Watumishi NBC wadai kudhalilishwa

Watumishi NBC wadai kudhalilishwa

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
BAADHI ya wafanyakazi wa Benki ya NBC,Tawi la Corporate jijini Dar es Salaam, wamedai kudhalilishwa na mabosi wao kwa kuvuliwa nguo zote.Wakizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, wafanyakazi hao walisema walifanyiwa hivyo Ijumaa iliyopita.

Tukio la wafanyakazi hao kufanyiwa unyama huo, tayari limeripotiwa polisi na kupewa kumbukumbu namba CD/RB/4073/2011 na CD/IR/1319/2011.

Mmoja wa wafanyakazi hao, Michael Matayo, alisema wafanyakazi waliofanyiwa udhalilishaji huo ni watano na kwamba ni wale wa kitengo cha usafirishaji fedha.Alisema siku ya tukio, walikuwa wanajiandaa kwenda kula na kwamba kabla ya kutoka lazima upite mageti matatu na kukaguliwa na mlinzi.

"Tulipofika geti la mwisho meneja wetu alituita akatuuliza mnajua tunachotaka kufanya, tukamwambia hatujui akasema tumsubiri nje,"alisema Matayo.Alisema baadaye waliitwa na kuingia chumba cha kubadilishia nguo chenye kamera ya CCTV na kwamba baada ya kutoka kwenye chumba hicho waliingia katika chumba kingine ambacho hakina kamera ya CCTV na kuanza kusachiwa.


Mfanyakazi mwingine aliyedai kudhalilishwa ni Ramadhan Mbwana, ambaye alisema kitendo hicho, kilidumu kwa dakika 20 na kwamba waliamriwa kuvua nguo zote na kubaki uchi na kuchuchumaa.

Alisema unyama huo ulifanywa na Mkuu wa Kitengo cha Usafirishaji Fedha katika benki hiyo ambaye ni raia wa Ghana."Baada ya kutusachi na kuridhika kuwa hatujaiba hela alituachia,"alisema Mbwana.

Wafanyakazi hao pia walidai kuwa Machi 19 mwaka huu, walifanyiwa udhalilishaji mwingine ambapo waliamriwa kunyanyua mikono juu kwa zaidi ya nusu saa, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kusachiwa.

Licha ya kuvuliwa nguo, wafanyakazi hao wamesema wamekuwa wakinyanyaswa kwa kutukanwa kudharauliwa na kufanyishwa kazi kwa muda mrefu.Hata hivyo, Meneja Uhusiano wa benki hiyo Robi Matiko,alisema hana taarifa kuhusu tukio hilo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, aikiri kuwa na taarifa kuhusu tukio hilo lakini alisema hawezi kuzieleza kwa undani zaidi kwa sababu hawajapata taarifa kamili.Uongozi wa NBC makao makuu nao ulisema hauna taarifa.
 
Nbc kuna mambo. Siku si nyingi nimesikia wanataka kugoma. Ujio wa Mafuru na Maharage Chande una kasoro.
 
Ndani ya nchi yetu? Nimesikia migodini, hata site senta?
 
tumewaleta hawa waghana waje wafanye kazi then wanaanza kutubagua weusi wenzao tena hapahapa kwetu
Nbc kuna mambo. Siku si nyingi nimesikia wanataka kugoma. Ujio wa Mafuru na Maharage Chande una kasoro.
 
Poleni wapiganaji wenzetu!hivi mimi naomba kuuliza swali moja tuu!hivi hawa wageni wa kiafrika wanaokuja kufanya kazi hapa nchini wanakuwa wapo juu ya sheria?manake hata ukienda sehemu ambazo kuna maboss ambao ni raia wa nchi jirani mfano Kenya wanatudharau sana sisi wabongo!hivi hicho kiburi wanakitoa wapi?hivi M bongo ukienda Kenya achilia mbali kupata kazi inakua ngumu kuupata huo u boss usahau kabisa!lakini kwa hapa kwetu kila kitu tambarare!
 
nchi yetu imekua kama shamba la bibi lisilo na mwenyewe ndio maana tunaendeshwa na kila mtu yaani wabongo hatuna msimamo kabsa na hatujiamini nadhani falsafa hii tunajengewa toka tukiwa shule yaani tumekua watu wa kunyanyaswa na kila mtu kisa eti tuna utu moyoni kweli jamani tuamke na tusimame kutetea haki zetu tuache uoga
Poleni wapiganaji wenzetu!hivi mimi naomba kuuliza swali moja tuu!hivi hawa wageni wa kiafrika wanaokuja kufanya kazi hapa nchini wanakuwa wapo juu ya sheria?manake hata ukienda sehemu ambazo kuna maboss ambao ni raia wa nchi jirani mfano Kenya wanatudharau sana sisi wabongo!hivi hicho kiburi wanakitoa wapi?hivi M bongo ukienda Kenya achilia mbali kupata kazi inakua ngumu kuupata huo u boss usahau kabisa!lakini kwa hapa kwetu kila kitu tambarare!
 
Poleni wapiganaji wenzetu!hivi mimi naomba kuuliza swali moja tuu!hivi hawa wageni wa kiafrika wanaokuja kufanya kazi hapa nchini wanakuwa wapo juu ya sheria?manake hata ukienda sehemu ambazo kuna maboss ambao ni raia wa nchi jirani mfano Kenya wanatudharau sana sisi wabongo!hivi hicho kiburi wanakitoa wapi?hivi M bongo ukienda Kenya achilia mbali kupata kazi inakua ngumu kuupata huo u boss usahau kabisa!lakini kwa hapa kwetu kila kitu tambarare!

