Watu 10 maarufu walioacha chuo na kuleta mabadiliko makubwa duniani

Watu 10 maarufu walioacha chuo na kuleta mabadiliko makubwa duniani

Nukta5

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2014
Posts
1,182
Reaction score
1,288
1. Steve Jobs
Inawezekana komputa za Mac na bidhaa nyinginezo kama iPhone zisingekuwepo kama Steve Jobs angebakia chuo.

2. Bill Gates
Moja wa watu walioacha chuo Harvard na wamefanikiwa na ni tajirimkubwa duniani. Mwanzilishi wa Microsoft. Kauli aliyoitoa kwenye mahafali pale Harvard mwaka 2007 alisema ” Mimi ni mshawishi mbaya ndio maana mmeniita niongee wakati wa mahafali. Ningeongea wakati wa kuanza masomo yenu ni wachache sana mngekuwepo hapa.”

3.Frank Lloyd Wright
Mbunifu mkubwa wa vyuo vingi marekani lakini hajawahi kuhudhuRia hata kimoja. Ingawa Frank Lloyd Wright
alichaguliwa kwenda chuo cha
Wisconsin-Madison mwaka 1886,
lakini aliacha baada ya mwaka
mmoja.

4. Buckminster Fuller
Bwana Huyu alifukuzwa Harvard
mara mbili lakini ni mtu ambaye
amefanikiwa sana na kuleta mawazo
mapya katika ulimwengu huu. “He
was expelled from Harvard twice:
first for spending all his money
partying with a vaudeville troupe,
and then, after having been
readmitted, for his “irresponsibility
and lack of interest.”

5. James Cameron
Muongozaji maarufu wa filamu za
Hollywood aliyetengeneza filamu
nyingi za kubuni na za kisayansi na
zenye gharama kubwa zikiwemo
Titanic na Avatar.

6. Mark Zuckerberg
Mwanzilishi wa mtandao wa
Facebook na aliyekuwa mwanafunzi
wa Harvard. Baada ya Facebook
kuanza kupata umaarufu aliamua
kuacha chuo.

7. Tom Hanks
Mwigizaji maarufu aliyeamua kuacha
chuo Sacramento State na kujiunga
na Great Lakes Theater Festival kule
Cleveland, Ohio. Huko akajifunza vitu
vingi kumfikisha kuwa moja ya
waigizaji na watengeneza filamu
maarufu huko Hollywood.

8. Harrison Ford
Jamaa hut=yu aliacha chuo pale
Ripon College siku chache kabla ya
kumaliza. Ni moja ya watu
waliofanya vitu vikubwa kwenye
filamu za Star wars miaka 1977.

9. Lady Gaga
Kabla ya kuwa Gaga, alikuwa
anaitwa Germanotta. alizaliwa
na Stefani Joanne Angelina
Germanotta, msanii ambaye kwa sasa
anaitwa Lady Gaga alianza
kusoma New York University’s Tisch,
Shule ya Usanii na baada ya hapo
aliacha chuo baada ya mwaka mmoja
na kuanza uimbaji wake pale New
York club na kuweza kusaini mkataba
wake na Interscope Records akiwa na
miaka hiyo hiyo 20.

10. Tiger Woods
Mtu maarufu katika mchezo wa golf,
baada ya miaka miwili aliacha
kusomea uchumi pale Chuo cha
Stanfold, kwa sasa analipwa zaidi ya
dola milioni 100 kwa mwaka.

source: bongo5
 
Uzuri hao ulio wataja mazingira yaliwasaidia sana kufanya maendeleo yao! Mfumo wao wa elimu pia ni mzuri kiasi kwamba hata wale drop out hawapati hasara ukilinganisha na huku!

Halafu wengi walizaliwa na uwezo mzuri kichwani na pia wana vipaji vya aina yake!

Mtu akisoma vibaya hii thread anaweza kufikiri kuwa hata akiacha shule anaweza kufanikiwa tuu kumbe hata swala la mazingira ya nchi vinasaidia sana!

