Watoto wa mke mkubwa tukutane hapa

Amini amini nakuambia... bado hujamsamehe mama yako mdogo. Na hili utaenda nalo mpaka kaburini usipobadilisha msimamo.

Nakuonea huruma sana
 
Hayo mateso yote ni laana ya kutompokea kristo yesu

Yesu ni mwema atawatendea yaliyo mema maishan mwenu
 
So sad Sara... Aisee pole sana. Nimesoma nilipofika hapo sehemu kuwa Dada yako alikuwa km analia nikacheka kwa Julia hadi machozi
 
mi bi mdogo namwogopa kama ninavyo ogopa nyoka hahaha kwahio wala simtembelei,,,dingi nae alifariki.
kweli bila kusamehe unajikuta umejitwika zigo kubwa sana,,,hakuna namna ni kusamehe tu

asante mpendwa
Jikaze nenda ukamsalimie tu
 
Amini amini nakuambia... bado hujamsamehe mama yako mdogo. Na hili utaenda nalo mpaka kaburini usipobadilisha msimamo.

Nakuonea huruma sana
Injili yako ya MSAMAHA nimeipenda
 
wale ambao baba zetu walikuwa na mke mmoja tupite......
 
Namaanisha kila mtu anakomaa kivyake huna habari nao ko hakuna cha mzigo wa kijitwisha
Yes, ila kama umekulia katika familia za dizaini hii, mzigo ni mawazo, uchungu na chuki, havikai vikaondoka bila msaada wa maombi, watu psychology, na watu wanaofundisha mafunzo ya imani.
Maana kuishi kwenye familia za hivi haina tofauti na child abuse, tulikuwa abused psychologically, emotional, financial sasa unapoona au kushuhudia ugomvi baina ya wamama wawili watu wazima wakitukanana au mmoja kutukanwa inauma aisee. yaani mama yako anatukanwa na huwezi msaidia lolote, na hakosa lolote shida ni ku share mume tu, huo ni mzigo mzito sana vifuani mwa watoto wa pande zote.
 
Jikaze nenda ukamsalimie tu
Kwa kweli ni jambo ambalo halinisumbui hata kidogo, hata sidhani kama anahitaji salaam yangu...namaanisha kila maja anaamani alipo. Hata kama hana amani basi ni yeye, mi nimefanya suruhu na moyo wangu
 
So sad Sara... Aisee pole sana. Nimesoma nilipofika hapo sehemu kuwa Dada yako alikuwa km analia nikacheka kwa Julia hadi machozi
Ni kweli mkuu, na ukiwa na huzuni hata upake mafuta ya aina gani huwezi pendera, unakua kama unalia hahah..yaani saivi kajifunza kuachilia amenawili achaaa.
 
Kwahiyo nyie watoto shida kwenu mnaona ni mashindano au sio
 
Amini amini nakuambia... bado hujamsamehe mama yako mdogo. Na hili utaenda nalo mpaka kaburini usipobadilisha msimamo.

Nakuonea huruma sana
Amini Amini nakwambia mimi naweza samehe hata mtu ambae hajaniomba msamaha, kikubwa nimejisamehe mwenyewe, nimejisamehe kwa kujitwika mizigo isiyonihusu-ndoa ya wazazi wangu
nimejisamehe kwa kutokujitunza na kujaza havira mwilini na kifuani
nimejisamehe kwa kusahau kujipenda na kuwapenda na kuwapa muda wengine
nina amani sana mkuu, alafu unadhan ukienda kumsalimia ndio atakupenda basi haha, lazimaa utaondoka amekukwaza asa kwa nini nijipeleke sehem najua kabisa si salaama?
Watoto wa bi mdogo na bi mkubwa wote tunaongea na kusaidiana pia, japo rohoni kila mtu anakinyongo na malezi au familia yetu, wazazi walifanya hivyo.
Afu Mungu mwema maana ametutawanya kama nini yaani wote tupo mbalimbali sana.
 
Pole...me wa mke mmoja na Mme mmoja ndani ya ndoa takatifu..asante Mungu kwa hilo.
Kweli mshukuru sana Mungu, nina rafiki yangu nae wakwenye mitala yaani yeye hata kuolewa imeshindikana, maana ni ameathirika sana, amekuwa too harsh.
 
Labda kwa nyie wanawake kwa wanaume tunapotezea na tusingeweza shuhudia hayo yakifanyika mbele ya macho yetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…