Watanzania wangapi wameshatajirika kupitia kilimo cha korosho?

Watanzania wangapi wameshatajirika kupitia kilimo cha korosho?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Inaonekana ni kati ya mazao yanayouzwa ghali sana. Sisi tunaoishi mikoa ya mbali na korosho inakolimwa, tumekuwa tukiuziwa korosho za kutafuna kwa bei isiyobadilika, miaka nenda miaka rudi. Kwa bei tunayouziwa mitaani na supermarket, inatoa picha kuwa ni bidhaa ghali kuzidi karanga, n.k.

Lakini sijawahi kusikia mtu ambaye amekuwa bilionea au hata milionea kupitia kilimo cha korosho.

Ni kwamba hawapo au wahusika wanajitahidi kujizuia wasijulikane?

Korosho ni ghali Tanzania, na inasemekana, huko ng'ambo, bei yake "haikamatiki"

Kulikoni hatuwasikii mabilionea waliotokana na kilimo cha korosho?
 
Angekuwepo JPM angekujibu, thesis yake ya PHD ilihusu Korosho, ndio maana alidiriki kutumia Jeshi kufanya biashara ya korosho.

Zitto kabwe ana mahekari ya mashamba ya korosho alihama from Tabata to Masaki Sababu ya Korosho.

Korosho ni dhahabu inayopandwa.
 
Kuna mtanzania juzi akiwa Canada aliomba kazi kiwanda cha yeboyebo, jibu la mchina akamwambia kuwa mshahara Kwa mwezi ni shilingi 5000 akashangaa sana huyu mtanzania akasema mbona mshahara mdogo sana Kwa maisha ya Tanzania?

Mchina akamwambia Sisi tulitaka tumlipe kila mfanyakazi shilingi 20000 Kwa siku LAKINI MAWAZIRI wa Tanzania wamewaambia walipeni fedha hiyo hiyo inatosha. Sasa mtoa mada ukisoma comment yangu utaelewa namna watawala wa CCM wanavyofikiri.
 
Inaonekana ni kati ya mazao yanayouzwa ghali sana. Sisi tunaoishi mikoa ya mbali na korosho inakolimwa, tumekuwa tukiuziwa korosho za kutafuna kwa bei isiyobadilika, miaka nenda miaka rudi. Kwa bei tunayouziwa mitaani na supermarket, inatoa picha kuwa ni bidhaa ghali kuzidi karanga, n.k.

Lakini sijawahi kusikia mtu ambaye amekuwa bilionea au hata milionea kupitia kilimo cha korosho.

Ni kwamba hawapo au wahusika wanajitahidi kujizuia wasijulikane?

Korosho ni ghali Tanzania, na inasemekana, huko ng'ambo, bei yake "haikamatiki"

Kulikoni hatuwasikii mabilionea waliotokana na kilimo cha korosho?

Njoo Newala huku utakuta mamilionea kibao wa korosho
 
Angekuwepo JPM angekujibu,thesis yake ya PHD ilihusu Korosho,ndio maana alidiriki kutumia jeshi kufanya biashara ya korosho.
Zitto kabwe ana mahekari ya mashamba ya korosho alihama from Tabata to Masaki Sababu ya Korosho.

Korosho ni dhahabu inayopandwa
Kumbe wamo🙏
 
Kuna mtanzania juzi akiwa Canada aliomba kazi kiwanda cha yeboyebo ,jibu la mchina akamwambia kuwa mshahara Kwa mwezi ni shilingi 5000 akashangaa sana huyu mtanzania akasema mbona mshahara mdogo sana Kwa maisha ya Tanzania?Mchina akamwambia Sisi tulitaka tumlipe kila mfanyakazi shilingi 20000 Kwa siku LAKINI MAWAZIRI wa Tanzania wamewaambia walipeni fedha hiyo hiyo inatosha ,Sasa mtoa mada ukisoma comment yangu utaelewa namna watawala wa CCM wanavyofikiri
Aisee!!!
 
Angekuwepo JPM angekujibu, thesis yake ya PHD ilihusu Korosho, ndio maana alidiriki kutumia Jeshi kufanya biashara ya korosho.

Zitto kabwe ana mahekari ya mashamba ya korosho alihama from Tabata to Masaki Sababu ya Korosho.

Korosho ni dhahabu inayopandwa.
🙏
 
Brother kila msimu hupata milioni 20 akishuka milioni 15.
Wengi wanaipata pesa ndefu ila naona elimu ya matumizi sahihi ya pesa ni tatizo kwa wengi.
Vijana wa Lindi na Mtwara milioni 2, 3, 4 wanapata sana kupitia ufuta na korosho ila wengi huishia kununua mapikipiki tu
 
Ili uone faida kwenye korosho inabidi uwe na miti sio chini ya kati ya 500_600. Hapo nazungumzia ekari 20 za shamba zilizotunzwa vizuri

Sasa wengi hawana mashamba ya ukubwa huo unakuta mtu ana ekari 3 mpaka tano na zinamtesa kuhudumia

Ilaa wachache wenye kupiga pesa wana ekari mpaka 200
 
Brother kila msimu hupata milioni 20 akishuka milioni 15.
Wengi wanaipata pesa ndefu ila naona elimu ya matumizi sahihi ya pesa ni tatizo kwa wengi.
Vijana wa Lindi na Mtwara milioni 2, 3, 4 wanapata sana kupitia ufuta na korosho ila wengi huishia kununua mapikipiki tu
Soma comment kama hii halafu ujichanganye uende kufungua duka kubwa huko ukidhani vijana wa Mtwara na Lindi milioni 2, 3, 4, siyo issue, ndiyo utakiona.
 
