Watu sita mbaroni kwa kula njama za kumuua Dk. Chegeni

Watu sita mbaroni kwa kula njama za kumuua Dk. Chegeni

Njama za mauaji CCM

• DK. CHEGENI ANUSURIKA KUUAWA KWA RISASI

na Sitta Tumma, Mwanza




KATIKA hali ya kushtusha, kundi la mtandao wa watu sita akiwemo mjumbe wa Kamati Kuu ya Siasa (CCM), mkoani Mwanza, wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kula njama na kutaka kumuua kwa kumpiga risasi aliyekuwa mbunge wa zamani wa Jimbo la Busega wilayani Magu mkoani hapa, Dk. Raphael Masunga Chegeni (CCM).

Watuhumiwa wa mtandao huo wa mauaji, walikamatwa Aprili 13 mwaka huu mkoani Mwanza, wakiwa katika harakati maalumu za kumuwinda kumuua Dk. Chegeni, ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita 2010 alishindwa kwenye kura za maoni ndani ya chama hicho tawala, na sababu kuu inayodaiwa kutaka kumuua mbunge huyo wa zamani wa Busega ni uhasama wa masuala ya kisiasa.

Taarifa zilizoifikia Tanzania Daima jana jijini Mwanza zinaeleza kwamba mtandao huo wa kutaka kumuua kwa kumpiga risasi Dk. Chegeni uliandaliwa tangu wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana na anayedaiwa kuhusika na mpango huo ni mwanasiasa mmoja ambaye pia ni kiongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi (jina tunalo).

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo pia zimethibitishwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, zimewataja waliokamatwa na polisi kwa tuhuma hizo kuwa ni Dismas Zacharia Kamani (mratibu wa mauaji), Erasto Casmil (alitafuta wauaji), Queen Joseph Bogohe (alitumika utoaji wa fedha kwa wauaji), Ellen Bogohe, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya siasa CCM mkoani Mwanza, na diwani wa zamani wa Viti Maalumu Kata ya Kisesa, wilayani Magu mkoani hapa.

Wengine wanaodaiwa kuhusika kwenye mtandao huo wa kutaka kumuua Dk. Chegeni ambao wamekamatwa na jeshi la polisi mkoani Mwanza, walitajwa kuwa ni Hamis Masoud mkazi wa Furahisha jijini hapa na Richard Kamugisha mkazi wa Mwanza.

Mbali na watuhumiwa hao wanaodaiwa kukamatwa, mtumishi mmoja wa serikali katika kitengo nyeti (jina na kitengo chake tumevihifadhi), kwa sasa, naye ametajwa kuwemo kwenye mtandao na hujuma hizo za kutaka kumuua Dk. Chegeni, lakini mtumishi huyo bado hajakamatwa na polisi.

“Ni kweli tukio la kutaka kuuawa Dk. Chegeni lipo, na baadhi ya wanamtandao huo wa mauaji wamekamatwa na wako ndani kwa sasa!

“Kati ya hao waliokamatwa, yupo mmoja wao presha ilimpanda baada ya kubanwa maswali mazito na polisi na hasa alipoona mawasiliano yake yote ya kupanga mikakati ya mauaji yapo mikononi mwa polisi,” kilisema chanzo kimoja ambacho hakikutaka kutajwa jina lake kwa sababu si msemaji wa polisi.

Habari zinaeleza kwamba siku ya Aprili 13 mwaka huu, baadhi ya wanamtandao hao wa walizulu jijini Mwanza kwa lengo la kukamilisha taratibu zote za mauaji, ikiwa ni pamoja na kukodi mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Kamanda Chakaza kutoka wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa ajili ya kumchakaza Dk. Chegeni kwa risasi.

Inadaiwa kwamba mhusika wa mtandao huo aliahidi kuupatia mtandao wake huo sh milioni 9 na kati ya fedha hizo sh milioni 4 zilikuwa kwenye utaratibu wa kupelekwa jijini Mwanza kwa ajili ya kutimiza azma hiyo ya mauaji, huku baadhi ya fedha zikidaiwa kutumwa kwa njia ya simu ya kiganjani.

