Watu walionufaishwa na Usomaji wa Vitabu

Watu walionufaishwa na Usomaji wa Vitabu

Tambua tu kwamba wewe kama husomi vitabu umekwisha, uko gizani na umepitwa sana na unaendelea kupitwa.

Mtu asiye msomaji wa vitabu ni sawa na mtu mfu anayetembea. Asiye msomaji wa vitabu hawezi kujua faida na manufaa ya usomaji wa vitabu. Usomaji wa vitabu ni chakula cha akili, huimarisha uwezo wa kufikiri na uwezo wa kujenga hoja. Usomaji wa vitabu huchangamsha akili, huongeza maarifa, huimarisha msamiati na hukuza uwezo wa lugha. Huboresha kumbukumbu, hujenga uwezo wa uchambuzi wa masuala mbalimbali, hujenga uwezo wa kuandika na umakini na pia njia bora ya kupunguza sononi.

Msomaji wa vitabu ana maudhui ya kutosha (Content) kuliko asiyesoma vitabu. Hata inapotokea ubishani au uchangiaji mada utaiona waziwazi tofauti ya wasomaji na wasio wasomaji wa vitabu. Wasio wasomaji badala ya kujadili hoja watapayuka, wataonesha ghadhabu, watashambulia mtu binafsi badala ya kutetea hoja yake. Mara nyingi wasomaji wa vitabu watachangia hoja kwa utulivu, kwa kujenga hoja na mifano na rejea mbalimbali kutoka kwenye vitabu alivyosoma, bila ghadhabu wala kupayuka.


Is reading the key to success?
It has been proven that children who read better, preform better in school and have a more active imagination, leading to a larger world and more possibilities for success.
🙏🙏🙏
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji120]

Usomaji utakusaidia kuepukana na umbra.

Wasomaji wa vitabu wanapokutana, ni kawaida kwao kujadili "ideas", lakini wale wengine sasa! Wakikosa cha kuongea huishia kuwajadili watu.
Yaani mkuu ukisoma vitabu ni rahisi kuwadanganya watanzania namuheshimu ruge lakini alikuwa anawakamata kupitia vitabu wananifurahisha wakisema ogopa mungu na teknolojia halafu wanasema ni msemo wa ruge watanzania wenzangu tusome vitabu tuache ujinga na kudanganywa.
 
Tambua tu kwamba wewe kama husomi vitabu umekwisha, uko gizani na umepitwa sana na unaendelea kupitwa.

Mtu asiye msomaji wa vitabu ni sawa na mtu mfu anayetembea. Asiye msomaji wa vitabu hawezi kujua faida na manufaa ya usomaji wa vitabu. Usomaji wa vitabu ni chakula cha akili, huimarisha uwezo wa kufikiri na uwezo wa kujenga hoja. Usomaji wa vitabu huchangamsha akili, huongeza maarifa, huimarisha msamiati na hukuza uwezo wa lugha. Huboresha kumbukumbu, hujenga uwezo wa uchambuzi wa masuala mbalimbali, hujenga uwezo wa kuandika na umakini na pia njia bora ya kupunguza sononi.

Msomaji wa vitabu ana maudhui ya kutosha (Content) kuliko asiyesoma vitabu. Hata inapotokea ubishani au uchangiaji mada utaiona waziwazi tofauti ya wasomaji na wasio wasomaji wa vitabu. Wasio wasomaji badala ya kujadili hoja watapayuka, wataonesha ghadhabu, watashambulia mtu binafsi badala ya kutetea hoja yake. Mara nyingi wasomaji wa vitabu watachangia hoja kwa utulivu, kwa kujenga hoja na mifano na rejea mbalimbali kutoka kwenye vitabu alivyosoma, bila ghadhabu wala kupayuka.


Is reading the key to success?
It has been proven that children who read better, preform better in school and have a more active imagination, leading to a larger world and more possibilities for success.
Kati ya jambo ambalo ninamshukuru sana Mungu, ni kuwa na tabia ya usomaji wa vitabu.

Sijui ningekuwaje bila vitabu! Vitabu vimenisaidia sana, vimenitoa pabaya mno.

Mtu anayekejeli usomaji wa vitabu ni wa kuonewa huruma sana. Najua, anayekejeli hajui kuwa hajui, hasa ikizingatiwa kuwa katika ulimwengu huu, karibia kila mtu utakayekutana naye, hata yule aliyeonekana wazi kuwa ni "mjinga", bado atajiona ana akili kukuzidi.

Ndiyo maana asiyejua manufaa ya vitabu haoni mapungufu yake. Atakapofanikiwa kujenga urafiki na vitabu ndiyo atajigundua kuwa alikuwa anaishi ndani ya boksi lenye giza katika ulimwengu mpana wenye nuru.
 
Yaani mkuu ukisoma vitabu ni rahisi kuwadanganya watanzania namuheshimu ruge lakini alikuwa anawakamata kupitia vitabu wananifurahisha wakisema ogopa mungu na teknolojia halafu wanasema ni msemo wa ruge watanzania wenzangu tusome vitabu tuache ujinga na kudanganywa.
You are right mkuu!

Hata Nyerere alikuwa msomaji sana wa Vitabu.

Umenikumbusha na Mwalimu mmoja, miaka ile nikiwa kidato cha Sita, alishawahi kuniambia kuwa "HATA MUNGU ANASEMA JISAIDIE KWANZA NDIPO NAMI NIKUSAIDIE", nilipomwuliza ilikoandikwa, aliishia kuniambia tu kuwa ni kwenye Biblia!

Maskini Mwalimu wa watu! Kumbe hiyo kauli ilikuwa ni ya Benjamin Franklin, mwanafalsafa wa Marekani aliyependa vitabu kuzidi hata chakula. Si bure mpaka sasa Wamarekani wangali wakimkumbuka! Alilisadia sana taifa lake. Na siri ya mafanikio yake ni ulafi wa vitabu. Alivifakamia mno.

Kama huyo Mwalimu angelikuwa msomaji wa vitabu, angefahamu kuwa huo usemi ulikuwa ni wa Benjamin Franklin na siyo Biblia.

Kusoma vitabu vizuri kunalipa sana.

Shukran mkuu🙏! Umenikumbusha mbali!!!
 
Yaani mkuu ukisoma vitabu ni rahisi kuwadanganya watanzania namuheshimu ruge lakini alikuwa anawakamata kupitia vitabu wananifurahisha wakisema ogopa mungu na teknolojia halafu wanasema ni msemo wa ruge watanzania wenzangu tusome vitabu tuache ujinga na kudanganywa.
🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom