Watanzania wajinga na kuvuna wanayopanda

Watanzania wajinga na kuvuna wanayopanda

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Tanzania ni nchi ya aina yake kulinganisha na zingine zote duniani. Kwa hakika ni halali wengine kuiita kuwa ni nchi ngumu sana.

Chukua muda uisome nchi hii kupitia kwa watu wake. Zanzibar wanaweza kuwa tofauti, lakini si bara.

Inasikitisha kuwa Tanzania bara ni jamii ya watu waliojaa ubinafsi, wivu, choyo, husuda, fitna, ujinga, na ujuaji uliopitiliza.

Watu wamekaa kichawi chawi kwamba mafanikio ya mwingine ni mwiba kwao. Watu wapo kusubiria anguko la mwingine ili wapate kufanya sherehe.

Inapiganiwa katiba mpya vipi kwenye jamii hii? Zinapiganiwa haki zipi kwenye jamii hii?

Matokeo yake ni tuyaonayo kutokea kwa CAG, wanavuna waliyopanda. Walisema waungwana hadi akili ziwakae sawa.

Waone wanaojifanya kuwa ni wapigania haki na u ndumila kuwili wao.

Ni Tanzania tu ambako si waziri Nchemba peke yake, bali hata mwananchi kapuku wa Makambako huko, anauthubutu wa kumchagiza mwingine akiwamo asiyemjua kuhamia Burundi.

Siyo bure tuna matatizo makubwa labda kuliko tunavyo fikiria.

Inaweza kuwa ni muhimu sasa tukajitathmini, labda kwa makini zaidi.

Wenye kuutuhumu mwenge wanaweza kuwa na hoja, wasikilizwe!
 
reet.jpg
 
Tanzania ni nchi ya aina yake kulinganisha na zingine zote duniani. Kwa hakika ni halali wengine kuiita kuwa ni nchi ngumu sana.

Chukua muda uisome nchi hii kupitia kwa watu wake. Zanzibar wanaweza kuwa tofauti, lakini si bara.

Inasikitisha kuwa Tanzania bara ni jamii ya watu waliojaa ubinafsi, wivu, choyo, husuda, fitna, ujinga, na ujuaji uliopitiliza.

Watu wamekaa kichawi chawi kwamba mafanikio ya mwingine ni mwiba kwao. Watu wapo kusubiria anguko la mwingine ili wapate kufanya sherehe.

Inapiganiwa katiba mpya vipi kwenye jamii hii? Zinapiganiwa haki zipi kwenye jamii hii?

Matokeo yake ni tuyaonayo kutokea kwa CAG, wanavuna waliyopanda. Walisema waungwana hadi akili ziwakae sawa.

Waone wanaojifanya kuwa ni wapigania haki na u ndumila kuwili wao.

Ni Tanzania tu ambako si waziri Nchemba peke yake, bali hata mwananchi kapuku wa Makambako huko, anauthubutu wa kumchagiza mwingine akiwamo asiyemjua kuhamia Burundi.

Siyo bure tuna matatizo makubwa labda kuliko tunavyo fikiria.

Inaweza kuwa ni muhimu sasa tukajitathmini, labda kwa makini zaidi.

Wenye kuutuhumu mwenge wanaweza kuwa na hoja, wasikilizwe!
''One man fall is another man gain''
wacha Nature ifuate mkondo wake
 
Tunataka Katiba Mpya SOON
Ndani ya katiba hiyo
1. pasiwepo na Mtu atakayekuwa Juu ya sheria.
2. Mahakama Iwe huru, Tume ya Uchaguzi iwe Huru, na Wananchi wawe huru kueleza maoni yao.
3. Mamlaka ya raisi yapunguze.
4. Raisi akifa Uchaguzi ufanyike upya nchi nzima baada ya siku 90 ,Makamu wa raisi akaimu uraisi kwa siku hizo.Lakini ikiwa yeye ana nia ya kugombea uraisi basi asikaimu nafasi hiyo ,badala yake Raisi wa Zanzibar akaimu nafasi hiyo kwa muda huo tajwa.
5. kabla ya Ucha guzi wowote ule wa raisi. Jaji mkuu akaimu nafasi ya Raisi kwa miezi Mitatu ili raisi Aliyepo Madarakani awe huru kujishughulisha na kampeni.Isitokee Raisi aliye Madrakani kuendelea kuwa Mgombea huku akiwa Bado raisi.
 
Tunataka Katiba Mpya SOON
Ndani ya katiba hiyo
1. pasiwepo na Mtu atakayekuwa Juu ya sheria.
2. Mahakama Iwe huru, Tume ya Uchaguzi iwe Huru, na Wananchi wawe huru kueleza maoni yao.
3. Mamlaka ya raisi yapunguze.
4. Raisi akifa Uchaguzi ufanyike upya nchi nzima baada ya siku 90 ,Makamu wa raisi akaimu uraisi kwa siku hizo.Lakini ikiwa yeye ana nia ya kugombea uraisi basi asikaimu nafasi hiyo ,badala yake Raisi wa Zanzibar akaimu nafasi hiyo kwa muda huo tajwa.
5. kabla ya Ucha guzi wowote ule wa raisi. Jaji mkuu akaimu nafasi ya Raisi kwa miezi Mitatu ili raisi Aliyepo Madarakani awe huru kujishughulisha na kampeni.Isitokee Raisi aliye Madrakani kuendelea kuwa Mgombea huku akiwa Bado raisi.

Mapendekezo mazuri kabisa lakini wadau kwenye kuyapigania hayo ni watanzania hawa:

"waliojaa ubinafsi, wivu, choyo, husuda, fitna, ujinga, na ujuaji uliopitiliza."

cc: Yonda
 
Back
Top Bottom