Watu wasiojulikana ndiyo msingi wa CCM kupoteza uchaguzi huu

Watu wasiojulikana ndiyo msingi wa CCM kupoteza uchaguzi huu

Noel france

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2012
Posts
1,104
Reaction score
917
Habari wanajukwaa!

Kiukweli uchaguzi wa mwaka huu ni wenye ushindani mkubwa sana, kwa pande zote.

Kwa upande wa chama tawala, turufu yao kuu ni ununuaji wa ndege, ujenzi wa miundombinu mbalimbali, pia kuleta mabadiliko ya kiuongozi ndani ya taasisi za serikali.

Kwa mfano: Katika baadhi ya taasisi za serikali hakuna ama zimepungua majigambo ambayo yalikuwa kero katika maofisi.
Lakini pia imeleta hofu kwa watumishi, kwa sababu ya kuogopana.

Vitu ambavyo vitaipelekea chama tawala kupoteza katika uchaguzi huu ni pamoja na:

1) Hofu kwa wananchi juu ya watu wasiojulikana.

2) Utawala usioheshimu utawala wa sheria.

3) Wateule kujiona miungu watu N.K

Kwa upande wa upinzani especially CHADEMA wana nafasi kubwa ya kuweza kuthubutu kuchukua nchi upande wa Tanzania bara, lakini pia kwa upande ACT wazalendo vivyohivyo wana nafasi kubwa ya kutawala katika uchaguzi wa mwaka huu haswa kwa upande wa Visiwani.

Vitu pekee vitokavyo vibeba vyama vya upinzani ni madhaifu na mapungufu yaliyojitokeza katika utawala wa sasa pia wananchi walio wengi kutaka kuona mabadiliko ya kiongozi na kimfumo.

Pia, kutakuwepo na kura ya huruma kwa mgombea aliyenusurika na kifo.

Pia viongozi wote wa upinzani wameonesha Uzalendo wao uliotukuka macho mwa wapiga kura wao na wanachama wao.

Pia kitu chaziada kitakacho wabeba wapinzani ni kule kutakwa kuonwa na kusikilizwa wao baada ya kufungiwa kwa muda mrefu kwenye majukwaa ya kisiasa.

Je, wewe mtazamo wako ni upi? Naomba kuwasilisha hoja.
 
Vitu pekee vitokavyo vibeba vyama vya upinzani ni madhaifu na mapungufu yaliyojitokeza kati utawala wa sasa pia wananchi walio wengi kutaka kuona mabadiliko ya kiongozi na kimfumo.
Duniani kote katika siasa za uchaguzi kinachobeba upande pinzani, ni mapungufu katika upande madarakani/tawala, ukitaka kushinda kesi katika Jinai, a competent advocate will create reasonable doubt! LAKINI lazima Judge/ Hakimu awe na werevu wa kuiona hiyo reasonable doubt so created/ presented by defence team.
 
Duniani kote katika siasa za uchaguzi kinachobeba upande pinzani, ni mapungufu katika upande madarakani/tawala... ukitaka kushinda kesi katika Jinai, a competent advocate will create reasonable doubt! LAKINI lazima Judge/Hakimu awe na werevu wa kuiona hiyo reasonable doubt so created/ presented by defence team!
Kiukweli wananchi mahaba yameongezeka kwa upinzani.

2485784_117195765_3213508722074131_2911542144163865371_n.jpg
 
Jpm yako mambo kajitakia, hakukuwa na haja ya kutuma wasiojulikana kudhuru wapinzani wake kisiasa
Pia kunyima uhuru wa kupata habari, imeleta changamoto na manung'uniko ya chini kwa chini.
 
Huwezi kuonekana ni bora bila ya kuonesha kilicho dhaifu.

CCM wamekazania sana, eti enezeni sera badala ya kuelezea upungufu wa CCM. Huo ni ujinga. Siku zote kwenye mashindano yoyote, ukitaka kushinda, kwanza uyajue mapungufu ya mpinzani wako, na hapo kwenye upungufu wake, ndipo ulipo ushindi wako. Mapungufu yake uyaseme kwa nguvu na ustadi wote ili wapiga kura wayajue na wamkatae.

Awamu hii mapungufu makubwa kabisa, kama alivyonena mtoa mada:

1) Watu kudhulumiwa maisha. Awamu hii ndiyo iliyoleta utaratibu wa kuteka, kuua, kutesa na kupoteza watu wanaoikosoa Serikali au Rais. Kuua na kuteka ni matendo ya kishetani. Hakuna hata muumini mmoja wa dini yoyote, hata ya jadi atakayeamini kuwa utawala huu upo na Mungu. Kazi ya kuua ni ya shetani. Hivyo wengi wanaufungamanisha utawala wa awamu hii na shetani, japo wanapebda sana kutaja jina la Mungu. Utawala wa Mungu umejaa huruma, upendo, msamaha na umoja.

Utawala wa awamu hii umejitambulisha kama utawala wa mabavu, visasi, chuki na ubaguzi. Mapungufu haya yatasemwa sana na wapinzani, na ni halali yasemwe maana hakuna kinachozidi usalama wa maisha ya mwanadamu. Hata ungenunua ndege, ukajenga reli au mabwawa ya umeme n.k; hizo ndege na barabara, watatumia nani kama kila atakayekosoa, hayupo duniani au anapotea tu, haieleweke yupo wapi.

