Watengeneza content za kuoga au kuvunja vitu kwenye barabara zenye foleni kubwa wachukuliwe hatua, wataleta maafa!

Watengeneza content za kuoga au kuvunja vitu kwenye barabara zenye foleni kubwa wachukuliwe hatua, wataleta maafa!

Huyu jamaa aliyejirekodi akioga na kuvunja nazi katikati ya barabara aliona hii ndio njia sahihi ya kuchekesha? Hapana, huu ni ujinga na hatari.

🤣🤣🤣
Hakika sio kila mtu anajua kila kitu cha duniani

Ni kama hivi

Mtu unapoenda kusali na kutoa sadaka naye huyo hiyo ndio njia yake ya maishani ili apae.

Kila mtu anaishi kivyake ndio maana tunaangalia na kupita
 
Mitandao imewafanya watu wamekuwa vichaaa
Kila kijana anataka kuwa content creator ,ujinga mwingiii

Ova
 
Wakuu mpo vizuri?

Huyu jamaa aliyejirekodi akioga na kuvunja nazi katikati ya barabara aliona hii ndio njia sahihi ya kuchekesha? Hapana, huu ni ujinga na hatari.

Kwanza, anachafua barabara kwa mabaki ya nazi na maji, akiharibu miundombinu. Pili, amesababisha foleni kwa madereva waliolazimika kusimama au kupita kwa tahadhari.

Zaidi ya hayo, anavunja sheria za usalama barabarani. Kitendo chake kilisababisha mkusanyiko wa watu eneo lisilo salama. Barabara ni mali ya umma kwa usafiri, si mahali pa kufanya maigizo kiholela.

Mtu akipata ajali kwa sababu ya vitendo hivi, nani wa kulaumiwa? Tabia za kujitafutia matatizo halafu tunailaumu serikali kwa uzembe wetu.

TANROADS na mamlaka husika zinapaswa kuchukua hatua kama funzo kwa wengine wenye tabia kama hizi. Au nyie mnaonaje, Wakuu?

View attachment 3206099
Watasema "msiwazuie huko ndiyo kujiajiri kwenyewe" sijui wao kama wanaweza kuoga hivyo
 
Si kwamba yuko ibadani?Kwa kawaida huwa tunafanyia njia panda nyakati za usiku wa manane na hivyo tustahimiliane tu.Watu wanakesha usiku wakiomba kwa msaada wa vipaza sauti,ni kero lakini tunavumiliana.
 
Hao Tanroads kwani hawaogopi kurogwa 😅😅😅
 
Back
Top Bottom