Watuhumiwa wa Ubakaji na Ulawiti mbioni kukosa dhamana

Watuhumiwa wa Ubakaji na Ulawiti mbioni kukosa dhamana

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Makosa ya ubakaji na ulawiti yapo mbioni kuondolewa dhamana kutokana na Serikali kuanza mchakato wa kufanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Hatua hiyo imetokana na utafiti mdogo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuonesha kuwa baadhi ya watuhumiwa wa makosa hayo wakiwa nje kwa dhamana wanakimbia na wengine kuharibu ushahidi au kumalizana na wazazi ama ndugu wa muathirika wa vitendo hivyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Happy Msimbe, aliyasema hayo jana kwenye kikao kilichowakutanisha wataalam na wadau wa masuala ya sheria kutoka Wizara, Taasisi za serikali ili kutoa mapendekezo ya sheria hiyo.

Alisema nia ya kukutana na wataalam hao ni kupata maoni yatayosaidia kujenga hoja ya kufanya makosa hayo kutokuwa na dhamana ili kupunguza matukio hayo kwa jamii.

Mkurugenzi huyo alisema wanalenga kulinda kundi la watoto na wanawake ambao ni waathirika wa vitendo vya ukatili.

“Kikao hiki kimelenga kuangalia na kupitia sheria nyingine ambazo zinamgusa mtoto ili ziweze kuendana na hali halisi iliyopo katika jamii ili kuwasaidia watoto wanaofanyiwa vitendo vya ukatili katika jamii,” alisema

Chanzo: Nipashe
 
Naunga mkono hoja 100% ila msije kuitumia sheria vibaya kuwasingizia watu kuwakomoa na kesi kama hizi wa kujuwa hakuna dhamana ila zitumike kwa watu kweli ili likomeshe haya mambo ya hovyo katika jamii yetu kusiwe na huruma na hawa mbwa. angalizo tu sheria nzuri tusitumie kukomoana kama utakatishaji wa fedha.
 
Huyu mkurugenzi ni mshenzi sn, watu wanataka makosa yote yawe na dhamana yeye analeta ujinga ujinga hapa, asubiri mume wake siku anawekwa ndani kwa makosa ya kubambikwa aone huu ujinga wake.
 
Huyu mkurugenzi ni mshenzi sn, watu wanataka makosa yote yawe na dhamana yeye analeta ujinga ujinga hapa, asubiri mume wake siku anawekwa ndani kwa makosa ya kubambikwa aone huu ujinga wake.
Vipi Mwanao akibakwa au akilawitiwa?🤨
 
sio dhamana tu, kukiwa na clear evidence kesi isidhidi mwezi mmoja, watolewe viungo vyao wakiwa wazima viuzwe (kuanzia figo na kila kinachohitajika) miili yao ichukuliwe ikaushwe kwa ajili ya experiment vyuo.

Hukumu ikitoka tu ni marufuku hata kuona na ndugu zao.
 
Huyu mkurugenzi ni mshenzi sn, watu wanataka makosa yote yawe na dhamana yeye analeta ujinga ujinga hapa, asubiri mume wake siku anawekwa ndani kwa makosa ya kubambikwa aone huu ujinga wake.
Naona wabakaji na walawiti wa watoto mmekuja juu! Mkuu muache hiyo tabia, mtafia jela
 
Huyu mkurugenzi ni mshenzi sn, watu wanataka makosa yote yawe na dhamana yeye analeta ujinga ujinga hapa, asubiri mume wake siku anawekwa ndani kwa makosa ya kubambikwa aone huu ujinga wake.
Endelea na tabia yako utakiona cha mtema kuni
 
Wanawake wengi ndo hufanya haya yatokee
embu sheria iwekwe na w.ke wafungwe jpo miaka 5 halafu tuone kma yatatokea tena haya ila tatizo w.ke wanaachiwa na wamepewa uhuru wa kutosha

M.ke atembea mapaja wazi na mzazi hamgombi mwanawe kinachotokea ni maelezo baada ya habari
 
