Watu wasiofahamika wa Usalama wana nguvu kuzidi demokrasia ya Watanzania wote

Watu wasiofahamika wa Usalama wana nguvu kuzidi demokrasia ya Watanzania wote

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Kama ni kweli Serikali imetumia usalama kugushi makaratasi ya uchaguzi, kupanga matokeo ya uchaguzi Tanzania nzima na kufilisi wapinzani wafanyabiashara na hata kuwajeruhi au kushiriki kwa namna yeyote kwenye mauaji ya wapinzani ni tishio kubwa sio tu kwasasa lakini kwa miaka mingi sana ijayo.

Tatizo kubwa kuna watu wanafikiri hili ni jambo la mpito tu lakini ukweli ni kwamba usalama wa taifa umejipa kazi isiyo ya kwao. Hiki kitengo hakitakuwa cha awamu moja maana ukisha onjesha madaraka makubwa hivi kwa idara moja haina tofauti sana na nchi kutawaliwa kijeshi.

Je, hii ina maana gani? Hii ina maana kwamba usalama unakuwa na nguvu kuliko Wananchi hivyo hakutakuwa na sababu ya Wagombea wa nafasi tofauti kuwafuata wananchi badala yake wanaweza kuwafuata viongozi wa chama na usalama pekee kwani ndiyo wachaguaji wa ukweli sio wananchi. Lakini la pili kwenye hili ni kwamba usalama utakuwa na nguvu ya kutishia bunge zima hadi Mawaziri.

Kwa wale washabiki hasa wenye elimu inaelekea wanashabikia kitu ambacho hawajui au wamejidanganya kwasababu tu wanampenda Magufuli na mambo anayofanya. Hili sio sawa maana bila mfumo mzuri wa kidemokrasia tunaweza kuwa na Raisi mbaya na hatutaweza kumtoa kwa namna yeyote. Lakini vilevile unaweza ukawa na viongozi wabaya usalama wenye malengo binafsi na wakamtisha mpaka raisi wa nchi maana serikali imewapa vitu na uwezo ambao hawatakiwi kuwa nao. Hatuwezi kukaa na kusali tu nkwamba kila siku tutapata watu bora kwenye hizi idara au hata Uraisi hivyo mnaoshangilia sana mjue mabadiliko haya makubwa inawezekana kabisa akapewa kiongozi ambaye si mzalendo na nchi yetu inaweza kurudi nyuma kwa miaka mingi bila na kuwa na sheria yeyote ya kumtoa.

Umri wa kati wa Watanzania ni miaka 17-18 tu hivyo Tanzania ina watoto wengi ambao hawawezi kugoma, kuandamana wala kuelewa mambo mengi kwa upana na wale wachache wanaoelewa wamekuwa vipofu kwa manufaa binafsi au kwa mapenzi yao. Binadamu ni kama maua yenye harufu nzuri mwisho wake yanaharibika hata yawe mazuri vipi. Hii ndiyo sababu pekee pamoja na mapenzi yangu binafsi kwa Magufuli jinsi alivyobadilisha siasa hasa kwa upinzani na CCM ilivyoshinda kwa kutumia usalama imeweka pengo kubwa ambalo itakuwa ngumu kuziba.
 
Ndivyo ilivyo usalama wa taifa inamzidi nguvu Rais na Mihimili mingine yote ndio ameruhusu usalama kusimamia zoezi la kupiga kura nchi sasa inafokewa na marafiki zetu wote
 

“Watu wasio fahamika usalama kuzidi demokrasia ya Watanzania wote”​

Hwading has no meaning!
 
Kama ni kweli Serikali imetumia usalama kugushi makaratasi ya uchaguzi, kupanga matokeo ya uchaguzi Tanzania nzima na kufilisi wapinzani wafanyabiashara na hata kuwajeruhi au kushiriki kwa namna yeyote kwenye mauaji ya wapinzani ni tishio kubwa sio tu kwasasa lakini kwa miaka mingi sana ijayo...
Kwa mfumo wa sasa sisiemu hawahitaji kuwa na wagombea wazuri, maana wapiga kura hawana sauti
 
Nitajitahidi kama wewe ulivyokosea lakini usipoteze nguvu na himuda wako kutafuta makosa ya wengine badala yake tumia muda huo kujifunza itakusaidia kwenye maisha yako ni wazo tu
Nasikitika watu hawaoni au ni vipofu.

Tunazama kiuchumi!

Hapa viwanda vimefungwa wawekezaji wanakimbiaTRA inakuwa mumiani inadhulumu na kunyanganya.

BOT nayo imedhulumu fedha za watu dola wamefilisi!

Nani awekeze hapa?

Kubomoa ni rahisi kujenga ni kazi!

Time will tell!!
 
Usalama unaburuzwa na watu ambao wako juu ya sheria na katiba ya nchi. Kama wengine walichimbwa biti kuwa yeye ndiye anayewalipa, unategemea hawa ni tofauti? Kwani si yeye ndiyo anaowalipa usalama pia kama wale wakurugenzi na wakuu wa wilaya nk?
 
Wale ambao wapo juu ya katiba na sheria, bado tena wana kinga ya kutoshitakiwa. Na hapo ni katiba mpya ndo inamaliza hili tatizo.
 
Kama ni kweli Serikali imetumia usalama kugushi makaratasi ya uchaguzi, kupanga matokeo ya uchaguzi Tanzania nzima na kufilisi wapinzani wafanyabiashara na hata kuwajeruhi au kushiriki kwa namna yeyote kwenye mauaji ya wapinzani ni tishio kubwa sio tu kwasasa lakini kwa miaka mingi sana ijayo....
 
Mkuu hakuna tena usalama wa Taifa. Huyo anayejiita mwendawazimu kawajaza wahuni huko wale wanaovaa magwanda ya kijani. Kila taasisi hapa Nchini imevurugwa na kufanywa kama vile ni taasisi ya wahuni wa maccm.
Kama ni kweli Serikali imetumia usalama kugushi makaratasi ya uchaguzi, kupanga matokeo ya uchaguzi Tanzania nzima na kufilisi wapinzani wafanyabiashara na hata kuwajeruhi au kushiriki kwa namna yeyote kwenye mauaji ya wapinzani ni tishio kubwa sio tu kwasasa lakini kwa miaka mingi sana ijayo..
 
Oneni TISS mnavyolaumiwa na wananchi inasikitisha sana TISS imeamuamua kumlinda mtu mmoja na kuwaumiza waTz walio wengi.TISS mnaonekana kuwa wasaliti kwa wananchi.JITAFAKARINI VIAPO VYENU NI KUITUMIKIA JMT NA SIO MTU MMOJA
Watanzania tulio wengi hatuna wasiwasi,mambo shwariiiiiiiii.
 
Watanzania tulio wengi hatuna wasiwasi,mambo shwariiiiiiiii.
Kama nilivyosema wachache ndiyo wataelewa Watanzania wengi asilimia 90% wanaangalia mlo wa kesho au wadogo.
 
Yani sisi TISS ya Nyerere tukiangalia yanayoendelea nchini tunatingisha vichwa vyetu nakusema WTF is going on.

Ila msijali tutapata Rais mwanamke hivi karibuni.
 
Kama nilivyosema wachache ndiyo wataelewa Watanzania wengi asilimia 90% wanaangalia mlo wa kesho au wadogo.
Exactly,na kama jambo halijamgusa basi kwake sio issue.Sad!
 
Back
Top Bottom