Watoto wa Wasira waliojiunga CHADEMA watoa ufafanuzi juu ya uhusiano wao na Waziri Wasira

Ingekuwa ni wewe ungeenda kulumbana na wanao vyombo vya habari? Angekaa kimpya habari hii ingeshakuwa historia sasa imezidi kuwajenga chadema na hao watoto pia
Habari imeandikwa kwenye vyombo vya habari ulitaka yeye akakanushie wapi kama si kwenye vyombo hivyo hivyo vya habari. Kama kuna chombo cha habari kiliandika "watoto ni wa Steven Wassira" kilikuwa sahihi?
 
Kumbe sio Steven Wassira.


Hata mmoja wapi wa waasisi wa CDM siyo huyu Steven Wasira, bali ni huyo kaka yake George Wasira mwenye hawa watoto.
 
Kwahio Mzee wasira anapigwa dongo jingine tena? hata siamini
 
Huyu Easter si ndo alishawahi kuimba Bongo flava ?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hoja hapa si kama watoto wa Kaka yake si wake, hoja hapa ni kwamba Baadhi ya vyombo vya habari vilitangaza na kuandika kwamba ni watoto wa Steven Wassira. Steven ana haki ya kuweka mambo sawa na wala hajawakana kama si watoto wa ukoo wao!!

HOJA si watoto wa nani, HOJA ni mabinti wawili LILIAN WASSIRA na ESTHER WASSIRA wamejiunga na CHADEMA baada ya kuona ndio chama kinachotoa matumaini kwa watanzania.
 
Kama ulitazama ITV siku ile ilielezwa wazi kabisa ni watoto wa ndugu yake waziri wasira,sasa sijui ilikuwaje yamekuwa mazito,labda siku hizi habari ni chache.

Hapana tuwe wazi na wa kweli... Nadhani tatizo sio habari tu, tatizo lipo kwa waandishi, wana CCM na wana CDM wenyewe.

Habari ya mabinti wawili kupata card mpya ya CDM alafu tena wamekabidhiwa hizo card na Slaa, unadhani itaacha kutengeneza headlines na hali ni wazi hivyo vyama pinzani kubwa?
 
Hongera sana liliani na ester kwa kujiunga na Chadema
,huo ndio ujasiri tunaohitaji ndani ya taifa hili.Mungu awabariki mfike mbali kisisasa.
 
kama umri wao unaruhusu kugombea ningeshauri mmoja wao agombee jimbo la steven wasira'yule mzee anatakiwa kupotea katika ulimwengu wa siasa

:biggrin1: na ndio itakavokua hivyo..sasa tuone ka mzee atakua tayari kuwapeleka mabwepande ndugu zake
 
Nafikiri wauza magazeti waliweka heading kwa kusudi wanalolijua. Sidhani kama watoto wanataka kusafiria nyota ya Wassira Steven maana huyu profession aliyokuwa nayo ni matusi, kejeli na ukigeugeu. Siasa za matope anazijua sana toka anapambana na Mzee Warioba hapo mwaka 1995. Moja ya kete alizotumia ilikuwa ni lugha ya matusi, dharau, kejeli na kila aina ya kiburi. Mahakama ilimwondolea ubunge kwa style yake na akabaki kuuza samaki pale ferry mpaka alipokumbuka kurudi kwenye chama kilichokuwa kimemtuma kufanya umamluki. Sasa kwenda public na kutoa maelezo ya kwamba hawa sio watoto wake wa kuzaa naona kajidhalilisha mno. Wawe wa kuzaa, wawe wa mjoma, wa shangazi, wa kaka, wa mdogo wake, watoto ni watoto na ni zawadi ya familia na ukoo. Alichopaswa kusema ilikuwa ni kumshukuru Mungu kwanba watoto tunawapa uwanja mpana kujiamulia na sio kukurupuka na kuongea wa jaziba na kuwawekea watu wengine maneno. Hakuna ambapo Dr.Slaa alisema hao ni watoto wa Steven. Kwa kifupi hakuna nyota ya kusafiri kwa Steven Wassira
 

Hongereni kwa maelezo ya kutosha kwani hayo maelezo yenu hayakuhitaji mtu yeyote aje ayajibu wala kukanusha
kipekee nimeshangaa mzee Wasira akijikanyaga eti kuwa akina Esther na mwenzake si watoto wangu bali ni watoto wa kaka yangu.Safi kwa uamuzi wenu mliouamua always AIM HIGHER@ M4C
 
Mzee Wasira huwa ana hulka ya ubabe nakujiona anajua sana kuliko mtu mwengine,huyu Mzee amelewa madaraka,
 
Hivi Wassira hajawahi kupata mtikisiko wa ubongo?
 

Now you're talking......
Jana niliyaongea haya almanusura nitolewe macho
Hawa watoto ni wanasheria na nihaki yao kujiunga CDM lakini pia walipaswa kutumia akili kuepusha conflicts za ukoo kwa kutokubali kutumiwa kama mtaji wa kisiasa kwa kile kinaonekana kumdhihaki wasira
What is so special kwa wao kwenda makao makuu kupokewa na Slaa Huku wamezungukwa na media?
 
Watu wanatoana povu kwa hoja nyepesi!
 
Kwamba wanatumika kisiasa ni maoni yako tu lakini haikatazwi kupokea kadi na kuzungumza na media. Kwanza wao ni watoto wa mwasisi wa chadema na pia ni wanaharakati wa kike, vijana wasomi, hiyo ilitosha kuivuta media. Na inaonekana media ilikuwa karibu kwa kuwa walienda kumuuliza Dr Slaa kuhusu kushindwa umeya mwanza
 

Haya mambo its all about timing... Weapon so lethal in politics hasa kama you have the rite moves... Dr. Slaa na wana CDM wanajua hilo na hata mabinti Wassira walijua hilo. Jina la Wassira is what carried weight to the news, hapo result ni kuwa tayari hawa dada wamejijengea jina Kisiasa kishabiki.... INASIKITISHA.

But believe me you hapo mmoja wao akiamua kugombea nafasi ya uongozi hata ya ubunge tayari wana full support ya Chama cha CDM na wanachama wao... Bila kujali kama kunaweza kuwa na possibility ya upandikizi, bila kujali kama wana uwezo huo wa kuongoza na bila kujali wana kuwa kuna wengine wanaweza kuliko hao. Yoote tu kwa ajili ya kukidhi kiu ya ushindi katika gutter politics ya ready made followers...
 
Safi sana. Hawa watoto wanaonekana wanabusara na wameelimika.
 
Anakasirika nini si kuna wakati alijiunga na NCCR anachoshangaa nini watoto wa ndugu yake kujiunga na CDM?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…