Kwa nyaraka zilizopo,shughuli hiyo itakuwa jioni.Leo,Bunge la Katiba linafikia vifungu vya 37,38 na 39 vya Rasimu ya Kanuni za Bunge hilo ili kuvipitisha.Vifungu tajwa,pamoja na mambo mengine, vinazungumzia namna ya upigaji kura wa kupitisha Rasimu ya Katiba utakavyokuwa ndani ya Bunge hilo.Wapo wa KURA YA SIRI na KURA YA WAZI/DHAHIRI. Leo watajulikana vyema.
Lazima leo Bunge liamue kupitisha au kuviondosha vipengele hivyo vya Kanuni. Ni leo.Si kesho. Lakini, kupitisha SIRI au DHAHIRI kutafanywa kwa SIRI au DHAHIRI? Mwenyekiti wa muda ataongozwa na Kanuni au Taratibu zipi leo kuamua kuendesha kura za SIRI au DHAHIRI wakati itakapojitokeza haja ya kufanya hivyo? Leo kitaeleweka tu.Zege halilali!
Sent from my iPhone