Watoto wa kishua hamuwezi kuielewa hii picha

ohoooo....huwez kuelewa haya maswala mjombaaa.....watu tunacheza kuanzia saa nne asubuh mpka saa kumi na mbili jioni...sasa hapo unategemea nini??
inamaana maswala ya lunch kwenu ilikuwa ni maswala ya kubabaishana?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi nilikuwa sikosi namba nilikuwa monitor majina ya wasumbufu na watoro ninayo mfukoni mkizingua tuu napeleka kwa ticha mkali
 
Nakumbuka nilimaliza godoro nusu kisa kushonea mipira inayodunda.....ilkuwa ukisikia gozi hata kama lipo kata nyingine mtaenda tuu
wenzio tulikua tunaweka kondom....yn ukisuka mpira na kuweka kondom ndani yake....weeeeeee yn hapo hata utamu wa gozi hauoni ndani.......kitu kinadunda freshiiii
 
Mimi nilikuwa sikosi namba nilikuwa monitor majina ya wasumbufu na watoro ninayo mfukoni mkizingua tuu napeleka kwa ticha mkali
heheheh,

kweli kipindi hicho kama sio utumie cheo chako basi namba kwako ione kama sumu.
 
ohoooo....huwez kuelewa haya maswala mjombaaa.....watu tunacheza kuanzia saa nne asubuh mpka saa kumi na mbili jioni...sasa hapo unategemea nini??


Kwa hapo nimekulewa.

Ila ilikuwa raha..nilikuwa natoroka shule (sana sana kaka yangu ndiyo alinifundisha kutoroka) tunaenda uwanja wa Ushirika (Moshi, KLM) tunacheza mpaka mida ya kutoka shule. Wenzetu wakija sisi tunachukua madaftari tunakopi notes kisha tunaendelea kucheza mpaka giza ndo kurudi home.

shule napo ilikuwa raha sana..ile breki ya saa nne au lunch ni mpira mwanzo mwisho...siku nyingine tunacheza mechi/ligi ingawa siku zote darasa la sita/saba ndio walishinda na wao mechi iliisha kwa ngumi.

UMITASHUMTA nao ulisaidia saidia kuendeleza vipaji ingawa nakubali sikuwa na kiwango cha kufika huko...them good old days!
 
inamaana maswala ya lunch kwenu ilikuwa ni maswala ya kubabaishana?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
yani njaa haiumi kabisa.....mwili unakua upo bize na maswala ya msingi zaid ya kupachika magoli tu.....yn mpka tumbo linashangaa
 
Mimi nilikuwa sikosi namba nilikuwa monitor majina ya wasumbufu na watoro ninayo mfukoni mkizingua tuu napeleka kwa ticha mkali
[emoji23][emoji23][emoji23] mwanangu ulikua unatumia umonta ipasavyo kwa kweli
 
wenzio tulikua tunaweka kondom....yn ukisuka mpira na kuweka kondom ndani yake....weeeeeee yn hapo hata utamu wa gozi hauoni ndani.......kitu kinadunda freshiiii
hii ilikuwepo heheheh,

ila upigani fulani wakuuchumpa mpira kwa kutumia kucha haukuwa unaruhusiwa maana unaweza pasua ndom,

ukionwa namba huna ndo umejitoa sub hivyo. [emoji16][emoji16][emoji16]
 
wenzio tulikua tunaweka kondom....yn ukisuka mpira na kuweka kondom ndani yake....weeeeeee yn hapo hata utamu wa gozi hauoni ndani.......kitu kinadunda freshiiii

Mh kondomu!??? hii mpya mkuu...sisi soksi na magorodo ndiyo viliumia. Sijui wazazi waliwezaje kutuvumilia aisee.

Hapa nimejikuta nawaza, kuna watu walikuwa wanajua kufuma mpira aisee...sijui kwanini hawakuwa wanafuma mingi watuuzie.
 
yaaah ila inaonesha hukuwa mpenz sana.....ulipata hata mda wa kukopy notes??? watu tumebandika maharage na jiko liko pembeni ya uwanja lkn mpka sufuria inatoboka hatuna habari......kuja kustuka ni pale unaskia bimkubwa anasalimiana na majirani....weeeee..!!!! ndo unaanza kuskia harufu ya maharagwe kuungua
 
kulikua na wale watu ambao kila siku mtu unatamani uwe nao timu moja
 

hahahahaha....huoni wewe uikuwa afadhali hata ulipata muda wa kurudi nyumbani aisee.

Nikiwa shule ya msingi, mama hakuamini kama tungefaulu kwenda sekondari.

Too many games.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…