Watu 4 wanaotuhumiwa ‘kutumwa na afande’ kumlawiti na kumbaka binti mkazi wa Yombo Dovya Mkoani Dar, Wafikishwa Mahakamani

Kama Kuna mtu aliwatuma lazima awe katika wasiwasi na majonzi makubwa kwa ku wahalibia maisha madogo.

Ila kauli isiyokuwa na umakini ya Bosi imeamsha hasira za wananchi.
 
Punguza kuangalia movies
 
Huyo mwenye jezi kama ya Simba kafupi sana, kaliwezaje kuwa Askari!
 

Kwani yule RC aliyefikishwa mahakamani kwa kesi ya ubakaji kulikuwa na video? Binti si ndiye aliyetendewa? Binti si ndiye aliyeenda kushitaki? Video(Picha jongefu) au CCTV footage ni just a supporting evidence tu na wala mahakama hawatorelay na hizo clips ,watarelay na maelezo ya Binti maana yeye ndiye aliyelawitiwa na madaktari watathibitisha kama kweli binti aliingiliwa.
 
Nakuuliza hizo namba zinazoanzia na MT na C ni za nini?
 

Hapa kuna tafsiri ya maandishi yako kwa Kiswahili:

Ushahidi wa kielektroniki unakubalika kwa mujibu wa
Sheria ya Miamala ya Kielektroniki ya mwaka 2015.
Kifungu cha 18 cha Sheria ya Miamala ya Kielektroniki kinaeleza kuwa ili ushahidi wa kielektroniki ukubalike mahakamani kama kielelezo, kinachohitajika kuthibitishwa ni uaminifu wa ushahidi wa kielektroniki kuhusu jinsi rekodi ilivyorekodiwa na jinsi ilivyohifadhiwa hadi ilipoletwa mahakamani kama ushahidi.

Shahidi anayetarajia kutoa ushahidi wa kielektroniki lazima kwanza aonyeshe ushahidi unaoondoa uwezekano wa kudanganywa kwa ushahidi wa kielektroniki kabla ya kuwasilisha.
Kabla ya kuwasilisha ushahidi wa kielektroniki, shahidi anapaswa kuridhisha Mahakama kwa ushahidi kwamba ushahidi wa kielektroniki unaotarajiwa kuwasilishwa ni halisi. Hii inafanywa kwa kuthibitisha hali ya kiufundi ya kifaa wakati wa kurekodi, jinsi rekodi ilivyofanywa, na nani aliyeifanya na kuhifadhi hadi ushahidi ulipowasilishwa mahakamani.

Ikiwa rekodi ya kielektroniki ilibadilishwa kuwa vyombo vya sekondari kama flash, njia ya kubadilisha kuwa vyombo vya sekondari pia inapaswa kuthibitishwa.
 
Waliona raha kuchezea tope la mtoto wa watu, acha waaibike pimbi hawa.
 
Ili ithibitike kwamba kulikuwa na ubakaji na ulawiti, ni lazima ithibitishwe kwamba watuhumiwa walimuingilia bila ridhaa yake Binti.

Ili kuthibitisha kwamba watuhumiwa ndiyo walimuingilia ni lazima ripoti ya daktari iseme kwamba kwenye sehemu za Siri za Binti kulikuwa na majimaji ya watuhumiwa.

Sasa changamoto hapa ni ukosefu wa hayo majimaji. Sidhani kama alipimwa kabla hajaoga. Hapa kimsingi hakuna uthibitisho wa kuingiliwa.

Tuje kwenye ushahidi wa video.

Kanuni za ushahidi wa video zinamtaka Shahid athibitishe kwanza kwamba vifaa vilivyorekodi vilikuwa vinafanya kazi Kwa ufasaha kabla ya kurekodi, na uthibitisho unatakiwa uwe wa mtaalamu aliyebobea kisomi katika fani ya electronic. Lengo la kanuni hii ni kuepuka uwezekano kwamba video imeyengenezwa na siyo halisi.

Pia kama video zimehamishwa kutoka kwenye simu, CCTV na kuwekwa kwenye flash, ni lazima ithibitishwe kwamba kuhamisha huko hakukuathiri ushahidi. Hili linaenda sambamba na kuthibitisha kwamba hiyo flash ilikuwa salama yaani haina virus au mechanical damage iliyopunguza ubora wa ushahidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…