Kulingana na tukio hilo, taarifa zinadai kwamba siku hiyo watuhumiwa hao wa kupanga mauaji walifika jijini Mwanza wakiwa wamepewa sh milioni 1.2 na kwamba baadaye polisi walipata taarifa juu ya mkakati huo kisha kuanza kuweka mtego ambapo ulifanikiwa kuwakamata watu hao.

“Baada ya kufika Mwanza, polisi walipata taarifa na kuweka mtego ambao ulifanikiwa kunasa mawasiliano yote ya mikakati ya kumuua Dk. Chegeni kwa kutumia bunduki na rissi za moto...baada ya hapo polisi walifanikiwa kuwazingira na kuwakamata wakiwa kwenye hoteli maeneo ya mtaa wa Rufiji,” kilisema chanzo kingine huku kikisema: “Siasa ni mchezo mchafu na mbaya sana.”

Uchunguzi wa Tanzania Daima unaonesha kwamba watuhumiwa hao wote kwa ujumla huenda leo Jumanne watapandishwa mahakamani kwenda kujibu tuhuma zinazowakabili na kwamba mtuhumiwa namba moja (jina linahifadhiwa), wa kupanga mtandao huo wa kutaka kumuua Dk. Chegeni ambaye hivi sasa anajihusisha na masuala ya biashara, bado anatafutwa na polisi na muda wowote akikamatwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yake.

Alipoulizwa jana ofisini kwake iwapo ni kweli tukio hilo lipo na watuhumiwa wamekamatwa, kamanda wa polisi mkoani Mwanza na kamishna mwandamizi wa polisi nchini, Simon Nyakoro Sirro, alisema kwa kifupi: “Tumewakamata, lakini kesho (leo) nitawapeni taarifa zote, kuna vitu fulani bado nakamilisha.”

Hata hivyo Tanzania Daima ilipomtafuta Dk. Chegeni ili kuelezea tukio hilo la kutaka kuuawa kwake, hakuweza kupatikana mara moja, licha ya kupata taarifa kwamba alikuwa katika hali ya hofu zaidi.

Matukio ya namna hii yakiwemo ya badhi ya wanasiasa mkoani Mwanza kumwagiwa tindikali mwilini si geni, kwani matukio kadhaa ya mauaji ya wanasiasa, kumwagiwa tindikali mwilini yalishawahi kutokea mkoani hapa, ikiwa sababu kuu ni uhasama wa kisiasa.

Kati ya mwaka 1995 aliyekuwa mbunge wa Mwanza mjini kipindi hicho, marehemu Saidi Shomali, alimwagiwa tindikali usoni na watu waliosadikiwa kuwa ni mahasimu wake wakubwa wa masuala ya kisiasa, mwaka 1994 aliyekuwa diwani wa Kata ya Kitangiri jijini Mwanza, Sylvester Lubala naye alipata maswahibu kama hayo.

Lakini matukio kama hayo, yaliendelea kuukumba mkoa wa Mwanza ambapo mwaka jana 2010 aliyekuwa meya wa jiji la Mwanza na diwani wa Isamilo, Leonald Bandiho Bihondo (CCM), alikamatwa na kufikishwa mahakamani hadi sasa kwa tuhuma za kula njama na kumuua kwa kumchoma visu sehemu mbalimbali za mwili Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephano kwa kile kinachodaiwa kuwa na uhasama dhidi yao wa masuala ya kisiasa.

source ;tanzania daima
 
Jaribu kueleza kilicho andikwa kwenye gazeti kwa ufupi. Wengine hatupo Tanzania au sehemu ambayo unaweza kupata gazeti hilo. Habari uliyotoa hajitoshelezi. Kama unalo hilo gazeti jaribu kuweka ufupisho wa hiyo habari.

ok mkuu kwa wewe ulie nje maana wengine awanunui mkuu na gazeti lazima ziuzwe..pole ntaongea na freemedia warekebishe mtandao wao

