Watu wanaosema Tume Huru ya Uchaguzi ianze kabla ya Katiba Mpya hawajui kwamba wanabariki Katiba Mpya kutopatikana hadi baada ya 2025!

Watu wanaosema Tume Huru ya Uchaguzi ianze kabla ya Katiba Mpya hawajui kwamba wanabariki Katiba Mpya kutopatikana hadi baada ya 2025!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Jiulize, kwani Tanzania ilikuwa imefikia wapi na Mchakato wa Katiba Mpya, na ni nini kilichokuwa kimebaki ili kuikamilisha?

Na pia jiulize, ni mambo gani yanatakiwa ili kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi?

Sasa unapokuwa na majibu yanayojitosheleza ya maswali haya, ndio utoe kauli kuhusu haya mambo mawili. Lakini pia, nani amesema haiwezekani suala la Tume Huu ya Uchaguzi kufanyika sambaba na harakati za kuwa na Katiba Mpya? Kumbuka kwamba, Tume Huru ya Uchaguzi ni jambo ambalo tayari lipo kwenye Katiba Mpya iliyopendekezwa, na kukiri kwamba inahitajika haraka ni kukiri kwamba Katiba mpya inahitajika haraka..

Suala la kuwa na Tume Huru ya Uchaguz ni dogo sana, na halipaswi kuonwa kwamba liwe utangulizi wa Katiba Mpya. Na watu wakumbuke kwamba Tume Huru ya Uchaguzi ni lazima ipewe nguvu na Katiba, ambapo Katiba iliyopo haiwezi kuipa nguvu Tume Huru ya Uchaguzi. Ukilazimisha kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa Katiba iliyopo sasa basi utakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi ambayo si tu haiko huru bali pia haina meno, kibogoyo.

Lakini jambo ambalo kila Mtanzania anapaswa kujua ni kwamba, ikiwa watu watakubali Tume Huru ya Uchaguzi liwe jambo la kutekelezwa kabla ya Katiba Mpya, basi wanabariki mbinu za kufanya Katiba Mpya isiwepo hadi baada ya 2025.

Labda kama watu wana utambuzi, basi wambane Samia na serikali ili watoke kauli ya lni basi suaa la Katiba Mpya litamalizwa. Tunatakiwa kusubiri hasi lini, mwezi gani, mwaka gani? La sivyo ni kudanganyana tu.
 
Wanashindwa Nini kumalizia mchakato wa katiba mpya ambayo ndani yake inapatikana tume huru ya uchaguzi, badala yake wanatuletea maigizo? Kwa katiba hii mtaleta tume huru policcm TISS watakuwa wapi?, Je wakiiiba kura Kama ilivyozoeleka?.
Mtahoji huo wizi wapi wakati katiba hii iliyopo inazuia kuhoji matokeo ya urais mahakamani hata Kama ukikamata contena la kura feki
WANACHEZA NA AKILI ZA WATANZANIA.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CHADEMA upeo wenu ni mdogo sana kwenye mambo ya msingi! Kwanza mjiulize Katiba inayopendekezwa mnaikubali?! Pili nyie mnazungumzia Rasimu ya Warioba hatua ambayo ilishavukwa!
Sasa kwenye bunge la sasa CHADEMA mna nguvu gani ya ku-influence jambo lolote la maana against CCM!?
Watu wenye akili wanaona ni heri tupate tume huru ya Uchaguzi then ikiwezekana mpate Wabunge angalau kwenye Bunge then mapambano ya kupigania Katiba Bora yaendelee kupitia platforms za maana ikiwemo Bunge la JMT.
Tatizo CHADEMA kumejaa utoto utoto na harakati za kijinga jinga sana!
Suala la Katiba bora ni long race !
 
CHADEMA upeo wenu ni mdogo sana kwenye mambo ya msingi! Kwanza mjiulize Katiba inayopendekezwa mnaikubali?! Pili nyie mnazungumzia Rasimu ya Warioba hatua ambayo ilishavukwa!
Sasa kwenye bunge la sasa CHADEMA mna nguvu gani ya ku-influence jambo lolote la maana against CCM!?
Watu wenye akili wanaona ni heri tupate tume huru ya Uchaguzi then ikiwezekana mpate Wabunge angalau kwenye Bunge then mapambano ya kupigania Katiba Bora yaendelee kupitia platforms za maana ikiwemo Bunge la JMT.
Tatizo CHADEMA kumejaa utoto utoto na harakati za kijinga jinga sana!
Suala la Katiba bora ni long race !
Mleta uzi amekuonesha kadi ya uanachama wa CHADEMA?
 
Tume huru ya uchaguzi bila katiba mpya ni sawa na kuziba mashimo ya Panya kwa Mikate!

Maana Tanzania uchaguzi ni mfumo sio tume tu.Nguvu ya Rais na wateule wake, polisi, TISS, Jeshi, Tume, Tamisemi na wengineo lazima viangaliwe kwa pamoja kupitia katiba mpya kwa kuwa vinahusiana na chaguzi.

Hiki kinachoitwa ni Tume huru ya uchaguzi ni changa la macho kwa wajinga ambao ndiyo wengi kwenye hii nchi.
 
CHADEMA upeo wenu ni mdogo sana kwenye mambo ya msingi! Kwanza mjiulize Katiba inayopendekezwa mnaikubali?! Pili nyie mnazungumzia Rasimu ya Warioba hatua ambayo ilishavukwa!
Sasa kwenye bunge la sasa CHADEMA mna nguvu gani ya ku-influence jambo lolote la maana against CCM!?
Watu wenye akili wanaona ni heri tupate tume huru ya Uchaguzi then ikiwezekana mpate Wabunge angalau kwenye Bunge then mapambano ya kupigania Katiba Bora yaendelee kupitia platforms za maana ikiwemo Bunge la JMT.
Tatizo CHADEMA kumejaa utoto utoto na harakati za kijinga jinga sana!
Suala la Katiba bora ni long race !
Ni kweli lakini wewe unafikili Upinzani hawamo bungeni just bcoz hawakubaliki? Just bcoz hawakuchaguliwa? Kwa mtu mwenye akili sawa sawa anaweza kujibu ndy swali hili?
 
CHADEMA upeo wenu ni mdogo sana kwenye mambo ya msingi! Kwanza mjiulize Katiba inayopendekezwa mnaikubali?! Pili nyie mnazungumzia Rasimu ya Warioba hatua ambayo ilishavukwa!
Sasa kwenye bunge la sasa CHADEMA mna nguvu gani ya ku-influence jambo lolote la maana against CCM!?
Watu wenye akili wanaona ni heri tupate tume huru ya Uchaguzi then ikiwezekana mpate Wabunge angalau kwenye Bunge then mapambano ya kupigania Katiba Bora yaendelee kupitia platforms za maana ikiwemo Bunge la JMT.
Tatizo CHADEMA kumejaa utoto utoto na harakati za kijinga jinga sana!
Suala la Katiba bora ni long race !
Ikiwa unaona kila kitu kinachoongelwa usichokipenda ni lazima kiwe cha kutoka Chadema, hata huko CCM watakuwa waanakuona wewe ni mzibgo uliye na IQ ya chini sana
 
Back
Top Bottom