Watuhumiwa zaidi waendelee kufutiwa mashtaka na kuachiliwa Huru

Watuhumiwa zaidi waendelee kufutiwa mashtaka na kuachiliwa Huru

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Waswahili walisema ndo ndo ndo si chururuu. Wala Lila na Fila havikupata kutengamana.

Hii ikiwa ni kwa maana halisi ya kuwa awamu ya sita si awamu ile ambayo mahabusu walikuwa wakipigiwa mahesabu kuwa chanzo cha nguvu kazi. Eti kuwa asiyefanya kazi na asile.

- DPP amewafutia kesi waliodaiwa kusafirisha wenye ulemavu, kuwatumikisha

Awamu ile ilitambua rasmi magereza kama chanzo muhimu cha nguvu kazi na mahakama kama chanzo kizuri cha mapato. Bila aibu ikapendekezwa hata mawakili watetezi wa watuhumiwa wawe nao wanaunganishwa vifungoni.

Nani alikuwa na uwezo wa kuyakemea yote haya yaliyokuwa yamepinda? Si bunge, si mahakama, si viongozi wa dini, si iliyojiita kamati ya amani ya dini, nk. Wote waliufyata!

Kwani nini vimezima mihemko ya legacy na kwamba kuifuatilia sasa hakupo tena? Kwani nini vimezima miito ya kuwa na waliokwenda days? Ikobwapi miito ya kuwa na baba wa pili wa taifa? Akili zinarejea. Kumbe kulikuwa na kupigwa upofu?!

Hongera mama Samia jitihada zako za kuikarabati hii nchi zimeonekana na zisiishie kuwa ni utashi wako binafsi. Isije ikawa hatari iko pale pale kuwa ukaja kutoka tukarejea tena Misri.

Mheshimiwa kumbuka ya Mungu mengi. Pamoja na wengi kukuombea ya heri ni nani aijuae kesho? Waswahili waliosema linalowezekana leo lisingoje kesho hakukosea.

Utayari wako kuijenga misingi imara ya nchi hii kuwa yenye haki siku zote bila kujali aliyeko madarakani, kutakuongoza kuliko kuwa na Mama halisi wa Taifa hili atakayekumbukwa daima.

Kwako Mama Samia rais wetu wa JMT ikikupendeza tafadhali, kazi inapoendelea.
 
Baba wa taifa alistahili wadhifa huo kwa busara zake na jitihada zake za dhati za kupigania Tanzania yenye usawa na haki.

Kama treni iliyo tayari kuondoka, mama Samia anaweza kuwa yuko njia moja kuelekea kuwa Mama wa taifa.
 
Kesi za kubambikiwa za kutengenezwa, ni heri arudishe heshima ya nchi ya utawala wa sheria.

Wanasheria wa serikali wafanye kazi kwa uhuru na weledi, siyo kwa matakwa ya wanasiasa.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Jana kuna jamaa katoka jela jirani yangu,yeye amefungwa juzi tu kwa kupangisha nyumba 1 watu wawili
 
mambo mengi ya kubumba yalifanyika mwendazake alipokuwepo, na bado yanaendelea kuwepo imagine Rais anaagiza kesi za kubumba zote zifutwe kimtu tu kama IGP kinasema kipewe miaka miwili, aisee nchi hii ni ngumu sana
 
Upumbavu.

Na mashekih walivyokamatwa walisingiziwa pia?

Kama hawakusingiziwa kulikua na kigugumizi kipi kuwahukumu muda wote waliokaa rumande?
kama sio Upumbavu wa akili zako na hoa waliowatesa mashekhe na wengine wengi waliobambikiwa kesi na kuteswa bure mahabusu
 
Kama hawakusingiziwa kulikua na kigugumizi kipi kuwahukumu muda wote waliokaa rumande?
kama sio Upumbavu wa akili zako na hoa waliowatesa mashekhe na wengine wengi waliobambikiwa kesi na kuteswa bure mahabusu
Usiwe unaoenda kufuata mkumbo kama mwanamke malaya..
Waliokuwa wanamwagia watu tindikali hawakufanya kosa walisingiziwa?
 
Usiwe unaoenda kufuata mkumbo kama mwanamke malaya..
Waliokuwa wanamwagia watu tindikali hawakufanya kosa walisingiziwa?

Acha ujinga fara we hivi uwamwagie watu tindikali halafu ukamatwe umemwagia watu tindikali inawezekana kukaa miaka yote minane bila kuhukumiwa ?
hivi wewe unatumia kiungo gani kufikiria kichwa au makalio?
 
Acha ujinga fara we hivi uwamwagie watu tindikali halafu ukamatwe umemwagia watu tindikali inawezekana kukaa miaka yote minane bila kuhukumiwa ?
hivi wewe unatumia kiungo gani kufikiria kichwa au makalio?
Nakupuuza maku wewe huna lolote umebakiza bla blah

Waliwamwagia au hawakuwamwagia watu?
 
Back
Top Bottom