Makosa ya ubakaji na ulawiti yapo mbioni kuondolewa dhamana kutokana na Serikali kuanza mchakato wa kufanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Hatua hiyo imetokana na utafiti mdogo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuonesha kuwa baadhi ya watuhumiwa wa makosa hayo wakiwa nje kwa dhamana wanakimbia na wengine kuharibu ushahidi au kumalizana na wazazi ama ndugu wa muathirika wa vitendo hivyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Happy Msimbe, aliyasema hayo jana kwenye kikao kilichowakutanisha wataalam na wadau wa masuala ya sheria kutoka Wizara, Taasisi za serikali ili kutoa mapendekezo ya sheria hiyo.

Alisema nia ya kukutana na wataalam hao ni kupata maoni yatayosaidia kujenga hoja ya kufanya makosa hayo kutokuwa na dhamana ili kupunguza matukio hayo kwa jamii.

Mkurugenzi huyo alisema wanalenga kulinda kundi la watoto na wanawake ambao ni waathirika wa vitendo vya ukatili.

“Kikao hiki kimelenga kuangalia na kupitia sheria nyingine ambazo zinamgusa mtoto ili ziweze kuendana na hali halisi iliyopo katika jamii ili kuwasaidia watoto wanaofanyiwa vitendo vya ukatili katika jamii,” alisema

Chanzo: Nipashe
Mtu hana hatia mpaka ithibitike na mahakama kuwa ana hatia. Kumejengeka tabia miongoni mwa jamii kuona kuwa kila anayetuhumiwa kwa ubakaji/ulawiti basi alitenda kweli makosa hayo. Hivyo a
Aanapoachiwa na mahakama kwa kutokuwa na hatia inaonekana amevuruga ushahidi au hakimu ksaa rushwa.. Mbona kwa makosa mengine watu wanadhinda kesi?
Kwanza mifumo yetu inatoa mwanya watu kubambikiwa kesi kuanzia na polisi, maafisa wa serikali na hata jamii yenyewe ili kumkomoa mtu.

Kama ni kuvuruga ushahidi kesi zote mtu anaweza kuvuruga ushahidi hivyo kama inaonekana dhamana haitakiwi basi iwe kwa,makosa yote.

Hoyu afisa asiingize uanaharakati katika haki za watu. Mwanae akituhumiwa kumbaka housegirl wake atakubali kwanza mwanae awekwe rumande?
 
Makosa ya ubakaji na ulawiti yapo mbioni kuondolewa dhamana kutokana na Serikali kuanza mchakato wa kufanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Hatua hiyo imetokana na utafiti mdogo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuonesha kuwa baadhi ya watuhumiwa wa makosa hayo wakiwa nje kwa dhamana wanakimbia na wengine kuharibu ushahidi au kumalizana na wazazi ama ndugu wa muathirika wa vitendo hivyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Happy Msimbe, aliyasema hayo jana kwenye kikao kilichowakutanisha wataalam na wadau wa masuala ya sheria kutoka Wizara, Taasisi za serikali ili kutoa mapendekezo ya sheria hiyo.

Alisema nia ya kukutana na wataalam hao ni kupata maoni yatayosaidia kujenga hoja ya kufanya makosa hayo kutokuwa na dhamana ili kupunguza matukio hayo kwa jamii.

Mkurugenzi huyo alisema wanalenga kulinda kundi la watoto na wanawake ambao ni waathirika wa vitendo vya ukatili.

“Kikao hiki kimelenga kuangalia na kupitia sheria nyingine ambazo zinamgusa mtoto ili ziweze kuendana na hali halisi iliyopo katika jamii ili kuwasaidia watoto wanaofanyiwa vitendo vya ukatili katika jamii,” alisema

Chanzo: Nipashe
Safi lazima watoto walindwe kwa Hali na mali.
 
Waondoe dhamana kwenye makosa ya rushwa na ufisadi ili wakubwa waonje joto ya jiwe
 
Back
Top Bottom