Watumishi wazoefu ndio wapelekwe Wizarani

Watumishi wazoefu ndio wapelekwe Wizarani

tutafikatu

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2011
Posts
3,327
Reaction score
4,624
Ukienda Wizara ya Afya, utakuta kuna watumishi kedekede, wanaosimamia jambo ambalo hawajawahi lifanya. Kuna wafamasia, ambao hawajawahi toa hata kidonge kimoja kwa mgonjwa, kuna madaktari ambao hata ndugu yake akiumwa Typhoid atapiga simu kwa daktari mzoefu hospitalini amtajie dawa nzuri. Kuna wauguzi ambao hawajui adha ya kugeuza mgonjwa maeneo kusikokuwa na magodoro maalumu. Hivi inakuwaje mtu hana uzoefu wa kutibu anasimamia sera zinazoendana na matibabu?

Hawa watu hawajui hata vifaa gani vinatakiwa katika taasisi zetu. Elimu waliyonayo ni ile waliyoipata shule. Hawana uzoefu zaidi ya kufanya utarajali tu (internship). Wanahusika kutengeneza miongozo ya magonjwa mbalimbali, lakini hawajawahi tibu hata mgonjwa mmoja. Kila wakati wanaenda kufanya mentorship na supportive supervision ya vitu wasivyovifahamu.

Watu hawa ndio wanatuangusha, kila siku wanashinda wakizunguka huku na huko na computer. Mtu kama huyu atajuaje changamoto zilizopo katika taasisi za afya? Changamoto zote zinapaswa uziishi.

Wengine wanaofanana na hawa ni wale ambao, alipofika tu Wilayani wakapewa ama uganga ufawidhi au uganga mkuu wa wilaya, na sasa ni makatibu wakuu au wakurugenzi kwenye wizara nyeti, hawajui adha za kuwa mdogo, hawajui changamoto za chini. Ni style ya Dr. Gwajima.

Tufuate mfumo wa Japan, unaanza ngazi ya kwanza kufika ngazi ya juu.
 
Kiuhalisia ndio mfumo uliokuwepo awali hadi pale tulipoanza kuingiza 'Makada' wenzetu kwenye nafasi za juu.
 
Mtoa mada,
Kama unafatilia vizur Raisi keshasema kila mbuz ale kwa urefu wa Kamba yake.

Kama kamba yako fupi Sana, Nikupe pole Sana mkuu.

Unachotakiwa kufahamu kwa sawa,
Hapa mjini cha muhimu ni connection, kadi ya Chama pamoja cv nzuri ya kukipigania chama na kujua kusoma na kuandika tu.

Mambo yako ya weledi,
Sijui uzoefu kazini,
Mara kupanda cheo kutokea chini.
Peleka uko uko nchini Japani Hiroshima na Nagasaki.

Nakukumbusha Tena,
Hapa nchini tuna makundi matatu,
1.wenye-nchi,
2. wana-nchi
3. wapigania-nchi

Maisha Ni Kupanga,
Na kupanga Ni kuchagua.
Na ktk kuchagua jitahidi sana uchague fungu lililosahii kwako,familia yako, ndugu zako na kizazi chako.

Ni hayo TU mkuu.

Alamsik[emoji106]
 
Tatizo ni kwamba kwenye nchi yetu maamuzi yanaanzia juu kushuka chini (centralization vs decentralisation)

Kama serikali kuu wangeshirikisha wadau wa nchi wenye weledi ktk wizara husika, kusingekuwa na tatizo lolote. Lakini baadhi ya maamuzi yanatolewa kwa mihemko na mtazamo wa watendaji walioko wizarani; matokeo yake watekelezaji wa hayo maamuzi wanashindwa kujua nini cha kufanya.

Hakuna uwiano sawa kati ya watunga sera (policy planners) na watekelezaji wa sera (policy implementers) na hilo ni tatizo katika kila sekta. Hasa elimu!
 
Ukienda Wizara ya Afya, utakuta kuna watumishi kedekede, wanaosimamia jambo ambalo hawajawahi lifanya. Kuna wafamasia, ambao hawajawahi toa hata kidonge kimoja kwa mgonjwa, kuna madaktari ambao hata ndugu yake akiumwa Typhoid atapiga simu kwa daktari mzoefu hospitalini amtajie dawa nzuri. Kuna wauguzi ambao hawajui adha ya kugeuza mgonjwa maeneo kusikokuwa na magodoro maalumu. Hivi inakuwaje mtu hana uzoefu wa kutibu anasimamia sera zinazoendana na matibabu?

Hawa watu hawajui hata vifaa gani vinatakiwa katika taasisi zetu. Elimu waliyonayo ni ile waliyoipata shule. Hawana uzoefu zaidi ya kufanya utarajali tu (internship). Wanahusika kutengeneza miongozo ya magonjwa mbalimbali, lakini hawajawahi tibu hata mgonjwa mmoja. Kila wakati wanaenda kufanya mentorship na supportive supervision ya vitu wasivyovifahamu.

Watu hawa ndio wanatuangusha, kila siku wanashinda wakizunguka huku na huko na computer. Mtu kama huyu atajuaje changamoto zilizopo katika taasisi za afya? Changamoto zote zinapaswa uziishi.

Wengine wanaofanana na hawa ni wale ambao, alipofika tu Wilayani wakapewa ama uganga ufawidhi au uganga mkuu wa wilaya, na sasa ni makatibu wakuu au wakurugenzi kwenye wizara nyeti, hawajui adha za kuwa mdogo, hawajui changamoto za chini. Ni style ya Dr. Gwajima.

Tufuate mfumo wa Japan, unaanza ngazi ya kwanza kufika ngazi ya juu.

Umepost kitu cha maana sana hongera yako na pia viongozi wenyedhamana wachukue hii kama hadidu rejea
 
Kiuhalisia ndio mfumo uliokuwepo awali hadi pale tulipoanza kuingiza 'Makada' wenzetu kwenye nafasi za juu.
Kweli kabisa. Mimi kila siku najiuliza , mtu kamaliza chuo moa kwa moja anakuwa DMO, DC, DED, DEO n.k. Huko shuleni hajawahi kuwa hata monitor wa darasa alafu anaongoza watu wenye elimu zaidi yake, uzoefu wa zaidi ya miaka 20, uadilifu usio na mashaka na sifa nyingine nyingi. Ndio maana baadhi ya viongozi wanajihusisha na jinai za kutisha. Hawachujwi. Tujitafakari.
 
Back
Top Bottom