Watanzania wengi wamekaa kiwiziwizi tu halafu cha ajabu wanashinda makanisani

Watanzania wengi wamekaa kiwiziwizi tu halafu cha ajabu wanashinda makanisani

Chikenpox

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2022
Posts
784
Reaction score
1,246
Watanzania wamekaa kiwizi wizi haijalishi ni mapasta, Madre, maaskofu au waamini. Ukitaka kujua Hilo mlemle kanisani dondosha elfu kumi halafu unifanye hujaiona nakwambia hata yule aliyekuwa ananena kwa lugha kwa Julia kabisa akiiona atachukua fasta na hakupi.

Kila siku watu wanashinda makanisani lakini wizi umeongezeka wa simu, radio, pesa nk na wanaoiba wengi ni Hawa wanaonena kwa lugha na wizi huo kuupa jina zuri eti mungu ameamua kumpa kwa njia ya kumnyanganya mwingine.
 
Kumbuka katika msafara wa mamba hawakosekani kenge. Ila wewe kwa makusudi umeamua kupeleka lawama kwa mamba wote pasipo hata kutaka kuelekeza lawama hizo kwa kenge ambao hasa ndiyo wenye kuhusika.

Haya bana.
 
"Wanaoiba wengi ni hawa wanaonena kwa lugha"

Kwa nukuu hiyo hapo juu ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Sijui wewe una imani gani ya kiroho, lakini kukufuru kazi za Roho wa Kristo ni laana kubwa sana. Unaweza kuandika uzi kwa uhuru wa matumizi ya maneno yoyote yale, lakini yale mazuri na ya staha hukufanya kujiepusha na dhambi.

Tambua tu kuwa nukuu ya maneno hayo hapo juu ni kuonyesha kuwa una kiburi cha uzima. Enenda katika kicho mbele ya Mungu na vitu vyake vitakatifu, kwa kuwa ndiye pekee mwenye kutambua kesho yako.
 
Watu weusi Ni version ya wanyama
Alisikika mzungu mmoja
 
Watanzania wamekaa kiwizi wizi haijalishi ni mapasta, Madre, maaskofu au waamini. Ukitaka kujua Hilo mlemle kanisani dondosha elfu kumi halafu unifanye hujaiona nakwambia hata yule aliyekuwa ananena kwa lugha kwa Julia kabisa akiiona atachukua fasta na hakupi.

Kila siku watu wanashinda makanisani lakini wizi umeongezeka wa simu, radio, pesa nk na wanaoiba wengi ni Hawa wanaonena kwa lugha na wizi huo kuupa jina zuri eti mungu ameamua kumpa kwa njia ya kumnyanganya mwingine.
Ubovu wa mada yako ni kwamba hutofautishi kati ya "waTanzania" na waTanzania ambao siyo wakristo.

WaTanzania wote umewarundika kwenye hilo kundi moja tu, ambayo siyo kweli.

Kwa hiyo mada yako ni ya hovyo!
 
Back
Top Bottom