Watumiaji wa mtandao wa X wamefilisika kifikra au?

Watumiaji wa mtandao wa X wamefilisika kifikra au?

Matakataka yashavamia huko, ni kama JF tu kipindi cha nyuma ilikuwa na watu smart sana na hata wale vilaza walikuwa na mipaka yao, lkn kwa sasa kumechafukwa vibaya.

Ni aina tu ya wajinga waliokosa contents kichwani basi wanaamua kupost kila aina ya mawazo yao wakitafta engagement kwa lazima.

Kwa sasa mtandao wa X ukiingia ukascroll nusu saa hujakutana na picha za uchi/contents za ngono basi shukuru sana.

Kwa Tanzania hii members wenye ushawishi huko X karibia 70% ni hao hao vijana wasio wastaarabu, wenye lugha chafu, uchochezi, wasambazaji maudhui ya hovyo, ngono na ujinga mtupu.

Kwa sasa hakuna tofauti kati ya instagram na X kimaudhui kwa upande wa Bongo, maana kote udaku,umbea wanashare, kinachosaidia kubalance maudhui angalau kuna baadhi ya watu wachache sana waliobase kwenye siasa angalau wanatoa ahueni ya maudhui.

Miaka 5 ijayo x itakuwa porn site/mtandao wa watu kujiuza, mtandao wa hovyo kuliko.

Sio mbaya ndio aina ya raia na akili zao tulio nao nchini, ambao ndio hawa hawa mitaani wanaojifanya kondoo kumbe mafichoni(nyuma ya keyboard) ni majangiri

Imagine kuna nyuzi zinaitwa WATOTO WAMELALA THREAD, huko ni hatari kabisa
Uwazi mkubwa sana kk
 
View attachment 3154876
Picha: Pinterest
Mimi nimeanza kutumia X kwa sasa toka 2017. Niliheshimu mtando huu sana kwa habari nzuri na kwa ufupi kutokwa kwa watu mbalimbali.

Leo hii unaingia X unakuta ndio watu wanaongoza kwa kusambaza video za ngono pamoja na kudhalilisha watu na mwisho naweza sema Facebook ni mtandao wa watu wastaarabu sana.

Jambo lingine ni tabia ya uchochezi wa taarifa hili ni kwamba watu wanasambaza taarifa za uongo kuchafua taswira ya mtu au watu na hili vijana wengi wa X wanaongozwa na hisia kuliko ukweli wa mambo.

Soma Pia: Netblocks: Mtandao wa X (Twitter) umepigwa pini nchini Tanzania

Pia, niwapongeze wale ambao wameendelea kutumia X katika kusaidiana na kujenga jamii kwa maandiko yao.

Hivyo nauliza huko X ni wanafunzi wa darasa la saba au watu wasomi?
Inategemea unawafollow watu gani. Ukiwafollow wapumbavu na usipowablock utakutana na upumbavu wao
 
Unaongelea X gani kwa sababu Mimi X ninayoijua sijawahi kutana na maudhui ya ajabu ajabu.
 
Kila kitu ulichoandika hapa siyo cha kweli,, me ni mtumiaji wa x (twitter) since 2014 lakini kuhusu ulichoandika hapa napingana nacho kabisa.

Unachopendelea kufuatilia zaidi ndicho kitakachokuwa kinaonekana sana upande wa Tl yako 😎🤝🏽
Kama mtu anaona face book ni bora kuliko x (twitter) huyo ni wakumsamehe.
 
Algorithm unapoperuzi irnakuwa inakuchekii tuu.
Macho yako yakidumuu kwenye kitu hicho kwa dakika 1 yenyewye inaamini unakiipenda.
Sasa ww umeona habari ya baltazarii,ukaona ile content imewekewa tahadhari ya ukungu na maelezo ya onto ww unaamua kuchungulia eeehh utoasogezewa nyuchi za kutosha maana inaona kumbe ww unapeendaa
 
Back
Top Bottom