Watanzania wote tuanze mapema Kujiandaa Kisaikolojia kwa lolote lile ambalo huenda tukalisikia Kuanzia Saa 4 Kamili Usiku wa leo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Tukifanikiwa sawa ila tukianguka basi tusianze Kulaumiana wala Kununiana au hata Kuwatafuta Wachawi. Ombi langu tu nawaomba Wahusika Siku za baadae wanijumuishe An Eagle katika Kamati ya Fitna na Umafia ( Roho Mbaya Iliyokithiri na Isiyo na Huruma kwa Wageni ) dhidi ya Wageni wanaokuja Kupambana nasi hapa Temeke kwani nina uhakika kila atakayeingia hatotoka salama kuliko ilivyo sasa Wageni wanakuja na ' wanatupiga ' hapa hapa Kisha wanatupa Mlima Mrefu wa Kupanda pale tukienda Kwao.

Kama tulimweza ' Mwarabu ' wa mbali huko Misri na ' akapigwa ' tena vizuri tu hapa Temeke ilikuwaje tukamshindwa ' Mwarabu Koko ' tena ambaye hata hatoki mbali nasi Kijiografia hapo tu juu ya Uganda na ' akatuumiza ' hapa hapa Nyumbani? Na kinachonima zaidi An Eagle ni kwamba Wao huko nchini Kwao hali ya Amani si nzuri ( wanapitia Kipindi cha Mpito Kiutawala ) wakati huku Sisi Tanzania tupo Shwari hakuna Shari halafu hapo hapo ' wanatutenda ' vibaya.

Niliumia sana na bado pia naumia mno. Nipeni hilo ' Jukumu ' Watanzania mfurahi kwa kila ajaye nchini.
 
Usihofu
Tutawaonyesha upepo wa kisulisuli unavyo tenda muujiza
 
Hivi kwani tunaruhusiwa kufanyia sherehe hii kwao,,maana nasikia waandaaji wa hii sherehe wanatafutaga uwanja huru kwa sababu kwao bado hali si shwari..
 
Hata siwezi jitia umwambafai

sijaelewa kitu
 
October 18, 2019
LIVE:
Live match second half:

Full time : Results

Sudan 1 - 2 Tanzania CHAN-2020

Ditram Nchimbi goli lake dakika ya 76 yaipa ushindi ugenini Tanzania ktk mashindano kuelekea fainali za CHAN 2020 zitakazofanyika Cameroon

 
Live match second half:

Full time : Results

Sudan 1 - 2 Tanzania CHAN-2020

Ditram Nchimbi goli lake dakika ya 76 yaipa ushindi ugenini Tanzania ktk mashindano kuelekea fainali za CHAN 2020 zitakazofanyika Cameroon

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…