--CHEGENI ANUSURIKA KUUWA KWA RISASI
--POLISI YAWAKAMATA WANAMTANDAO SITA

Katika hali ya kshtusha kundi la watu sita akiwemo mumbe wa kamati kuu ya ccm mwanza wamaekamatwa na polisi kwa tuhuma za kutaka kumuua kwa kumpiga risasi aliekuwa mbunge wa zaman jimbo la busega DK Raphael chegeni

watuhumiwa hao wa mtandao walikamaatwa tar 13 apr 2011 wakiwa ktkt harakati maalum za kumuwinda dk chegen na sababu kuu inayodaiwa kutakaa kumuu dk chegen ni uhasama wa sias

taarifa zilizoifikia tanzania daima mtandao huo ulitaka kumuu dk chegen uliandaliwa kufanyika wakati wa uchaguzi mwaka jana na anaedaiwa kuhusika ni mwanasias na mfanyabiashara mkubwa wa CCM jina tunalo

kwa mujibu wa taarifa za polisi waliokamatwa na polisi ni pamoja na ellen bagohe ambae ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm mkoa wa mwanza..mbali na watuhumwia hao kukamatwa mtuhumiwa mmoja alieko usalaama wa taifa nae anahusika kikamilifu na shuguli hii na uchunguzi unaendelea muda si mrefu tutamkamata walisema....

habari zinasema siku ya tar 15 wanamtandao walizulu hotel moja na kumkodisha jamaa mmoja aiitwae kamanda chakaza kutoka kahama kwa sh million 4...watuhumiwa hao waliakuja mwanza wakiwa wamepewa sh mil 2 kama advance

baada ya kufika mwanza polisi walipata taarifa na kuweka mtego ikiwemo mazungumzo yao yotte na wakati wakishindina kiasi wanachoitaji..uchunguzi wa daima tanzania unaonyesha hunda wakasimamishwa kizimban leo kwa makosa yao

mkuu hpe umeeleewaa wauwaji wetu
 
Waacheni wavuane magamba kisawasawa ..huko kwetu kuna nyoka mmoja anaitwa Olunyambabi,huyu nyoka inaaminika akikua huvua gamba lake na kuwa mkali zaidi na hata jina hubadilika na kuitwa Enkolantima,haya ndo magamba ya ccm wanavua moja na sumu inaongezeka maradufu mara Iringa wanajiua,mara wanatafutana kuuana...kaaaaaaazi kweeeeli kweeli,ccm ni Enkolantima

sio olunyambabi anaitwa Olunyalubabi ila umeleweka mkuu na ni ukweli usio na doa
 
WAKATI CCM ikijivua gamba, Jeshi la Polisi mkoani Mwnaza limenasa kundi la mtandao wa watu sita akiwemo mjumbe wa Kamati Kuu ya Siasa (CCM), mkoani Mwanza kwa tuhuma za kula njama na kutaka kumuua kwa kumpiga risasi aliyekuwa mbunge wa zamani wa Jimbo la Busega wilayani Magu mkoani hapa, Dk. Raphael Chegeni (CCM).

Watuhumiwa wa mtandao huo wa mauaji, walikamatwa Aprili 13 mwaka huu mkoani Mwanza, wakiwa katika harakati maalumu za kumuwinda kumuua Dk. Chegeni, ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita 2010 alishindwa kwenye kura za maoni ndani ya chama hicho tawala, na sababu kuu inayodaiwa kutaka kumuua mbunge huyo wa zamani wa Busega ni uhasama wa masuala ya kisiasa.

Taarifa zilizoifikia Tanzania Daima jana jijini Mwanza zinaeleza kwamba mtandao huo wa kutaka kumuua kwa kumpiga risasi Dk. Chegeni uliandaliwa tangu wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana na anayedaiwa kuhusika na mpango huo ni mwanasiasa mmoja ambaye pia ni kiongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi (jina tunalo).

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo pia zimethibitishwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, zimewataja waliokamatwa na polisi kwa tuhuma hizo kuwa ni Dismas Zacharia Kamani (mratibu wa mauaji), Erasto Casmil (alitafuta wauaji), Queen Joseph Bogohe (alitumika utoaji wa fedha kwa wauaji), Ellen Bogohe, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya siasa CCM mkoani Mwanza, na diwani wa zamani wa Viti Maalumu Kata ya Kisesa, wilayani Magu mkoani hapa.

