Watoto wa 'Mcharo' wapo vizuri hatari, waongoza matokeo Kidato cha Nne

Watoto wa 'Mcharo' wapo vizuri hatari, waongoza matokeo Kidato cha Nne

King Kong III

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2010
Posts
56,205
Reaction score
79,515
Umofia kwenu wana JF,

Watoto wa Mcharo Angel na Jennifer waongoza matokeo ya kidato cha nne kwa kupata Div I za point 7(GPA 5.0) kila mmoja.

Hongera Sana Mcharo.
 
Umofia kwenu wana JF,
Watoto wa Mcharo Angel na Jennifer waongoza matokeo ya kidato cha nne kwa kupata Div I za point 7(GPA 5.0) kila mmoja.Hongera Sana Mcharo.

Bado kuna division 1?
 
Nimeangalia Matokeo yao ni kweli wamepata G.P.A za 5.0 kila mmoja,wote wamepata A 7 na B tatu,wametofautiana katika B,mmoja(Angel) kapata B ya B/Knowledge na Mwingine(Jenifa) Kapata B ya B/Maths,Masomo mengine yote nane wamepata Alama Sawa.Hongera sana Familia ya Mcharo.
St Francis Mcharos.jpg
 
Kutokana na matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni na baraza la mitiani, kama ukifuatilia vizuri wale watoto waliofanya vizuri zaidi kwenye mitihani yao na kuingia kwenye top ten kuna mabinti wawili wa familia moja ya mzee Mcharo yaani: Angel Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya na Jenifa Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya. Hawa watoto wameshika nafasi za juu kabisa kwenye hiyo mitihani iliyofanyika mwaka jana. Kufanya vizuri kwa hawa watoto kunanikumbusha kabisa lile tangazo la Vodacom linalosema Mcharo amekuwa mtamu, yaani mzee ambaye alikuwa ni muendesha bodaboda na ghafla maisha yake yalibadilika na kuanza kutunza familia yake vizuri sana ikiwemo watoto wake wanaosoma boarding. Yaani kwa kweli nilivyoona haya matokeo mazuri ya hawa mabinti Angel na Jenifa yamenifanya nione kama kuna uhalisia fulani. Ningependa kuchukua nafasi hii kuwapongeza watoto hawa na familia nzima ya mzee Mcharo.
 
Kutokana na matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni na baraza la mitiani, kama ukifuatilia vizuri wale watoto waliofanya vizuri zaidi kwenye mitihani yao na kuingia kwenye top ten kuna mabinti wawili wa familia moja ya mzee Mcharo yaani: Angel Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya na Jenifa Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya. Hawa watoto wameshika nafasi za juu kabisa kwenye hiyo mitihani iliyofanyika mwaka jana. Kufanya vizuri kwa hawa watoto kunanikumbusha kabisa lile tangazo la Vodacom linalosema Mcharo amekuwa mtamu, yaani mzee ambaye alikuwa ni muendesha bodaboda na ghafla maisha yake yalibadilika na kuanza kutunza familia yake vizuri sana ikiwemo watoto wake wanaosoma boarding. Yaani kwa kweli nilivyoona haya matokeo mazuri ya hawa mabinti Angel na Jenifa yamenifanya nione kama kuna uhalisia fulani. Ningependa kuchukua nafasi hii kuwapongeza watoto hawa na familia nzima ya mzee Mcharo.

Hivi lile ndo tangazo la vodacom mkuu? Ya Airtel yanakuwaje?
 
Ungetupia ufaulu wao ingenoga zaidi
 
Mchalo Kawa mtamuuu, tulikua na Mchungaji wetu anaitwa Mzee Mchalo, Lushoto miaka hioo
 
Nadhani wamevunja record kwa kutoka familia moja.

Mcharo is real delicious aisee.
 
Ungeijua hiyo shule hata usingeshangaa, hiyo shule hakuna anaefeli tangu nimeanza kuijua hiyo shule miaka ya 1990?sijui huko nyuma. na kupata nafasi ni shida kwa kwakua inachukua watoto wachache sana ila mwanao akipata nafasi pale basi mzazi amani mwanao yupo kwenye mazingira salama.
 
Div I ya point 7 ni sawa na GPA ya 5.0 ni kitu kimoja ni sawa kama tulivyozoea kuita vituo vya mafuta sheli.

Shell ya BP, Shell ya Total! Kwa kweli kazi ipo, kwamba One ya distinction! Anyway, tutakujaga kuelewa tu!!
 
Back
Top Bottom