nzalendo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 12,106
- 12,916
Wasalaam si kama nina pinga elimu la hasha!
Lakini kwa upande wangu sioni sababu ya kwenda Chuo Kikuu ''haraka'' mara tu umalizapo kidato cha sita.
Watu wengi huenda kwa kuiga bila kuwa na mpango mahsusi au kujiuliza baada ya chuo/au nina kwenda ''chuo'' then what next?(KUJITAMBUA)
Ieleweke wazi dunia hii tunayoishi ni tofauti na ile ya zama za mwanzo za Uhuru.
Mfumo wetu wa Elimu hasa ya Chuo na Sekondari si rafiki tena kukuwezesha wewe uweze kujitegemea.
Hivyo usitafute/hangaikie kitu ambacho ni kama mchezo wa kubahatisha.
Mfano unasoma
1. Sheria halafu eti unarudi mtaani unaanza ujasiriamali wa kutengeza sabuni na blah blah.
2. Unasoma Sijui nini B nini komu..halafu unakuja mtaani eti wewe unaanza ukulima ...hivi maana ya elimu ni nini hasa?
Mbona hao wasioenda CHUO wanafanya mambo ya maana kuliko mtu unaejiita eti msomi halafu mambo unafanya kinyume kabisa na usomi?
(ZAMANI NYUMBA YENYE MTU WA FORM FOUR,UKIPITA HATA KWA NJE,UTAJUA HII NYUMBA ANAKAA MSOMI)
Mfano.
1.Mwanamuziki Diamond yeye alisema hana mpango wa kwenda shule kusoma watu walimshangaa sana ...lakini mimi nilimuunga mkono...manake alisema kama akienda shule atasoma lugha na muziki lakini si kwenda kusoma Jiografia kitu ambacho anaona hakitamsaidia. ''bora aachie wengine wahangaike navyo.''
2. Hivi hamuoni wahindi?.....mbona hawahangaiki na mambo yenu ya chuochuo na wana fanikiwa sana? wanaangalia upepo Je?ana nia ya ''Transport'' yeye ataenda kujifunza usafirishaji na mara nyingi si shule.
( WENGI HUJIFUNZIA MITAANI TU)
''Umefika wakati mfumo wa Elimu ubadilike''
Lakini kwa upande wangu sioni sababu ya kwenda Chuo Kikuu ''haraka'' mara tu umalizapo kidato cha sita.
Watu wengi huenda kwa kuiga bila kuwa na mpango mahsusi au kujiuliza baada ya chuo/au nina kwenda ''chuo'' then what next?(KUJITAMBUA)
Ieleweke wazi dunia hii tunayoishi ni tofauti na ile ya zama za mwanzo za Uhuru.
Mfumo wetu wa Elimu hasa ya Chuo na Sekondari si rafiki tena kukuwezesha wewe uweze kujitegemea.
Hivyo usitafute/hangaikie kitu ambacho ni kama mchezo wa kubahatisha.
Mfano unasoma
1. Sheria halafu eti unarudi mtaani unaanza ujasiriamali wa kutengeza sabuni na blah blah.
2. Unasoma Sijui nini B nini komu..halafu unakuja mtaani eti wewe unaanza ukulima ...hivi maana ya elimu ni nini hasa?
Mbona hao wasioenda CHUO wanafanya mambo ya maana kuliko mtu unaejiita eti msomi halafu mambo unafanya kinyume kabisa na usomi?
(ZAMANI NYUMBA YENYE MTU WA FORM FOUR,UKIPITA HATA KWA NJE,UTAJUA HII NYUMBA ANAKAA MSOMI)
Mfano.
1.Mwanamuziki Diamond yeye alisema hana mpango wa kwenda shule kusoma watu walimshangaa sana ...lakini mimi nilimuunga mkono...manake alisema kama akienda shule atasoma lugha na muziki lakini si kwenda kusoma Jiografia kitu ambacho anaona hakitamsaidia. ''bora aachie wengine wahangaike navyo.''
2. Hivi hamuoni wahindi?.....mbona hawahangaiki na mambo yenu ya chuochuo na wana fanikiwa sana? wanaangalia upepo Je?ana nia ya ''Transport'' yeye ataenda kujifunza usafirishaji na mara nyingi si shule.
( WENGI HUJIFUNZIA MITAANI TU)
''Umefika wakati mfumo wa Elimu ubadilike''