Watu watano wafariki dunia baada ya Lori kufeli breki kwenye mlima Mbalizi, Mbeya

Watu watano wafariki dunia baada ya Lori kufeli breki kwenye mlima Mbalizi, Mbeya

Juzi pale mikumi, Morogoro, Lori limefeli brake na kuingia ndani ya nyumba iliyoko pembeni mwa barabara na kuuwa mtu mmoja..
Haya maisha ya duniani tunaishi lakini hatujui ni lini tutaondoka ,na kifo kinakuja kwa njia mbalimbali cha msingi ni kuomba mungu atujalie afya njema,unaweza ukajiwekea ulinzi na usalama wa kila namna kwa gharama zozote na za juu mwisho wa siku, ukaondoka
 
Hi
Maskini Kamanda Mpinga aliyekua RPC Mbeya aliwahi kutolewa kafara na Mwendazake kwa kushushwa cheo. Kisa ni kwanini hakukagua gari lililotokea Tabora na kuja kupatia ajali Mbeya usiku mwingi kwa ku fail brake!!!

Marehemu alikua akitaka kula kichwa chako basi atakutafutia lolote la kukutosha na kukubandika nalo huku ukiwa huna pa kujitetea[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

R. I. P wote waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo
Hiv Huyu Kamanda kashasttafu mana ç'i msikii tena
 
Serikali inashauriwa KILA siku ule mpando wa mbalizi utamaliza watu pale iwe one way pekee na sio two way. Malori kufeli brake ni wimbo wa taifa pale
 
Wataalamu wa mechanics hivi Hakuna namna ya kulock tairi za tela zisizunguke pindi brake inapofeli. Au tairi za nyuma za kichwa zisizunguke Ili gari isiende mbele?
 
Serikali inashauriwa KILA siku ule mpando wa mbalizi utamaliza watu pale iwe one way pekee na sio two way. Malori kufeli brake ni wimbo wa taifa pale

Nadhani pale serikali imeamua wananchi wake wafage tuuu!
 
Wataalamu wa mechanics hivi Hakuna namna ya kulock tairi za tela zisizunguke pindi brake inapofeli. Au tairi za nyuma za kichwa zisizunguke Ili gari isiende mbele?

Ishuke pekee au ipande pekee
 
Imezoeleka kila mwisho wa mwaka ndipo jeshi la polisi linakuja na hamsha hamsha kusimamia usalama barabarani, ikiwa ni pamoja na kufuatilia mabasi ambayo imeonekana ndiyo chanzo kikubwa cha ajali.

Miezi kadhaa sasa ajali zimeongozana na baadhi ya hizo zimeshuhudiwa zikitokana na maroli au waendesha pikipiki a.k.a bodaboda.

Kwa wiki hii iliyoisha mpaka leo jumatatu ni ajali kama nne zimetokea na kuleta madhira kwa jamii.

Najiuliza, kwa nini hali hii, nikikumbuka kipindi fulani huko nyuma wakati kama huu iliwahi kutokea ajali mbaya na watu kufa.
 
R.I.P Mwl John,alikuwapo ajali Hio.

Mke wake alikufa mwaka Jana akijifungua,akamwachia kichanga...dah nae ametembea.

Huruma sana kwa watoto.
 
Watu watano wamefariki Dunia na wengine wanne kujeruhiwa mkoani Mbeya baada ya Lori la Mizigo kufeli breki kwenye mteremko wa Mlima Mbalizi na kuyagonga magari madogo matatu, Bajaji na watembea kwa mguu.

==========================

Akizungumzia kuhusu taarifa hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei amesema: “Tukio lililotokea ni Machi 27, 2022 baada ya Scania kufeli breki ikaenda kugonga Bajaji kisha ikagonga mwendesha pikipiki na kusababisha vifo vya watu wawili.

“Waliofariki ni Jermiah Mwasega na Suza Mbwiga ambaye alikuwa ni dereva wa bodaboda.”

Kuhusu madai ya watu watano kufariki amesema anachojua yeye waliofariki ni wawili na ndiyo ripoti aliyonayo.


==============================================

AJALI YA GARI KUACHA NJIA KUGONGA MAGARI 02 BAJAJI NA PIKIPIKI NA KUSABABISHA VIFO NA MAJERUHI.

Mnamo tarehe 27.03.2022 majira ya saa 21:18 usiku huko katika Barabara ya Mbeya – Tunduma, Kata ya Utengule Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya na Mkoa wa Mbeya.

Gari yenye namba za usajili T. 909 DQC na tela namba T.205 DSF aina ya Scania likiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la ABDULRAZACK HASSAN alishindwa kulimudu gari hilo akiwa anashuka Mlima Lwambi baada ya kufeli break na kwenda kugonga Bajaji yenye namba ya usajili MC.999 CUD aina ya TVS King iliyokuwa uelekeo mmoja ikiendeshwa na SHUKRANI PAUL na kusababishia majeruhi.

Baada ya hapo ikagonga Gari yenye namba ya usajili T.128 ALE aina ya Nissan Double Cabin ikiendeshwa na EMMANUEL MAKONGANYA na kusababisha kifo kwa JEREMIAH MWASENGA ambaye alikuwa abiria kwenye gari hiyo, kisha kugonga Gari yenye namba ya usajili T.387 DBD aina ya Toyota Noah iliyokuwa ikiendeshwa na dereva ANYENGULILE MWAMULUKI na mwisho kugonga Pikipiki yenye namba ya usajili MC.205 ARK aina ya T-Better iliyokuwa ikiendeshwa SUSA MBWIGA na kumsababishia kifo.

Katika ajali hiyo watu wawili wamejeruhiwa na wanaendelea na matibabu Hospitali Teule ya Ifisi – Mbalizi.

Aidha, vyombo vyote vilivyohusika katika ajali hiyo vimeharibika. Chanzo cha ajali ni kufeli breki ya Gari Lori yenye namba ya usajili T.909 DQC/T.205 DSF Scania na kusababisha dereva kushindwa kulimudu Gari hilo.

Jeshi la Polisi mkoani hapa nilimshikilia Dereva wa Gari T.909 DQC/T.205 DSF Scania kwa hatua zaidi za kisheria.

Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA


=======================================================

Mungu asante kwa kumlinda Mchungaji Mwamluku na wengine waliopona katika ajali hii. Mtumishi huyu anachunga kanisa la TAG Isamilo Jijini Mwanza.
 
Ule utaratibu wao wa malori na gari ndogo kupita kwa zamu uliishia wapi??
Lile zoezi wangelisimamia vizuri lingesaidia sana kupunguza ajali mlima mbalizi.

Tatizo ni pale gari kubwa bado hazijamaliza kushuka kutoka iwambi na kule mbalizi washaruhusu gari ndogo zianze kupanda.
Workdone inakuwa sawa na sifuri.


Timing inakosekana.
Wangepiga hesabu za muda vizuri kwamba tukiruhusu hizi gari kushuka basi zitachukua muda fulani kumalizika..
Lakini utashangaa wanaangalia tu baada ya nusu saa wanaruhusu gari ndogo zianze kushuka na kupanda.
Matokeo yake zile gari ndogo zinatokea kule chini Mbalizi kwa pupa zinakutana na Malori yaliyotoka Iwambi bado hayajamalizika na baadhi ya Lori pia zinakuwa hazimaliza kupanda .. matokeo yake ni ajali.
 
Back
Top Bottom