Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Kuna sehemu Yohana aliwahubiria watoza ushuru. Walimuuliza. "Sisi ni watoza ushuru. Unatushauri tufanye nini?" Yohana aliwajibu, "Msitoze zaidi ya kiasi kilichowekwa."
Zamani kulikuwa kuna kitu kinaitwa tax farms(mashamba ya kodi). Tajiri anaifuata serikali ya Roma na kuomba tenda ya kukusanya kodi kwenye eneo fulani.
Serikali inamwambia lipa kiasi kadhaa cash halafu utakusanya kodi labda kwa mwaka, miaka miwili nk. Lakini serikali inakuwa na muongozo wa jinsi kodi inavyopaswa kuwa.
Huyu tajiri akishalipa anaingia hilo eneo na jeshi lake la watoza ushuru kufanya kazi. Walikuwa makatili sana.
Inabidi watoze kadri wawezavyo ili kupata faida. Mara nyingi walitoza hata kiasi kilichozidi kilichopo kwenye muongozo. Wengi ambao walishindwa kulipa kodi waliuzwa utumwani.
Ndiyo kisa cha Yohana kuwaambia wasitoze zaidi ya kiasi kilichowekwa.
Zamani kulikuwa kuna kitu kinaitwa tax farms(mashamba ya kodi). Tajiri anaifuata serikali ya Roma na kuomba tenda ya kukusanya kodi kwenye eneo fulani.
Serikali inamwambia lipa kiasi kadhaa cash halafu utakusanya kodi labda kwa mwaka, miaka miwili nk. Lakini serikali inakuwa na muongozo wa jinsi kodi inavyopaswa kuwa.
Huyu tajiri akishalipa anaingia hilo eneo na jeshi lake la watoza ushuru kufanya kazi. Walikuwa makatili sana.
Inabidi watoze kadri wawezavyo ili kupata faida. Mara nyingi walitoza hata kiasi kilichozidi kilichopo kwenye muongozo. Wengi ambao walishindwa kulipa kodi waliuzwa utumwani.
Ndiyo kisa cha Yohana kuwaambia wasitoze zaidi ya kiasi kilichowekwa.