Ukiangalia hao jamaa nchi yao marekani ina thamini sana sanaa na teknologia na wamewekeza sana kwenye hayo mambo kiasi kwamba hata school droup out wanaweza fanikiwa kirahisi.....

Ndio maana kwetu huku mtu anapo acha shule anaonekana kuwa hatoweza kufanikiwa na watu huamini shule pekee ndio njia ya mafanikio.....

Hao shule wanafundishwa kujiwezesha, ubunifu na kukuza vipaji vyao tofauti na huku kwetu.....ndio maana umeona mtandao wa Facebook ulibuniwa na jamaa akiwa chuoni na huo ndio utofauti wetu na wenzetu!

Tukiuliza ni wanafunzi wangapi ambao wanasoma computer science kwenye vyuo vya hapa nchini wameweza kutengeneza au kubunikitu au apps ambayo imeweza kuwabadilisha wao na kuwa chanzo cha mapato?

Kuna wanafunzi wengi wanamaliza vyuo lakini hawawezi ku practise walicho jifunza sasa je wangeacha?

Kwakweli mazingira yana changia sana kwenye hili.
 
Uzuri hao ulio wataja mazingira yaliwasaidia sana kufanya maendeleo yao! Mfumo wao wa elimu pia ni mzuri kiasi kwamba hata wale drop out hawapati hasara ukilinganisha na huku!

Halafu wengi walizaliwa na uwezo mzuri kichwani na pia wana vipaji vya aina yake!

Mtu akisoma vibaya hii thread anaweza kufikiri kuwa hata akiacha shule anaweza kufanikiwa tuu kumbe hata swala la mazingira ya nchi vinasaidia sana!

Ukiangalia hao jamaa nchi yao marekani ina thamini sana sanaa na teknologia na wamewekeza sana kwenye hayo mambo kiasi kwamba hata school droup out wanaweza fanikiwa kirahisi.....

Hivi havard ni chuo cha watu wenye vipaji maalum coz watu wengi maarufu duniani hupitia husoma pale
 
mbona wa hapa bongo hujawaweka?!"............

Grand PA
 
Hao wenzio waliacha shule.sio kwa kufeli, bali kwa kukosa ada ama kuwa na biashara kabambe (kama zuckeberg). Weeh uache shule shauri ya ujinga afu uone mziki wake.
 
Kwani kwa tanzania waliofanikiwa wote ni wasomi? Wengine waliacha shule kwa kukosa fees,family problems,kufeli ,Kuendeleza bizness! Etc Kuna jamaa aliacha shule form two sasa hivi yupo safi sana sio tajiri kama mengi lakini ana utajiri wa kibongo nyumba 6,maduka ya jumla 3,maduka ya hardware ma2 na maduka ya rejareja 6,gari 4,mbili za kutembelea,2 za kubebea bidhaa zake za dukani,bodaboda 20.
 
Mmh Kwa Bongo Sidhani Kwakweli....Labda Uache Afu Ulete Changes Kwako Wewe Kama Wewe Na Sio Duniani....Mazingira Yetu Yako Complicated Sana Jamani!!!! 🏃
 
Hapo kwenye list umemsahau Diamond platnuzz baabie na Sean Comb a.k.a puff Dady
 
Ushasema chuo that means waliona umuhimu wa kusoma kindergarten mpaka chuo wakaacha.. na kwa upande wa majuu mtu mpaka kufika chuo kikuu ameshakuwa na skills za kutosha za kuweza kujiajiri mwenyewe tofauti na wanavyuo wa huku kwetu mpk mtu ana masters bado hajitambui yeye ni nani...
IGA UFE!!!
 
mnyika aliacha chuo kuwakomboa wana ubungo, mbatia alifukuzwa kwa kutetea maslahi ya wanyonge, ongeza na wewe,
 
mbona kabarou alikuwa anafundisha pale, sumai alivyostaafu uwaziri mkuu kaenda kupiga book pale

Kabarou hajawahi findisha pale....
http://www.parliament.go.tz/index.php/members/mpcvs/1246/2000-2005
 
Back
Top Bottom