Watu 160,000 hatarini kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula Yemen

Watu 160,000 hatarini kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula Yemen

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1647370126929.png

Mashirika ya misaada kadhaa ya Umoja wa Mataifa yamesema watu wapatao 160,000 wamo hatarini kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula nchini Yemen.

Ripoti ya mashirika hayo juu ya hali hiyo ya kutisha imetolewa kabla ya mkutano wa wafadhili utakaofanyika hapo kesho. Umoja wa Mataifa umetayarisha mkutano huo kwa ajili ya kuchangisha fedha.

Ripoti ya asasi za Umoja wa Mataifa inatanabahisha juu ya hali mbaya inayoikabili Yemen ambayo imekuwamo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu mwaka 2014 baada ya waasi wa kihouthi wanaoungwa mkono na Iran kuutwaa mji mkuu wa Yemen, Sanaa na sehemu kubwa ya kaskazini mwa nchi hiyo.

Mfungamano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia uliingia vitani kupambana na waasi hao mnamo mwaka 2015 ili kuisaidia serikali inayotambuliwa kimataifa.
 
Back
Top Bottom