Wengine wanaodaiwa kuhusika kwenye mtandao huo wa kutaka kumuua Dk. Chegeni ambao wamekamatwa na jeshi la polisi mkoani Mwanza, walitajwa kuwa ni Hamis Masoud mkazi wa Furahisha jijini hapa na Richard Kamugisha mkazi wa Mwanza.

Mbali na watuhumiwa hao wanaodaiwa kukamatwa, mtumishi mmoja wa serikali katika kitengo nyeti (jina na kitengo chake tumevihifadhi), kwa sasa, naye ametajwa kuwemo kwenye mtandao na hujuma hizo za kutaka kumuua Dk. Chegeni, lakini mtumishi huyo bado hajakamatwa na polisi.

Habari toka ndani ya CCM na jeshi la polisi ambazo zimethibitishwa na kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Simon Sirro zinaeleza kwamba watuhumiwa hao walikamatwa kuanzia Aprili 13 mwaka huu wakiwa katika harakati za mwisho kukamilisha mpango wao wa mauaji.

Imeelezwa kuwa wanamtandao hao walikutana jijini Mwanza kwa lengo la kukamilisha taratibu zote za mauaji, ikiwa ni pamoja na muuaji aliyedaiwa kutumia silaha aina ya SMG iliyokuwa ikikodiwa kutoka wilayani Kahama mkoani Shinyanga lakini hawakujua kuwa walikuwa wakifuatiliwa na jjeshi la Polisi na hivyo kutiwa mbaroni.

Mpango huo wa mauaji ulikuwa umepanga kufanyika kwa kiasi cha sh. 10.2 milioni ambapo katika kiasi hicho walilipwa awali kiasi cha sh. 1.2 ambapo milioni 1 ilikuwa ni kwa ajili ya kukamilisha zoezi ikiwa ni pamoja na kukodi silaya huku ikielezwa kuwa sh. 2 zilikuwa ni kwa ajili ya usafiri wa kufuatilia nyendo za mbunge huyo.

Hata hivyo kutokana na polisi kutambua mapema njama hizo waliweka mtego na kufanikiwa kuwanasa watu hao na hivyo kuzuia mauaji hayo mapema na sasa jeshi lake linawashikilia watu hao sita kwa kuhusika na njama hizo.

Uchunguzi zaidi wa jeshi la polisi umedokeza kuwa Njama hizo zilikuwa zikipangwa na Mbunge mmoja wa kanda ya ziwa ambaye hajakamatwa.

Kamanda Simon Sirro ameahidi kutoa taarifa ya matukio hayo leo kwa vyombo vya habari.

Matukio ya namna hii yakiwemo ya badhi ya wanasiasa mkoani Mwanza kumwagiwa tindikali mwilini si geni, kwani matukio kadhaa ya mauaji ya wanasiasa, kumwagiwa tindikali mwilini yalishawahi kutokea mkoani hapa, ikiwa sababu kuu ni uhasama wa kisiasa.

Kati ya mwaka 1995 aliyekuwa mbunge wa Mwanza mjini kipindi hicho, marehemu Saidi Shomali, alimwagiwa tindikali usoni na watu waliosadikiwa kuwa ni mahasimu wake wakubwa wa masuala ya kisiasa, mwaka 1994 aliyekuwa diwani wa Kata ya Kitangiri jijini Mwanza, Sylvester Lubala naye alipata maswahibu kama hayo.

Lakini matukio kama hayo, yaliendelea kuukumba mkoa wa Mwanza ambapo mwaka jana 2010 aliyekuwa meya wa jiji la Mwanza na diwani wa Isamilo, Leonald Bandiho Bihondo (CCM), alikamatwa na kufikishwa mahakamani hadi sasa kwa tuhuma za kula njama na kumuua kwa kumchoma visu sehemu mbalimbali za mwili Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephano kwa kile kinachodaiwa kuwa na uhasama dhidi yao wa masuala ya kisiasa.
 
