Watu 4 wanaotuhumiwa ‘kutumwa na afande’ kumlawiti na kumbaka binti mkazi wa Yombo Dovya Mkoani Dar, Wafikishwa Mahakamani

Hapo wafanye kufuatilia mawasiliano ya simu watapata vingi.

Inaonekana hili suala hawajataka kulifuatilia ipasavyo, wakiamua kuminywa hayo mapumbu watasema nani kawatuma.

Tena huyo mwenye jezi alionekana kabisa sijui wanakataa nini...
 

Wewe namna gani aisee!

Mwenye mzigo na wajibu kuthibitisha kesi ni anayeshitaki yaani, kwenye kesi hii, Jamuhuri ndiyo yenye wajibu wa kuthibitisha kwanza kwamba kulikuwa na jinai na hiyo jinai ilitendwa na watuhumiwa na watuhumiwa ndiyo hao hapo.

Lazima Jamuhuri iwasilishe ushahidi wa utambuzi na Form ya Gwaride la Utambuzi* mujibu wa PGO.

Lazima form ya Gwaride la Utambuzi iwe imejazwa kikamilifu Kwa mujibu wa PGO.

Once Jamuhuri ikifeli kwenye identification na au Identification Parade, basi kesi inaishia hapo Kwa sababu watuhumiwa waliotenda kosa wameshindikana kutambulika.

NB: Mahakama haifanyi kazi Kwa taarifa za mtandaoni bali inafanya kazi ushahidi uliowasilishwa mbele ya Mahakama.
 

Kwa hiyo umesusa?

Mahakamani hakuna hisia wala siasa bali uhalisia.

Lazima vielelezo vitolewe kwamba hiyo video ni halisi na siyo imetengenezwa
 
Kwa hiyo umesusa?

Mahakamani hakuna hisia wala siasa bali uhalisia.

Lazima vielelezo vitolewe kwamba hiyo video ni halisi na siyo imetengenezwa
Ndio maana nikasema wawaache huru kama hata video hazina ushahidi yasiwe mambo mengi wawaache huru mambo mengine yaendelee maana hiyo Sheria unayoleta hapo ni ya kupindisha ukweli kama hawajabaka waachwe huru warudi kulitumikia taifa maana hata video ni uongo hivi wewe Kwa akili Yako Ile video imetengenezwa
 
Ndio maana nikasema wawaache huru kama hata video hazina ushahidi yasiwe mambo mengi wawaache huru

Umma umefanya sehemu yake, Serikali nayo inafanya wajibu wake, na Sasa ni zamu ya Mahakama kufanya wajibu wake wa kutoa tafsiri halisi ya tukio na hukumu.
 
Umma umefanya sehemu yake, Serikali nayo inafanya wajibu wake, na Sasa ni zamu ya Mahakama kufanya wajibu wake wa kutoa tafsiri halisi ya tukio na hukumu.
Wajibu Gani hukumu ni kufunga au kuacha huru kama hiyo mahakama inaona kwenye video walikua wanacheza na sio kubaka basi wawaache huru maneno mengi ya nini wawaache huru mbona kawaida tu tushazoea watu kunyimwa haki hapa tanzania Kwa kisingizio Cha sheria hatutoshangaa
 
Hizo namba za Mt..na C... Zinafikirisha sana.
Na wanaopiga kelele kwamba wanataka kulindana, kumbe wapo sahihi.
 
Kuthibitisha kuwa aliwatuma. Hapo ndiyo muziki ulipo. Kutoa uthibitisho mahakamani kuhusu jambo fulani kama hili, siyo jambo la kitoto.
Inategemeana na muunganiko wa vielelezo vitakavyokusanywa.

Ila mantiki ya kubaka huku unafotoa ilikuwa ni nini?
 
Umma umefanya sehemu yake, Serikali nayo inafanya wajibu wake, na Sasa ni zamu ya Mahakama kufanya wajibu wake wa kutoa tafsiri halisi ya tukio na hukumu.
Kuna muda nikiliangalia hili suala jinsi wabongo walivyolichukulia kwa hisia kali, natamani mahakama itoe hukumu ambayo iko kinyume kabisa na matarajio yao... halafu nione reaction yao itakuwaje, nataka nione je, kwa hizi hasira zao wataingia mabarabarani kwa ajili ya kudai justice kwa huyo binti kweli kama wanavyowafanya wanawake wa India kwa yule daktari aliyebakwa? Au hasira zao zitaishia kwenye kucomment tu huku mitandaoni halafu baada ya hapo watasahau.

NB: hata mimi nimechukizwa sana na hili tukio hasa nikiangalia hawa wahusika kada waliopo inanichukiza zaidi.
 
Duuh... wewe jamaa kwa hizi spana unaonekana unaweza hata kuwa wakili mtetezi wa wale magaidi yaliyofungwa kule Guantanamo Bay na mkashinda kesi.
 
***** acha kabisaaa tuliwahi kuwa na kesi yaani ushahidi CCTV camera inaonesha kabisaaa ila wana tulitoboa🤣🤣🤣
UShahidi wa video ni mgumu sana aisee,yaani kumfunga mtu ni kipengele ndio maana hata yule afande rama wa zenji alitoboa kwa sababu vipengele ni vingi sana.

Na ninadhani kwenye jicho la sheria hawa jamaa huwenda wakatoboa
 
Hizo kesi jamaa wanaweza kutoboa, Amini usiamini. Hapo kosa kabisa ni makosa ya mtandao ila hayo mengine wanaweza yapangua vizuri kabisa.
Unamaanisha wasiojulikana waliojulikana?
 
Upo sahihi msomi mwenzangu.

Na ugumu upo kwenye kupeleka original device iliyotumika kurekodi tukio! Yaani ile simu ya kwanza kurekodi:

N.b case imekaa vibaya sana upande wa hawa madogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…