Kuna haja ya sisi nasi kuwabagua wageni
 
Hawa mbona wamezoea kunyanyaswa!
Kunawakati nilisikia hawaruhusiwi kuingia mlango mmoja wala kupanda kwenye lift moja na wazungu wa South, pia kupark magari ndani ya fence, ni wazungu tu wanao ruhusiwa.
 
poleni sana ndugu zanguni wa NBC. ushauri ni kwamba tusiogope kutoa taarifa yanapotokea mambo kama hayo. ni udhalilishaji usiokuwa na mantiki yoyote ile. hata kama ni security ya fedha zao,kwani wameanza kusafirisha pesa leo? miaka yote walikuwa wanatumia mbinu gani kukagua staff wa kitengo hicho? usikute huyo mghana anamind kuchungulia dada zetu if nao wapo ktk department hiyo.
 
Hivi hawa NBC walisharudisha ile Server waliyoifunga south africa?
Branches na operations zote zinafanyika Tanzania iweje Server ikae south africa?
Yaani watanzania ni watumwa kwenye nchi yetu.
 
Sijui kwa nini watanzania tunanyanyasika ndani ya nchi yetu, tulizoea kwenye viwanda watu wanalalamika leo ni kwenye mabank ambamo tunaamini watu waliomo huko wengi wamesoma na wana uelewa na kujua haki zao na kuwa na uwezo wa kujitetea. sasa mtu anaambiwa anyunyue miko juu kwa muda mrefu hivyo na yeye anakubali.........hapo ipo kazi.
 
l used to work there, sera za ubaguzi zikanikimbiza.
mbona umenichanganya??

Ubaguzi ulikuondoa pale... lakini tena unasema Maharage na Mafuru kuja ndio mambo yakaharibika, sasa mbaguzi ni mafuru na maharage au hao foreigners?

I thought ujio wa mafuru na marage ndio unaashiria kupunguza ubaguzi?? hebu nisaidie dadangu
 
mbona umenichanganya??

Ubaguzi ulikuondoa pale... lakini tena unasema Maharage na Mafuru kuja ndio mambo yakaharibika, sasa mbaguzi ni mafuru na maharage au hao foreigners?

I thought ujio wa mafuru na marage ndio unaashiria kupunguza ubaguzi?? hebu nisaidie dadangu
Nazjaz hebu tusaidie kwa hili dada yetu
 
Faida ndogo ndogo za kuwakumbatia wanaoitwa wawekezaji toka nje,huu ni unyama...
 
BAADHI ya wafanyakazi wa Benki ya NBC,Tawi la Corporate jijini Dar es Salaam, wamedai kudhalilishwa na mabosi wao kwa kuvuliwa nguo zote.Wakizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, wafanyakazi hao walisema walifanyiwa hivyo Ijumaa iliyopita.

Tukio la wafanyakazi hao kufanyiwa unyama huo, tayari limeripotiwa polisi na kupewa kumbukumbu namba CD/RB/4073/2011 na CD/IR/1319/2011.

Mmoja wa wafanyakazi hao, Michael Matayo, alisema wafanyakazi waliofanyiwa udhalilishaji huo ni watano na kwamba ni wale wa kitengo cha usafirishaji fedha.Alisema siku ya tukio, walikuwa wanajiandaa kwenda kula na kwamba kabla ya kutoka lazima upite mageti matatu na kukaguliwa na mlinzi.

"Tulipofika geti la mwisho meneja wetu alituita akatuuliza mnajua tunachotaka kufanya, tukamwambia hatujui akasema tumsubiri nje,"alisema Matayo.Alisema baadaye waliitwa na kuingia chumba cha kubadilishia nguo chenye kamera ya CCTV na kwamba baada ya kutoka kwenye chumba hicho waliingia katika chumba kingine ambacho hakina kamera ya CCTV na kuanza kusachiwa.


Mfanyakazi mwingine aliyedai kudhalilishwa ni Ramadhan Mbwana, ambaye alisema kitendo hicho, kilidumu kwa dakika 20 na kwamba waliamriwa kuvua nguo zote na kubaki uchi na kuchuchumaa.

Alisema unyama huo ulifanywa na Mkuu wa Kitengo cha Usafirishaji Fedha katika benki hiyo ambaye ni raia wa Ghana."Baada ya kutusachi na kuridhika kuwa hatujaiba hela alituachia,"alisema Mbwana.

Wafanyakazi hao pia walidai kuwa Machi 19 mwaka huu, walifanyiwa udhalilishaji mwingine ambapo waliamriwa kunyanyua mikono juu kwa zaidi ya nusu saa, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kusachiwa.

Licha ya kuvuliwa nguo, wafanyakazi hao wamesema wamekuwa wakinyanyaswa kwa kutukanwa kudharauliwa na kufanyishwa kazi kwa muda mrefu.Hata hivyo, Meneja Uhusiano wa benki hiyo Robi Matiko,alisema hana taarifa kuhusu tukio hilo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, aikiri kuwa na taarifa kuhusu tukio hilo lakini alisema hawezi kuzieleza kwa undani zaidi kwa sababu hawajapata taarifa kamili.Uongozi wa NBC makao makuu nao ulisema hauna taarifa.


Yani Robi nae ndio jibu la kutoa?kwanini asingeendelea kwa kusema atafuatilia kiundani?! halafu ni mbongo,agrrrr!!
Kama hili tukio ni kweli ni unyanyasaji wa hali ya juu!
 
Back
Top Bottom