Uchaguzi 2020 Watia nia wengi 2020 bomu jipya kwa CCM | wataiangusha CCM 2025

Uchaguzi 2020 Watia nia wengi 2020 bomu jipya kwa CCM | wataiangusha CCM 2025

Wingi wa wagombea CCM ni dalili mbaya sana, kwa sababu ndio inaleta hatari kubwa sana ya "MPASUKO MKUBWA" ndani ya chama pindi watakapo katwa majina walio wengi wao (Asilimia kubwa ya hawata ridhika pindi panga likipita).

Sasa chukua hao watakao kutana na "PANGA", jumlisha "WAFANYABIASHARA (Waliofilisiwa/Tapeliwa/Walioonewa na TRA/BODI YA MADINI), VIJANA WASIO NA AJIRA, WAKULIMA WALIOKAANGWA BEI ZA MAZAO, MADEREVA WALIOBAMKIZIWA FINE BARABARANI (MABASI, BAJAJI, BODABODA, DALADALA), WANANCHI WALIOTOLEWA MANENO YA DHARAU NA VIONGOZI, WANANCHI WALIOBAMBIKIZWA KESI ZA UHUJUMU UCHUMI NA JINAI, WALIOTUMBULIWA, WALIOTEKWA/KUPOTEZWA/KUULIWA.

Usisahau na hasira za wananchi dhidi ya "UTAPELI" uliofanyika kwenye "UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MTAA".

Majibu ya kasheshe watakayokutana nayo CCM #Uchaguzi2020 utayapata.

CCM tatizo lao ni ubishi na kujisifia kupita kiasi, ila kwa wenye akili hio ni dalili ya kushtua sana.
Asante kwa kuongezea,hili bomu halitawaacha salama kabisa ndio itakuwa mwisho wao. Bado wanaomaliza vyuo na hakuna ajira ni hatari sana
 
Form ni laki tu, nimesema wana njaa kutokana na kua hawaridhiki na madaraka waliyonayo. Mfano tu kesho wakitangaza kua ubunge ni kazi ya kujitolea sidhani kama utasikia watia nia
Asante sana kwa jibu,kama unavyosema upepo ukigeuka gafla uRC ugombewe na ubunge uwe ni kaz ya hayari(mshahara mdogo tu) waliokimbia ukuu wa mkoa warudi tena huko huko kama sio njaa ni nini?
 
Safari hii watoto wa nyerere wawili wamejitosa hapo butiama pamoja na ndugu yao mwingine

Siasa ya ccm imeingiliwa


2025 wagombea urais watakuwa 500
 
Ukiona kunguru wengi sehem ujue kuna mzoga.

Kwenye mada: Kwanza kabisa tunapaswa kukumbuka kuwa hii ni rekodi mpya kwa watia nia wa Ubunge.

Katika tafiti za kawaida tu inaonyesha ukosefu wa ajira na kukimbilia maslahi makubwa bila kuwa na sera zenye tija,kweli wote watakuwa na nia ya kuwatumikia watanzania? Kama ndio kwanini mtu aache kazi akatafute kazi? Uache uRC ukagombee ubunge? Kwani huko haukua ukiwatumikia watanzania?.

Watakao katwa pamoja na watakao shindwa ubunge watatoka na hasira kali sana na kutakuwa na wimbi la wakosoaji wengi sana kipindi hichi,kipindi cha utawala wa Magu waliotumbuliwa,wenye vyeti feke wapiga dili wote hao. Jambo ambalo litafanya CCM ichukiwe au kutokeza makundi mengi.

Hitimisho.
Kutokana na vuguvugu hilo lazma wengi wawe na hasira ya kuitoa ccm kwa hali yoyote ile. Kwaio usemi wa Nyerere wa atakaeiangusha CCM ni CCM wenyewe. Ni hayo tu.

(Mchambuzi mdogo wa mambo ya kisiasa na kijamii)
Watu wamechoka na namna rais anavyoongoza nchi kuna vuguvugu la mapinduzi ndani ya ccm sasa hivi taratibu tutaona makubwa.
 
Unajua hadi makamu na rais wamekasirika kweli kweli!
Mpaka kuipa ajenda juzi na kutafuta wasemaji duh!

'Tumeipenda wenyewe!
 
Back
Top Bottom