Watu wa Stationery tunaomba serikali ichunguze kupanda kwa bei za karatasi na vifaa vingine

Watu wa Stationery tunaomba serikali ichunguze kupanda kwa bei za karatasi na vifaa vingine

Mchokozi wa mambo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2014
Posts
201
Reaction score
159
Ndugu zangu watu wa Stationery hali yao ni mbaya sana. Kwani bidhaa muhimu katika Stationery hasa karatasi nyeupe zimepanda sana na haijawahi kutokea.

Kabla ya kauli ya Rais kuwa bidhaa nyingi zitazidi kupanda bei ya Katoni ilikuwa inauzwa Tsh 43000 ghafla baada ya ile kauli kutoka katoni ya ream sasa ni Tsh75000.

Fikiria kabla ya kupanda bei Ream pc1 kwa bei ya rejareja ilikuwa ni Tsh 9000 au 8000 lkn inauzwa kwa Tsh 17000 na 18000.

Kwa utafiti mdogo nilioufanya nimegundua kuwa Ream nyingi zinazotumika nchini kwetu zinaagizwa kutoka Afrika ya Kusini. India, China na Indonesia. Sasa hizi bei zitapanda mpaka wapi.

Waagizaji na wasambazaji wakubwa wanakula njama na ushirikiano acha kabisa. bei tunaziona wanazipanga wao kwa makubaliano kuwa na bei moja ili kila mtu apate faida kubwa hasa kwa kuzingatia kauli ya Mheshimiwa Rais ilikuwa amewapa nguvu.

Hii ya kusema kila kitu kinapanda bei sababu ya vita vya Urusi na Ukraine ni kichaka cha kujifichia ili kutesa raia. Wakuu wa Wilaya na mikoa tokeni pamoja wa wahusika mjionee hali halisi. Huu ni uhuni mkubwa kwa nchi yetu
.
 
Mi ni mmoja wa wahusika

Kwa upande wa soko la jumla kwa maana ya kariakoo saiv rimu ni kati ya 65 mpaka 70 na kama upo mkoani ongeza 3000 mpaka 4000 ya usafir kwa kila katoni


Sasa kama nikanunua kwa bei hiyo kutoka 43 mpaka 45 ongezeko la zaid ya 70%

Nikuuzie tsh ngapi?


Nilichofanya mimi kwakuwa nilikuwa na stock yangu nimeamua kutoziuza rim ili nitumie mwenyewe kwa uzalishaji NDAni ya ofisi maana nikisem kwa bei ya sasa ninunue italazimu zip zipande bei kitu ambacho sitaki kabisa kitokee
 
Acha tu mzee,vitu vingi sana vimepanda aisee,hizo ream ilikuwa 7500 moja,saizi eti ream ni 70,000.

Na wanaagiza bei ile ile ya mwanzo,ukiuliza wanasema wanauza bei ambayo iko sokoni.
 
Tanzania tuna kiwanda cha karatasi cha Mgololo kilichopo Mufindi Iringa! Kwa bahati mbaya kinazalisha makaratasi ya kaki tu!

Ili kupata karatasi nyeupe, inatulazimu kama nchi kuagiza kutoka nje.
Kuna jamaa yuko I-print ananileteaga rim
 
Tupunguze matumizi ya karatasi na haswa matumizi ya karatasi nyeupe.
 
Back
Top Bottom