Watuhumiwa wenzake na Mbowe yawezekana kweli waliteswa na kupigwa, lakini je hawakupanga kushiriki njama za ugaidi?

Ni vigumu sana kudifine ugaidi katika ngazi ya kimataifa maana Sheria ya ugaidi ni ya kimataifa.kwa hawa wameshtakiwa kwa kupanga maandamano yasiyo na ukomo,kutaka kulipua vituo vya mafuta (ambavyo mpaka sass havijajulikana)na kutaka kudhuru viongozi.katika mambo you're haya kunahitajika uthibitisho usio tia shaka kuwa tia hatiani.ni kazi ya mahakama kupima ushahidi utaoletwa na upande wa jamhuri kisheria kama unajitosheleza.rejea tukio la mwakab1998 ubalozi wa marekani uliposhambuliwa dar,walikamatwa watu zaidi ya 200 lakini Cha kushangaza walipotua FBI walisema hakuna hata mmoja miongoni mwa walikamatwa alihusika na ulipuaji .Bali wao walikuja na picha ya mtu aliyehusika.nakusema huyu ndiye anaetafutwa.ugaidi sio mchezo kama watu wengine wanavyo fikiri ugaidi ni kilele Cha uhalifu duniani ndio maana vita ya ugaidi ni ya ulimwengu mzima sio ya nchi moja.
 
Basi hakuna sababu ya kumlaumu CDF, tusubiri kwanza mahakama iamue, kama wale jamaa wana hatia wawajibike.
 
Ni sawa na kutakatisha fedha. Huwezi pata fedha kwa njia chafu inayovunja sheria halafu uje uanzishe kitu kwa fedha hiyo hiyo uliyoipata kwa nj8a chafu kwa kufuata sheria zote za uanzishwaji wa kitu hicho
 
Wapi nimeandika polisi wanayo haki ya kupiga?

Ishu ni kama walikiri kwa kupigwa na kuteswa na kweli walipanga kulipua vituo vya mafuta. Kama ni kweli mahakama itauchukua huo ushahidi.
Kinachoendelea kwa sasa ni kutaka kujua ukweli wa madai yenyewe.Suala la mateso linaangaliwa vizuri ili kujua kama watuhumiwa walitoa maelezo Yao katika mazingira huru kiasi gani.wananchi wengi bila kujali itikadi za vyama,tayari Wana mashaka makubwa juu ya uhalisia wa kesi yenyewe.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Tuinue mikono yetu kumuelekea Mola muumba wa mbingu na nchi atuletee amani na upendo vitamalaki nchini mwetu.
Tusiyoyajuwa tusiyazungumze.


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu umeilewa mada hapo juu? Umeelewa matiki ya kifungu cha 29 sheria ya ushahidi?
 
Kabisa yaani, mashaka ni makubwa sana... Ukiangalia ushahidi wa polisi jinsi wanavyojichanganya lazima upate mashaka. HALAFU;
1. JINSI STATION DIARY ILIVYOPOTEZA BAADHI YA KURASA NA NYINGINE KUONGEZEWA inatia shaka
2. Polisi wengine eti hawaijui PGO..!!! NI AJABU... ni sawa na Padre au mchungaji kutoijua biblia au Shehe kutoijua kurani..!!
 
Huenda kuna 'komanduu' (miongoni mwa hawa) alitumiwa na 'wapanga deal kusuka' hili
Hata hivyo mpango mzima ulisukwa hovyo sana na ndio maana mashahidi (maaskari) pamoja na kuwa trained kutoa ushahidi wa uongo wanapoteana mhakamani!
ILA Majaji wamepangwa kutoa hukumu inayoipendelea serikali, time will tell. ila ole wao siku ya kiyama hawa watu kwa ouvu huu.
 
Tupeni maiti ya Ben Saanane , au twambieni mlipo mfukia tukamfukue tumfanyie ibada mpendwa wetu.
MaCCM nyie ni MAUJI wakubwa. na Mlaaniwe MaCCM wote
 
Tuna mabunduki na akina nani? Tunazunguzia ishu iliyopo mahakamani,sisi ni raia . Je sheria za nchi zinasemaje?
Kingai na timu yake ndio mlituma kumuua Lissu na mabinduki yenu.?!
MaCCM nyie ni LAANAKUM katika nchi,
 
Lakini kwa kiasi kikubwa JPM alikosa hekima ndo kasababisha haya yote .Huwezi kuteua wakuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama kwa asilimia zaidi ya 90 kutoka Kanda Moja Yani Kanda ya ziwa .Hapo unakua umeondao uwajibikaji.Ni makosa makubwa yalifanyika na hii hali tusikubali itokee tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona makamandoo wamedhalilishwa sana.Inaogopesha.
 
Tupeni maiti ya Ben Saanane , au twambieni mlipo mfukia tukamfukue tumfanyie ibada mpendwa wetu.
MaCCM nyie ni MAUJI wakubwa. na Mlaaniwe MaCCM wote
Acha upuuzi
 
Naona makamandoo wamedhalilishwa sana.Inaogopesha.
Makamandoo kudhalilishwa inavyoonekana kwenye kesi ndo ilikuwa main issue kwamba watu wakisikia Mbowe ametumia makomandoo basi public au watu watashituka sana lakini imekuja kinyume chake badala ya watu kuweka taharuki wao wamekuwa upande wa makomandoo kwamba pia wanastahili kufanya kazi popote maana hawapo jeshini Sasa hicho kitu naona ndo kimeweka kesi kuwa ngumu ila watu wangewalaumu makomandoo kwenda kumlinda Mbowe kama ilivyotegemewa basi mashitaka sasahivi yangekuwa na nguvu kubwa kama nguvu iliyoupande wa Mbowe ilivyokubwa.
 
....wafuasi wa Chadema wanashupalia......usemi huu unaonesha upande ulioko wewe ambao ni wa mashitaka, kitendo hiki kinaondoa hadhi ya mada yako kujadiliwa kwani tayari unao uamuzi wako mfukoni.
 
Ndiyo swali linakuja ni sheria gani hiyo ya kupiga mtuhumiwa ili akiri hata kama ni mkosaji? Actually kama amekiri inatakiwa pamoja na kukiri kwake hao askari nao washtakiwe kwa kitendo hicho maana huko chuoni wamepewa mbinu kibao za kuujua ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…