Brother kila msimu hupata milioni 20 akishuka milioni 15.
Wengi wanaipata pesa ndefu ila naona elimu ya matumizi sahihi ya pesa ni tatizo kwa wengi.
Vijana wa Lindi na Mtwara milioni 2, 3, 4 wanapata sana kupitia ufuta na korosho ila wengi huishia kununua mapikipiki tu
Hizo milioni 20 zinatokana na ekari ngapi?
 
Inaonekana ni kati ya mazao yanayouzwa ghali sana. Sisi tunaoishi mikoa ya mbali na korosho inakolimwa, tumekuwa tukiuziwa korosho za kutafuna kwa bei isiyobadilika, miaka nenda miaka rudi. Kwa bei tunayouziwa mitaani na supermarket, inatoa picha kuwa ni bidhaa ghali kuzidi karanga, n.k.

Lakini sijawahi kusikia mtu ambaye amekuwa bilionea au hata milionea kupitia kilimo cha korosho.

Ni kwamba hawapo au wahusika wanajitahidi kujizuia wasijulikane?

Korosho ni ghali Tanzania, na inasemekana, huko ng'ambo, bei yake "haikamatiki"

Kulikoni hatuwasikii mabilionea waliotokana na kilimo cha korosho?
Wapo wengi tu ila hawataki kujitangaza mitandaoni. Kwa kuwa wenyewe hawajitangazi basi nami naficha majina yao ila ukitaka kujuwa ukweli fika Mtwara, Tandahimba, Nachingwea, Ndanda,, Masasi, Tunduru, Newala, na sehemu zingine za Kusini ukajionee matajiri wa huko.
 
Kuna mtanzania juzi akiwa Canada aliomba kazi kiwanda cha yeboyebo, jibu la mchina akamwambia kuwa mshahara Kwa mwezi ni shilingi 5000 akashangaa sana huyu mtanzania akasema mbona mshahara mdogo sana Kwa maisha ya Tanzania?

Mchina akamwambia Sisi tulitaka tumlipe kila mfanyakazi shilingi 20000 Kwa siku LAKINI MAWAZIRI wa Tanzania wamewaambia walipeni fedha hiyo hiyo inatosha. Sasa mtoa mada ukisoma comment yangu utaelewa namna watawala wa CCM wanavyofikiri.
Yaani adui wetu tunae hapahapa!!!!!
 
Wapo wengi tu ila hawataki kujitangaza mitandaoni. Kwa kuwa wenyewe hawajitangazi basi nami naficha majina yao ila ukitaka kujuwa ukweli fika Mtwara, Tandahimba, Nachingwea, Ndanda,, Masasi, Tunduru, Newala, na sehemu zingine za Kusini ukajionee matajiri wa huko.
Sawa mkuu. Nitafanya hivyo.
 
Wapo wengi tu mbona

Mfano nakupa na jina yuko mzee

Wangu mmoja yuko kiwangwa,ana deal na nanasi anaitwa mzee mikugo
Huyo ni hatari sana kifedha yuko vzr sana hata wakati wa utawala ule mambo ya kuchungulia ac walishanga
Kuona mtu Ana mpunga wa mrefu,mzee akawambia yeye mkulima tu

Ova
 
Kuna mtanzania juzi akiwa Canada aliomba kazi kiwanda cha yeboyebo, jibu la mchina akamwambia kuwa mshahara Kwa mwezi ni shilingi 5000 akashangaa sana huyu mtanzania akasema mbona mshahara mdogo sana Kwa maisha ya Tanzania?

Mchina akamwambia Sisi tulitaka tumlipe kila mfanyakazi shilingi 20000 Kwa siku LAKINI MAWAZIRI wa Tanzania wamewaambia walipeni fedha hiyo hiyo inatosha. Sasa mtoa mada ukisoma comment yangu utaelewa namna watawala wa CCM wanavyofikiri.
Hii Ni kweli kabisa. Wakanada walipokuja Bulyanhulu walikua tayari kulipa MISHAHARA ya kufa mtu. Wakuu wa wilaya na mkoa walipoona hiyo MISHAHARA Ni zaidi ya MISHAHARA wanayolipwa na serikali walitia timu pale Bulyi na kuwashawishi wakanada wafyeke hiyo MISHAHARA.
CCM ndio janga la nchi hii.
Ukija kwenye korosho sote twakumbuka mwendazake alivyowafanya wamakonde. Halafu akaleta mkenya mhuni wakaketi na Prof mhuni kalamaganda kule Arusha, mkenya kaingia mitini mpaka korosho zikaoza.
Niambie mwendazake alumteteaje mkulima? CCM inamtaka mkulima apumue tu ili aweze kupiga kura na kulipa Kodi vinginevyo........
 
Back
Top Bottom