Mbali na watuhumiwa hao wanaodaiwa kukamatwa, mtumishi mmoja wa serikali katika kitengo nyeti (jina na kitengo chake tumevihifadhi), kwa sasa, naye ametajwa kuwemo kwenye mtandao na hujuma hizo za kutaka kumuua Dk. Chegeni, lakini mtumishi huyo bado hajakamatwa na polisi......


Mhh, hiki kitengo lazima kitakuwa kile maarufu kwa ajili ya kuongoza Mikakati ya Uchakachuzi na
Usalama wa Wachakachuzi Tanzania

All, in all.......watamalizana.....na huu ni mwanzo tu, so much more to come
 
Tunatoana roho, yarabi...kwa mali alizoacha baba...
Mali ya baba inanitoa roho, bora nikae pembeni, niyanusuru maisha yangu...

Marehemu TX Moshi William
 
Hiyo nayo ni njia ya kujivua gamba! Mpaka 2015, watakolimbana hadi wajimalize wenyewe!
 

Mhh, hiki kitengo lazima kitakuwa kile maarufu kwa ajili ya kuongoza Mikakati ya Uchakachuzi na
Usalama wa Wachakachuzi Tanzania

All, in all.......watamalizana.....na huu ni mwanzo tu, so much more to come
Siyo UWT ni Mtumishi wa mahakama.
 
Waandishi wetu bwana. Mmeshindwa kumfikia Dr Chegeni aseme angalau neno moja tu na roho zetu zisuuzike?
 
Code:
Police hold 6 over Chegeni death plot [URL="http://www.thecitizen.co.tz/component/mailto/?tmpl=component&link=aHR0cDovL3d3dy50aGVjaXRpemVuLmNvLnR6L25ld3MvNC1uYXRpb25hbC1uZXdzLzEwMTAzLXBvbGljZS1ob2xkLTYtb3Zlci1jaGVnZW5pLWRlYXRoLXBsb3QuaHRtbA%3D%3D"] Send to a friend[/URL] Tuesday, 19 April 2011 12:12 digg

By Frederick Katulanda, The Citizen Reporter
Mwanza. Mwanza police are holding six people including the region's Chama Cha Mapinduzi (CCM) political committee member over an alleged murder plot on former Busega MP Raphael Chegeni.
Information reaching The Citizen and confirmed by the region's police commander, Mr Simon Sirro, said the six were arrested between April 13 and 17 following a tip off.
The information links the incumbent Busega MP, Dr Titus Kamani, through SMS and conversations among the six who have been arrested, including Dr Kamani's relative, who is allegedly the coordinator of the plot.
However, in a quick rejoinder, Dr Kamani denied having any information regarding the matter, including the arrest of his relative over the plot.
He added that his relationship with the arrested CCM political committee member was purely political despite the fact that his younger sister was also among those arrested. His sister is alleged to have engineered the delivery of Sh5 million as an initial payment.
It is reported that the contracted murderers, who are among the six arrested, were paid Sh1 million by another suspect in order to hire a gun, study Dr Chegeni's movements as well as facilitate the killing.
The killers were promised Sh10 million with an initial Sh5 million being paid as down payment before the killing and the rest after the ‘work.'
The MP's male relative was arrested after police set a trap involving the contracted hitmen and an undercover police, who posed as a killer from Shinyanga, at a guest house in Mwanza.
He went to the guest house to finalise the deal with the killers, including meeting in person with the killer hired from Shinyanga, who turned out to be an undercover policeman. Another plainclothes policeman who stationed himself outside the guest house stormed the room and arrested the MP's relative.
According to information from the police, after the mobile phones of the suspects were inspected, text massages linking Dr Kamani with the murder plot over political reasons were revealed.

Dr Chegeni could not be reached yesterday for comment as his telephone was switched off the whole day.

Ukiangalia hii habari ya the Citizen inaonyesha kuwa kumbe mauaji hayo yalikuwa yakiandaliwa na Mbunge wa Busega....looo hatari
Send to a friend
 
Back
Top Bottom