Huyu jamaa aliyejirekodi akioga na kuvunja nazi katikati ya barabara aliona hii ndio njia sahihi ya kuchekesha? Hapana, huu ni ujinga na hatari.
Kwanza, anachafua barabara kwa mabaki ya nazi na maji, akiharibu miundombinu. Pili, amesababisha foleni kwa madereva waliolazimika kusimama au kupita kwa tahadhari.
Zaidi ya hayo, anavunja sheria za usalama barabarani. Kitendo chake kilisababisha mkusanyiko wa watu eneo lisilo salama. Barabara ni mali ya umma kwa usafiri, si mahali pa kufanya maigizo kiholela.
Mtu akipata ajali kwa sababu ya vitendo hivi, nani wa kulaumiwa? Tabia za kujitafutia matatizo halafu tunailaumu serikali kwa uzembe wetu.
TANROADS na mamlaka husika zinapaswa kuchukua hatua kama funzo kwa wengine wenye tabia kama hizi. Au nyie mnaonaje, Wakuu?
Mbona anaerekodi na anaeoga hawapo pamoja? Na wanaorekodi ni wengi tu, huyo hatengenezi content, kachotwa tu akili kwamba afanye hivyo atafanikiwa. Ni uwendawazimu, ni ugonjwa wa akili tu.