Watu wa mataifa mengine hasa Wachina kufanya biashara za umachinga ni kuua soko la wazawa

Watu wa mataifa mengine hasa Wachina kufanya biashara za umachinga ni kuua soko la wazawa

Hii sijui niite ujinga ama ubinasfi au kukosa kabisa maarifa juu ya upendo wa nchi yako au kwa jamii yako kabisa?

Kuna hili sakata kwa sasa kwa wageni haswa wachina wamekuwa wengi sana hapa nchini na. Mbaya zaidi wanafanya kazi za wazawa tena zile za chini kabisa, nazungumzia umachinga

Unakuta mgeni(mchina) anamtaji mkubwa alafu anafanya biashara kama machinga na si muwekezaji, rudi kwenye masoko yetu makubwa na mikoa yetu hakuna sehemu mchina kwa sasa hayupo na mbaya zaidi anatumia supply chain ile ile kumfikia hadi mteja wa mwisho, kiufupi ni ana uwa soko kabisa

Tunaweza tusilione hilo kwa sasa lakini embu fikiria kwa kijana mwenye mtaji mdogo anawezaje. Kuwa na ushindani kwa mgeni ? Huyo?

Kilichonikera zaidi wachina nchini ndio wanaongoza kukwepa kodi tena wanashirikiana na wazawa kabisa ambao ni wafanyakazi wao kukwepa kodi. Sasa hivi wanawatumia wazawa kuwaweka front haswa kwenye nyaraka za umiliki, alafu wana waforce kuhakikisha hawalipi mapato ya seriakali. Mfano mdogo tuh mchina naingiza mtaji wa Tsh 500M alafu anasema yeye ni retail store kwahiyo makadirio ya kodi yako chini na bado ujanja ujanja ni mwingi sana wakisaidiwa na wazawa ambao wanasahau hiyo kodi ndio inayojenga nchi yetu.

Kama umeshindwa kufanya kodi iende serikalini kwann usiipige wewe mzawa? Ukajipatia na mtaji? Achane kuwaogopa wageni kwanza mtu anakufokeaje nchini kwako na unajua hajanyooka?

Wachina wanatabia ya kukutafutia mbadala hata uwe bora kiasi gani so kama upo kwa wageni itetee nchi yako ama tetea mkate wako na familia yako sio kumpa chance ya kutunyonya.

Hawa jamaa wametuona mazuzu kiasi kwamba wanazidi kuongezeka, wanapita hadi madukani kwa sasa wanauza hadi pc 1 sasa kinachofata si watapita majumbani kutafuta wateja???
Ndio maana ya SOKO HURIA na UTANDAWAZI, maingiliano ya kibiashara, sijui kama watanzania hawapo China wakifanya biashara au wanakatazwa kufanya hivyo. Ukweli ni kwamba hiyo pia ni fursa, mtafute mchina kama huyo ushirikiane naye pengine ukatoka mapema, wapo wengi wameshirikiana na wachina na mambo yao yapo vyeeee.
 
Back
Top Bottom