Watoa huduma shughuli za Usafi na Urembo wanahitajika Dar es Salaam, changamkia fursa sasa

Watoa huduma shughuli za Usafi na Urembo wanahitajika Dar es Salaam, changamkia fursa sasa

FAJES

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2017
Posts
720
Reaction score
644
TANGAZO LA KAZI TAREHE 17, DISEMBA 2020.

BEITO IINTERNATIONAL COMPANY LTD,
tunajihusisha na shughuli za usafi na urembo. Ofisi zetu zipo Dar es Salaam, Wilaya ya Kinondoni, Mwenge, ITV.

Huduma tunazozitoa ni hizi zifuatazo;

USAFI
  • Usafi wa nyumbani wa kila namna kama vile kusafisha ndani na nje ya nyumba, usafi wa masofa, carpets, sehemu za jiko, vyoo/bafu.
  • Kufua nguo na kunyoosha
  • Usafi kwenye nyumba mpya kwa ajili ya kuhamia
  • Usafi kwenye mashule, hospitali, migahawa, makanisa, kumbi za harusi na starehe
  • Gardening
UREMBO
  • Kusuka mitindo aina zote
  • Kunyoa mitindo yote
  • Kutengeneza kucha
  • Kufanya MAKE-UP
  • Matunzo ya ngozi
NAMNA TUNAVYOFANYA KAZI
  • Huduma zetu tunawafuata wateja mahali walipo hasa hasa majumbani kwao.
  • Muda mfupi ujao, wateja wetu watakuwa na uwezo wa kuomba huduma kwa njia za kidijitali (kupitia website na mobile- App) hivyo kwa baadae siyo sasa) watoa huduma wetu watatakiwa kuwa na Smartphone ili kupata acess ya kuwasiliana na Ofisi yetu na wateja wetu.
SIFA TUNAZOTARAJIA KUTOKA KWAKO
  • Uaminifu wako ni sifa kubwa zaidi tunayohitaji
  • Uwe na haiba na tabia njema isiyo na mashaka
  • Mchapakazi na mwenye kujituma
  • Msafi na Mtanashati
  • Mkweli, mcheshi na mkarimu
  • Uwe unaishi sehemu yoyote Dar es Salaam.
  • Ujue kusoma na kuandika
  • Ujue kutumia Smartphone
  • Ujuzi na uzoefu ni muhimu lakini si lazima
    Mwenye experience ya kazi husika angalau kuanzia miezi 6 atapewa kipaumbele.
NAMNA YA KUWASILISHA MAOMBI
  • Fika mwenyewe katika Ofisi zetu zilizopo Mwenge ITV, Bagamoyo road kwa ajili ya usaili mfupi.
  • Fika kati ya Jumatatu hadi Ijumaa; muda kuanzia saa 3 asbh - 10 Jioni.
Mawasiliano: + 255 742 417 677

Fika na nakala zifuatazo.

1.Barua ya maombi ya kazi, ikiainisha aina ya kazi unayohitaji kufanya, unaruhusiwa kuomba kufanya kazi zaidi ya moja kulingana na uwezo wako
Maombi yatumwe kwa;

Mkurugenzi Mtendaji,
BEITO International Company Ltd
S.L.P 391,
Dar es Salaam.


2. Barua ya Utambulisho kutoka Ofisi ya Mtaa

3. Uthibitisho kuwa haujawahi kuhusika na makosa ya jinai kutoka kituo cha Polisi unapoishi (Ni muhimu lakini siyo lazima).

4. Nakala ya kitambulisho cha Taifa (NIDA) au kitambulisho kingine kinachotambulika.
5. Barua ya mdhamini na mawasilino yake ( anaweza kuwa ndugu, mwenza au mzazi).
6. Cheti kama unacho (siyo lazima) chochote kinachoendana na aina ya kazi unayoomba.

MALIPO
  • Watoa huduma wetu watafanya kazi kama Freelancers (kujiajiri) kwa kuwa na mkataba na kampuni ya BEITO International, isipokuwa watoa huduma wa usafi katika sehemu za Ofisi, mashule, vyuo, hospitali n.k ambako majukumu yao ni ya kila siku, wao wataajiriwa kama wafanyakazi wa kudumu.
  • Watoa huduma watakaokuwa wamejiajiri (Freelancers) watapata malipo ya aslimia 70 (70%) ya malipo ya kazi husika.
  • Wafanyakazi wa kudumu watalipwa mshahara kulingana na makubaliano na mwajiri.
NOTE: Tangazo hili limetolewa kuanzia leo tarehe 17 Disemba, 2020. Mwisho wake itategemea na kiasi cha watoa huduma watakaopatikana kwa wakati huo.


UPDATES 22.12 2020

Wahudumu wa Usafi kutoka katika maeneo yafuatayo watapewa kipaumbele:

Tegeta
Kawe
Mbez beach
Kinondoni
Makumbusho
Kigamboni
Tabata

Mwenye experience ya kufanya kazi ya Usafi angalau miezi 6 atapewa kipaumbele.
 
Wakuu nafasi bado zipo karibuni sana. Unaweza kumshtua nduguyo au kijana mwenzio akachangamkia fursa.

OMBI: Naomba wenye nia muda wa kupiga simu ni kuanzia sa 3 asbh hadi sa 10 jioni. Huo ndio muda wa kazi Wakuu.

Halafu naona maswali mengi maelezo yake nimeshaandika yote hapa, hivyo tunatarajia ukipiga simu ni kuwa ushafika maeneo ya ITV mwenge na unahitaji kuuliza kwamba hapo ITV Ofisi ipo wapi.
 
Tunashukuru kwa mlio kwisha kuonesha nia. Milango bado ipo hujachelewa.
 
Vijana wanaohitaji kufanya kazi za usafi na urembo tunawakaribisha. Nafasi bado zipo. Wiki ijayo tunaanza kazi rasmi. Karibuni sana. Msilie lie kwamba kazi hazipo. Fursa ndio hizi zinawahitaji. Mpaka sasa wwmejitokeza vijana wanne tu kupitia Tangazo hili. Bado tunahitaji vijana kuanzia 10 hivi.
 
Tunawashukuru Vijana wa Usafi mliojitokeza. Bado nafasi za vijana wanaohitaji kazi za urembo mnakaribishwa.
 
UPDATES 22.12 2020

Wahudumu wa Usafi kutoka katika maeneo yafuatayo watapewa kipaumbele:

Tegeta
Kawe
Mbez beach
Kinondoni
Makumbusho
Kigamboni
Tabata

Mwenye experience ya kufanya kazi ya Usafi angalau miezi 6 atapewa kipaumbele.
 
Back
Top Bottom