Watanzania wanawaza kumtukuza mtu au Rais kuliko taifa lenyewe

Watanzania wanawaza kumtukuza mtu au Rais kuliko taifa lenyewe

Nkerebhuke

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2021
Posts
796
Reaction score
2,026
Huwa nakaa najiuliza nani alituletea hili balaa maana imefika kipindi unaona kabisa jinsi gani watanzania wanashindwa kujali na kathamini taifa lau zaidi ya umaarufu binafsi wa kiongozi mkubwa wa nchi. Tabia ya viongozi kujenga umaarufu binafsi kuliko hata taifa lenyewe limezaa balaa kwenye nchi yetu maana kumezaa machawa na walamba asali ambao wanaamini kiongozi hakosei na wala hapaswi kuelekezwa jambo.

Pia soma: Watanzania wanawaza kumtukuza mtu au Rais kuliko taifa lenyewe

Kama kuna muhasisi wa hili jambo ametuletea balaa maana watu wetu hawataki tena kuelimika na kujifunza wanapenda kusikia nani kakosea, nani kasema hivi au nani katumbuliwa. Zinaimbwa nyimbo nyingi za kumtukuza raisi kuliko hata taifa lenyewe ambalo ndio msingi wa hatma ya kizazi kijacho.

Taifa letu linapita kwenye hali ngumu ya mfumuko wa bei, elimu yetu kudumaa, ukosefu wa ajira kupita kiasi na changamoto tele cha ajabu tuko bize kusifia na kulaumu viongozi wakuu waliopo na waliopita. Tumejaa ubinafsi, uroho, ujuaji na ujinga wa kuwasujudia viongozi badala ya kuwapa changamoto ili kuwaonesha tunataka nini kwa future ya watoto wetu. Watanzania tubadilike.
 
Hii kitu ilianzia Kwa magufuli inaboa,unaangalia Habari, Kila anaezungumza anasema kauli inayofanana,"tunamshukiri mama Samia Kwa madarasa, tunamshukuru mama Samia Kwa daraja"hata viongozi nao hivo hivo.hadi watoro wa shule hivo hivo. Uzalendo uchwara.
 
Kama kuna muhasisi wa hili jambo ametuletea balaa maana watu wetu hawataki tena kuelimika na kujifunza wanapenda kusikia nani kakosea, nani kasema hivi au nani katumbuliwa. Zinaimbwa nyimbo nyingi za kumtukuza raisi kuliko hata taifa lenyewe ambalo ndio msingi wa hatma ya kizazi kijacho.
Maneno mazito sana kama mwanaadamu mwenye kufahamu. Mwananchi anajita chawa kwa kiongozi alie mchagua tena kiongozi amejiwekea kinga akikosea asiende jela. Chawa yeye atakwenda jela na familia yake
 
Maneno mazito sana kama mwanaadamu mwenye kufahamu. Mwananchi anajita chawa kwa kiongozi alie mchagua tena kiongozi amejiwekea kinga akikosea asiende jela. Chawa yeye atakwenda jela na familia yake
Hali hii imesababisha kama taifa tukose wazo la pamoja ili kuonesha kiu na nini tunataka hasa kwenye maishe yetu. Hivi sasa kila mtu anaongea la kwake, huyu anasifia yule anaponda. Nchi yetu kuna monopoly watu hawataki kujua wao wanaimba mapambio yao ya kusifu na kuabudu. Kila sehemu kumeshikwa na mabig fish hakuna sehemu vijana wanaweza kujiajiri waka survive competition wanaishia kufa na vipaji vyao.
 
Ubinafsi na ujinga ndio chanzo chake, unasababishwa na njaa na kujipendekeza.
 
Muasisi wa hili jambo ni Mwl. Nyerere...alikuwa anasifiwa sana na alikuwa anapenda sana hilo.
 
Ndio maana kilio kikubwa cha watanzania wengi wenye akili ni kupunguza madaraka ya Rais kikatiba.Kitendo cha Rais kuteua 70% ya viongozi au kuwa na influence ya watu kupata vyeo automatically imesababisha watu kuwa machawa wa Rais ili wakumbukwe kwenye teuzi.Iko wazi ili mtu ajihakikishie kuwa mgombea hata wa ubunge lazima awe mtu wa kujikomba kwa mwenyekiti wa chama .Na akiwa ni mtu wa kumcrisize atakuwa yupo kwenye hatari ya kutopitisha atakapoomba udhamini wa chama ili agombee.Tusipobadili katiba yetu machawa watazidi ongezeka kila iitwapo leo mpaka tushindwe kuwathibiti
 
Back
Top Bottom