Watu wamevurugwa aisee, ona vituko hiv barabarani

Joined
May 21, 2016
Posts
74
Reaction score
46
Jamaa mmoja kagoma kupisha ambulance, dereva anapiga kelele atoke barabarani jamaa anajibu ebu zima dude lako Usinisumbue😛😛😛😀

Juzi kati napo kuna jamaa nae alikua anatembea njiani mwenye gar kampigia mi honi jamaa aka kaa kabisa chini na njia ni ndogo ili bidi mwenye gari ashuke aje amuombe jamaa ampishe😀😛😛😛😛
weka na wewe kituko ambacho umewahi kukishuhudia au kukisikia
 
Kuna jamaa alikuwa na corola anatembea katikati ya barabara, gari ya jeshi ikawa inawasha taa za hazard gari ya jeshi inakuja inafumuka balaa, bado jamaa wa corola kabana pale katikati ya road, aisee alicho fanyiwa na yule mwanajeshi hatakaa asahau alimpiga pasi moja matata sana
 
Hahaaa kama namuona vile alivopigwa pasi akaambaa ambaa utazani shuti la Ronaldo lililoenda nje ya gori
 
Dogo wa miaka 12 kaingia baa akagida bia za Kilimanjaro kama chupa 6 na kisha baada ya apo akataka kuondoka na mhudumu akataka alipwe chake na badala yake dogo akamwonyesha mhudumu kikaratasi cha tangazo la tahadhari kilichoandikwa "TAHADHARI HAIUZWI KWA ALIYE CHINI YA UMRI WA MIAKA 18".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…