Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Watu wawili wanaodaiwa kushirikiana na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu yakiwamo makosa yajinai wanashikiliwa na polisi mkoani Kilimanjaro.
Kaimu Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Kilimanjaro, Arterio Kawonga alisema uchunguzi wa matukio yaliyofanywa na Sabaya mkoani humo unaendelea na unafanywa na timu kutoka makao makuu ya ofisi hizo.
Juni 4, mwaka huu Sabaya alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na wenzake watano kusomewa mashtaka sita, likiwamo la uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kupokea rushwa.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Juni 18 na kusomewa mashtaka mawili yeye na wenzake wawili ambayo upelelezi wake ulikuwa umekamilika.
“Uchunguzi wa matukio aliyoyafanya Sabaya Kilimanjaro bado unaendelea, utakapokamilika tutawapa taarifa maana bado suala hili lipo mkononi mwa timu yetu kutoka makao makuu, bado wanaendelea na uchunguzi na taarifa ambazo zimepokewa zinaendelea kufanyiwa kazi,” alisema Kawonga.
“Kuna kesi nyingine za kijinai ambazo zipo polisi na tayari kuna watuhumiwa wawili tuliwakabidhi polisi Mkoa wa Kilimanjaro, wengine ni walewale anaoshtakiwa nao Arusha aliofanya nao matukio katika wilaya za Hai na Moshi.”
Juni 15,mwaka huu Kamanda wa Takukuru mkoani humo, Frida Wikesi alisema wanaendelea kuchunguza tuhuma nyingine saba zinazomkabili Sabaya alizozifanya wakati akiwa mkuu wa wilaya.
Wikesi alisema wapo watu wanatajwa kushirikiana na Sabaya kufanya uhalifu na endapo uchunguzi ukithibitisha walihusika, watafikishwa mahakamani.
Pia, alisema wote wanaotajwa kushirikiana na Sabaya kufanya uhalifu katika mkoa huo chunguzi dhidi yao zinaendelea ili waliotendewa uhalifu huo, haki zao zipatikane.
Juni 18, katika Mahakama hiyo, Wakili wa Serikali Mkuu Tumaini Kweka na wenzake, Abdallah Chagula na Tarsila Garvas, walisoma mashtaka hayo mbele Hakimu Mfawidhi, Martha Mahumbuga na Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mshasha huku watuhumiwa wakiwa wanatetewa na Wakili Moses Mahuna.
Kweka alisema upelelezi katika makosa mawili ya ujambazi wa kutumia silaha yaliyokuwa yanawakabili Sabaya na walinzi wake wawili upelelezi umekamilika na wapo tayari kuwasomea maelezo.
Akisoma maelezo hayo, Gervas alisema Februari 9, mwaka huu, Sabaya na watuhumiwa wawili Silvester Nyengu na Daniel Mbura, walivamia duka la Mohamed Saad lililopo Mtaa wa Bondeni.
Alisema katika mashtaka hayo ya unyang’anyi walitumia silaha ambayo ni kinyume cha kifungu cha 287(a) cha mwenendo wa makosa ya jinai, kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, watuhumiwa hao baada ya kuvamia duka hilo, waliwalaza sakafuni, kuwapiga na kuwatishia kwa bunduki, Bakari Msangi ambaye ni diwani wa Sombetini (CCM) na Ramadhani Khatibu.
Gervas alisema watuhumiwa hao waliiba Sh390,000 fedha za Msangi, baada ya kumtishia kwa bastola na kabla ya kumpora, Silvester alimfunga pingu Msangi.
Katika kosa la pili watuhumiwa hao walimtishia kwa bunduki Khatibu na kumpora Sh35,000 na simu aina ya Tecno.
Baada ya kusomewa mashtaka, waliyakana na Hakimu Salome aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 2, mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa.
Hata hivyo, Wakili Mahuna aliomba upande wa mashtaka kumkabidhi hati ya mashtaka katika shauri hilo na maelezo ya walalamikaji.
