Watu wa Karatu nini kimewapata hadi kuanza kujenga mabondeni?

Watu wa Karatu nini kimewapata hadi kuanza kujenga mabondeni?

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimesikitishwa sana na ninachoona mtandaoni kuhusu watu wa Karatu kukumbwa na mafuriko na nyumba zao kuzingirwa na maji. Mungu awatangulie kwenye hiki kipindi kigumu. Lakini nimeshangaa imekuwaje watu wa Karatu kuanza kujenga kwenye bwawa ambalo kila mwaka hujaa maji? Inakuwaje serikali iruhusu ujenzi bwawani? Au kuna watu wa Msimbazi Dar walihamia Karatu na kupeleka akili zao huko?

Ikumbukwe Karatu ipo kwenye muinuko mkubwa hivyo kusema kukumbwa na mafuriko ni jambo gumu mno. Ninadhani sis raia tutumie sana akili kabla ya kufanya maamuzi ya kujenga. Serikali nayo isitoe vibali vya ujenzi kiholela.
FB_IMG_1717146670100.jpg

FB_IMG_1717146667198.jpg

FB_IMG_1717146662538.jpg

FB_IMG_1717146659570.jpg
 
Baadhi ya watu hujenga katika mabonde wakiamini ni gharama kubwa kujenga milimani
 
Wanatakiwa waulizwe wanajenga nyumba za nn labda kufugia samaki
 
Balise diridiri milah baragee nasi loalee ...ni ukorofi tu na tamaa
 
Back
Top Bottom