Watoto wana uwezo mkubwa sana, ila sijui tatizo ni nini?

Nokla

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2012
Posts
3,190
Reaction score
1,774
Mtu anayepata divion zero aka Dunia duara anawezaje kuandika haya?
"nawashangaa wabunge, wamekaa kama wapo kijiweni, wabunge wamekosa ustaarabu, badala ya kujadili kero za wananchi waliowachagua, wanapokea timu zilizoshinda makombe.........timu ikishinda Kombe la Kagame inapokelewa bungeni. Bunge limekuwa kama kijiwe, bungeni siyo ukumbi wa starehe kama mnataka kupokea timu hizo nendenikatika ofisi zao au viwanjani"
INAKUAJE MWANAFUNZI HUYU ASHINDWE KUSOMA AU KUFAULU HATA KISWAHILI?
 
Ndio maana tunasema mtaala wakufundishia ndio umepitwa na wakati, hii ni kizazi ya digitali huwezi fundisha vitu vya analogia wakaelewa. Kama tumehama analogia tuhame mazima sio biashara ya ving'ambuzi tu.
 
Ndio maana tunasema mtaala wakufundishia ndio umepitwa na wakati, hii ni kizazi ya digitali huwezi fundisha vitu vya analogia wakaelewa. Kama tumehama analogia tuhame mazima sio biashara ya ving'ambuzi tu.

Tatizo si mtaala, hata wangefundishwa kianalog na wakawa na wakati wakufuatilia mafunzo, ingekuwa safi tuu
Mimi naona turudi zama za Nyerere' kuwa vitu vya mawasiliano majumbani ni anasa. Watu waache kununua ili watoto wapate time ya kupiga book. Sio wanasoma wakiwa mashuleni tuu.
 
Yani Mkuu unasema mawasiliano na taarifa ni anasa? Sasa elimu ina mchango gani kwa taifa hili?
Dunia nzima iende mbele sisi tu ndio tuchague kurudi karne ya 19 sio? :nono: Mkuu unajua ile Maktaba yote ya Tanganyika inaingia kwenye Ipad moja tu.
 
Yani Mkuu unasema mawasiliano na taarifa ni anasa? Sasa elimu ina mchango gani kwa taifa hili?
Dunia nzima iende mbele sisi tu ndio tuchague kurudi karne ya 19 sio? :nono: Mkuu unajua ile Maktaba yote ya Tanganyika inaingia kwenye Ipad moja tu.

Mimi naona tatizo namba moja linaanza na wanafunzi wenyewe they are not motivated kabisa, shule kama azania, Benjamini Mkapa, zilikuwa hazina walimu wakutosha lakini wanafunzi walikuwa wanafaulu kama kawaida, ila siku hizi, dah!!!!!
 
Nimekuwa nafadhaika mno kuona jamii inakubali kuburuzwa na watu wenye dhamana ya elimu nchini kwa kutoa sababu za kijinga kuhusu matokeo mabaya ya mitihani kwa shule za msingi na sekondari.
Sikubaliani nao kwa sababu ikiwa mtoto utamfundisha 1 + 1 = 3 unategemea jibu liwe tofauti kwenye mtihani?
Kiini cha yote haya ni wenye dhamana kupuuzia walimu na ualimu wake (masilahi na uweledi), kwa mfano shule zina walimu wa kutosha? Baba wa taifa aliisha sema kuwa na majengo mazuri na wingi wa shule bila kuwa na walimu (wenye weledi) na vifaa tosha kwenye shule huo ni upuuzi.
Sote tumeshuhudia mwaka jana mgomo wa walimu ulizotatuliwa na walimu walivokubali kufundisha, sasa tunategemea matokeo yawe vipi?
Sasa jana nimemsikia RC wa Mzizima (Dar Es Salaam) akisema kuwa heshima aliyopewa rais Kibaki wa Kenya atakapo fika mjini hapo kuaga ni kuiita 'barabara ya old Bagamoyo road jina lake'!!!!!!!!!!!!!
 
Mimi naona tatizo namba moja linaanza na wanafunzi wenyewe they are not motivated kabisa, shule kama azania, Benjamini Mkapa, zilikuwa hazina walimu wakutosha lakini wanafunzi walikuwa wanafaulu kama kawaida, ila siku hizi, dah!!!!!

Nakubaliana na wewe kabisaa
 
imedhihrika
wakati tunawataarifu watawala kwamba wameanzisha vituo vya kulelea vijana na si shule walituzonga. migomo ya walimu waliwaambia wametumwa na wapinzani kuyumbisha nchi
Mbatia wamemwambia mjengoni hakufanya utafiti wa kina.
subiri ngonjera mpya.
msukumo wa mafanikio tunao sisi 2015.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…