Mwananchi
Kaimu Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Kilimanjaro, Arterio Kawonga alisema uchunguzi wa matukio yaliyofanywa na Sabaya mkoani humo unaendelea na unafanywa na timu kutoka makao makuu ya ofisi hizo.
Juni 4, mwaka huu Sabaya alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na wenzake watano kusomewa mashtaka sita, likiwamo la uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kupokea rushwa.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Juni 18 na kusomewa mashtaka mawili yeye na wenzake wawili ambayo upelelezi wake ulikuwa umekamilika.
“Uchunguzi wa matukio aliyoyafanya Sabaya Kilimanjaro bado unaendelea, utakapokamilika tutawapa taarifa maana bado suala hili lipo mkononi mwa timu yetu kutoka makao makuu, bado wanaendelea na uchunguzi na taarifa ambazo zimepokewa zinaendelea kufanyiwa kazi,” alisema Kawonga.
“Kuna kesi nyingine za kijinai ambazo zipo polisi na tayari kuna watuhumiwa wawili tuliwakabidhi polisi Mkoa wa Kilimanjaro, wengine ni walewale anaoshtakiwa nao Arusha aliofanya nao matukio katika wilaya za Hai na Moshi.”
Juni 15,mwaka huu Kamanda wa Takukuru mkoani humo, Frida Wikesi alisema wanaendelea kuchunguza tuhuma nyingine saba zinazomkabili Sabaya alizozifanya wakati akiwa mkuu wa wilaya.
Wikesi alisema wapo watu wanatajwa kushirikiana na Sabaya kufanya uhalifu na endapo uchunguzi ukithibitisha walihusika, watafikishwa mahakamani.
Pia, alisema wote wanaotajwa kushirikiana na Sabaya kufanya uhalifu katika mkoa huo chunguzi dhidi yao zinaendelea ili waliotendewa uhalifu huo, haki zao zipatikane.
Juni 18, katika Mahakama hiyo, Wakili wa Serikali Mkuu Tumaini Kweka na wenzake, Abdallah Chagula na Tarsila Garvas, walisoma mashtaka hayo mbele Hakimu Mfawidhi, Martha Mahumbuga na Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mshasha huku watuhumiwa wakiwa wanatetewa na Wakili Moses Mahuna.
Kweka alisema upelelezi katika makosa mawili ya ujambazi wa kutumia silaha yaliyokuwa yanawakabili Sabaya na walinzi wake wawili upelelezi umekamilika na wapo tayari kuwasomea maelezo.
Akisoma maelezo hayo, Gervas alisema Februari 9, mwaka huu, Sabaya na watuhumiwa wawili Silvester Nyengu na Daniel Mbura, walivamia duka la Mohamed Saad lililopo Mtaa wa Bondeni.
Alisema katika mashtaka hayo ya unyang’anyi walitumia silaha ambayo ni kinyume cha kifungu cha 287(a) cha mwenendo wa makosa ya jinai, kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, watuhumiwa hao baada ya kuvamia duka hilo, waliwalaza sakafuni, kuwapiga na kuwatishia kwa bunduki, Bakari Msangi ambaye ni diwani wa Sombetini (CCM) na Ramadhani Khatibu.
Gervas alisema watuhumiwa hao waliiba Sh390,000 fedha za Msangi, baada ya kumtishia kwa bastola na kabla ya kumpora, Silvester alimfunga pingu Msangi.
Katika kosa la pili watuhumiwa hao walimtishia kwa bunduki Khatibu na kumpora Sh35,000 na simu aina ya Tecno.
Baada ya kusomewa mashtaka, waliyakana na Hakimu Salome aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 2, mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa.
Hata hivyo, Wakili Mahuna aliomba upande wa mashtaka kumkabidhi hati ya mashtaka katika shauri hilo na maelezo ya walalamikaji.
Mwananchi