2) Uonevu. Awamu hii ndiyo iliyoleta utaratibu mpya wa kuwaonea watu na kuwabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha. Wanawaweka watu mahabusu kwa muda mrefu kisha wanakulazimisha ukiri makosa. Hakuna hata mtuhumiwa mmoja ambaye iliwahi kuthibitika kwenye mahakama kuwa alihusika na hayo makosa. Wote wanaokiri wanafanya hivyo ili kuyaepuka mateso. Huu ni utaratibu mbaya na hovyo kabisa. Unawakamata watu, unawatesa kisha unawalazimisha wakiri makosa.

3) Wasiojulikana kupewa ruhusa ya kufanya chcohote. Katika awamu hii ndiko kumeanzisha kikundi cha wasiojulikana ambacho hakiguswi na yeyote. Na hao wanaweza kufanya chochote ambacho wengine hawaruhusiwi kufanya. Angalia uchafu wa Bashite kuanzia kwenye vyeti. Angalia matusi na vitisho vya msiba au gumbo. Tumeacha mfumo rasmi wa utawala, na kuweka vikundi vinavyofanya kazi kama vikundi vya kigaidi.

4) Kuanguka kwa Ukuaji wa Uchumi. Watu wengi hawajui lakini ukweli ni kuwa katika awamu hii, ukuaji wa uchumi kwenye sekta zote za uchumi, umeanguka. Ukuaji wa uwekezaji umeanguka toka 28% (2015) mpaka 4% (2019), ukuaji wa sekta ya utalii umeanguka toka 15% (2015) mpaka 3.6% (2019), thamani ya mauzo ya nje ya mazao ya kilimo mwaka 2019 yalianguka kwa 50%. Kushuka kwa uwekezaji kumesababisha tatizo kubwa kwenye ajira.

5) Utawala wa Mungu Mtu. Kwenye awamu hii, kuanzia Rais mpaka wateule wake, karibia wote wanaongoza kama miunguwatu. Hawaangalii sheria wala kanuni bali wanachotamka ndiyo sheria.

Yapo mengi ya hovyo kama sheria za kidikteta zinazohusiana na uhuru wa vyombo vya habari, upatikanaji taarifa, uhuru wa maoni, demokrasia, n.k. Kwa ujumla, mazuri ni machache ukilinganisha na mabaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi kuonekana ni bora bila ya kuonesha kilicho dhaifu.

CCM wamekazania sana, eti enezeni sera badala ya kuelezea upungufu wa CCM. Huo ni ujinga. Siku zote kwenye mashindano yoyote, ukitaka kushinda, kwanza uyajue mapungufu ya mpinzani wako, na hapo kwenye upungufu wake, ndipo ulipo ushindi wako. Mapungufu yake uyaseme kwa nguvu na ustadi wote ili wapiga kura wayajue na wamkatae...
Nashukuru mkuu kwa Kuchangia, Kunakitu nilikisahau juu ya kunyimwa wapinzani ama wakosoaji wa serikali haki ya kuishi
 
Kwa mambo yaliyotokea Arusha,Moshi na Mbeya yanasaidia kuipasha upinzani lakini pia uwezekano mkubwa wa viashiria vya mchafuko wa amani ama mpasuko kwa Taifa.

Pia ni mambo ambayo naweza kusema wateule wamelewa madaraka na kujiona wao ndiyo miungu watu.

Chuki inayojengekeka ndani ya mioyo ya Watanzania,itakuwa mbaya sana pale itakapotokea dalili za moshi.
 
Kwa mambo yaliyotokea Arusha,Moshi na Mbeya yanasaidia kuipasha upinzani lakini pia uwezekano mkubwa wa viashiria vya mchafuko wa amani ama mpasuko kwa Taifa.

Pia ni mambo ambayo naweza kusema wateule wamelewa madaraka na kujiona wao ndiyo miungu watu.

Chuki inayojengekeka ndani ya mioyo ya Watanzania,itakuwa mbaya sana pale itakapotokea dalili za moshi.
Ningekuwa afande Sibula pale mbeya, sio tuu ningemtia mjeki sugu Bali angechezea kichapo kikali.
 
Viongozi wetu wanapaswa kujitafarikari kwanza pasipo kulewa madaraka, wakumbuke lolote litalotokea kutaleta madhara kwa pande zote.

Viongozi aina mkuu fulani wa wilaya kule moshi na yule officer fulani kule mbeya,kiutaribu wamekosea sana kumfanyia vile kwa kumdhalilisha Mh sugu. Viongozi mnapaswa kujichunga kwa kila kitu mnachokifanya.
 
Ningekuwa afande Sibula pale mbeya, sio tuu ningemtia mjeki sugu Bali angechezea kichapo kikali.
Lakini anatengeneza chuki kwa jamii, pia italeta shida kwake na familia yake. Haya ni maoni yangu kwako na kwake
 
Back
Top Bottom