asake mshiko wake nani ana mamlaka ya kumpangia? Hiyo mienendo itakuwa kuhusu kazi sio pesa zao I guess, ukistarehe na kusahau kazi hilo ni lako mwenyewe ila kusema watu wanastarehe kwa pesa zao sidhani kuna mtu ana haki ya kuuliza au kujudge!
 
Nadhani ni ushamba, 2011 vijana wa Kitanzania walipata fursa za kuwa walimu wa Kiswahili. Kila Jimbo la US alipelekwa kijana mmoja.
Kumbe jamaa walikuwa wanawazoom mienendo yao. Baada ya mwaka mmoja walitimuliwa wote akabakishwa mmoja tu.
Kisa jamaa walikuwa busy na starehe
Hamna kitu kama hicho kilitokea. Kwanza hiyo program haijawahi kupeleka Watanzania kila jimbo la Marekani kufundisha kiswahili mwaka wowote tangu imeanzishwa. Huwa wanapelekwa ktk vyuo ambavyo vinataka na vinakidhi vigezo vya kushiriki ktk hiyo program - haijalishi majimbo vilipo hivyo vyuo.
Halafu ni starehe gani wangeweza kufanya mpaka kufukuzwa wote akabaki mmoja kwa pesa ndogo ya kujikimu ambayo huwa wanalipwa ktk hiyo program - huku wakiwa mbalimbali kila mmoja wao akiishi ktk mazingira tofauti tofauti in terms of cost of living?
 
Wanaorudishwa ni wahamiaji haramu na ni kutoka mataifa yote.

Wahamiaji haramu ni mzigo kwa pesa za walipa kodi & matukio ya kihalifu.

Jifunze kudadisi jambo kabla hujaandika shauri ya wivu.

Kwani wewe kuna mtu alikuzuia kufika Marekani kihalali?
 
Msalimi
Mkuu,

Unapenda kuona Watanzania wanarudishwa mpaka wakiwa hawarudishwi unauliza kwa nini hawarudishwi?

Watu wengi wana visa halali, wengine wamechukua green cards na mpaka uraia wanaishi kisheria ndiyo maana unaona hawarudishwi.

Mfano mimi nimechukua uraia miaka mingi, nafanya kazi, nalipa kodi, sina tatizo lolote na sheria za nchi, ninachangia uzalishaji vizuri, nina biadhara zangu zinajulikana, sasa Trump atanirudisha wapi na mimi nishatia nanga hapa na kesi ya kunivua uraia hana?

Na kuna wengine wengi kama mimi, na hata hao ambao hawana visa halali au uraia, kama haeana kesi au hawapi katika raid, kufikiwa na Trump si rahisi.
Msalimie EBM
 
Sio Roho Mbaya. Watanzania wengi sana wanaokwenda Ulaya na Marekani iwe kihalali au kimchongo huwa hawana faida kwa Taifa wala ndugu zao. Hawajali wala kukumbuka kwao na hawatoi connection kwa wenzao.(ubinafsi, Roho Mbaya na kukosa uzalendo). Mkenya akitoka na kufanikiwa lazima awekeze kwao, mkenya akitoka lazima avute wenzake wa kutosha tu.

NAUNGA MKONO WABONGO WARUDISHWE MAANA HAWANA FAIDA HATA KWA FAMILIA NA JAMAA ZAO.

NAJUA NA WEWE NI MMOJA WAO
Wewe una faida gani kwenye hili taifa?

Zaidi ya kunya na kujaza choo.
 
Unataka vanessa mdee atimuliwe?
Rotimi abaki na nani sasa?
 
Hivi kiusalama hili limekaaje?
Watu wanasafirishwa huku wamefungwa minyororo mikono na miguu?
Vipi kama ikitokea ajali,wataweza kujisaidia kwa lolote lile? wataweza kuvaa life jacket au Oxygen?

Hao watu walikua na threat gani wakati tayari wapo chini ya ulinzi na wamesha ingia ndani ya Ndege?
 
Back
Top Bottom