Watz mkopo wote huu wa SGR wakati mlisema mtajenga kwa hela yenu

khaaaa yani unakuwa mtumwa kwenye nchi yako mwenyewe?? kudadadeki!!
kweli Kenya ina wenyewe...
Ukisikia mateso wanayoyapata na jinsi mradi walivyotapeliwa utashika kichwa. Yani mchina ndio anaendesha mradi na wanamlipa karibia billion kumi kila mwezi nje ya deni lake.
 
halafu huyu jamaa sijui anatokea wapi ye anafikiri akilala akiamka atakuta reli tayari..haaaaaa haaaaaa aki ya nani wakenya hamuishi vituko..
Naishiaga kushika kichwa tu na kujichekea, wanasikitisha Sana aisee.
 
Kwa hiyo wewe ulivyo msikia Heche akiuliza uka ona yes na mimi nimepata cha kuongea! Unakuja humu unarudia maneno ya Heche kama yalivyo! Siku nyingine usiseme reli imejengwa kwa mita ngapi, sema mradi ume kamilika kwa asilimia ngapi? tafuta taharifa, mbona vitu vipo wazi.
 
Sisi tunashughulikia kwanza vyombo vya habari na makanisa hiyo ya SGR nimesema sipangiwi.
 


Geza, I think you missed his point. Yeye amesema hapo juu kukopa sio vibaya. Kile tu amesema ni kwamba TZ walisema wana hela za kutosha, ila sasa wanakopa. Wewe hapa unajadili juu ya hela ngapi nchi zimetumia kujenga ambapo haikuwa pointi yake.

Narudia tena kusema kwamba amesema "kukopa sio vibaya". Anajadili kwamba Tz sasa wameanza kukopa lakini hakujadili mambo na hela ngapi nani amekopa.
 
Wewe ni sawa na wale wazee wanaouliza wazungu kama kweli wamefika kwenye mwezi, kwanini wasiupake rangi tuone?

Reli haianzi kwa kutandika mataruma ... and that is not even the hardest , time consuming and expensive part of building an electric powered railway.

Jisomee.
 
Well noted Mkuu.
 
aisee wewe kama ni jogoo utakuwa unaatamia.si utembee tembee hata youtube au tatizo bundle????
 
Cha kuchekesha ni kwamba JPM anasema reli na ndege zimwjengwa kwa cash, lakini kwa miaka jana na juzi, ripoti ya benki kuu Tz inaonyesha Tz imekopa deni la zaidi ya $1.9B kutoka kwa wafadhili tofauti... hizi pesa ziliingia directly kwa bajeti...kwahivyo just bevause hazikutangazwa zinatumika kwa sector gani, haimaanishi hakutenga hizi pesa za loan kwa ujenzi wa sgr ... na hata kama hakutenda directly, atakua alichukua pesa za afya na kutumia kujenga SGR kisha akatumia pesa za mkopo kujaza pengo la bajeti ya afya... vyovyote vile alivyofanya ukweli ni kwamba alikopa hela..... kama angekua hakukopa kitu kabisa miaka hiyo miwili ndo ningeamini
 
Phase 1 na 2 zimeshajengwa mita ngapi?
Au ni kuweka vizimba na kuzindua phase 3 tu?
Ahaa kumbe na mkopo pia ipo eehh!
Sasa jamaa anavyotamba ni fedha za ndani tu na mnamuitikia kama mazuzu bongo zenu zinakuwaga zina utapiamlo..?
Hii kali mkuu,ulitaka ianze kutandazwa reli kabla ya kuweka kuweka vizimba,km sio wivu unaokusumbua bhas utakua comedian,na inawezekana nyumba yako utaanzaa kuweka paa kabla ya kujenga msingi na boma!
 
Yaani jamaa anajikomba kwa wakenya bila hata aibu, aisee.
Punguani huyo alafu kwan rais alisema hatuto kopa??? 700km kwa fedha za ndani sio mchezo buda. Je hao nyang'au walijenga hata mita moja ya SGR kwa fedha yao? Alafu anaforce eti nioneshen hata mita moja kwani wewe ni nani, subir muda tuliokubaliana na mkandarasi ufike hapo utakua na haki ya kuhoji kama mlipa kodi wa nchi hii. Acha kiherehere kijana.
 

From day one Watanzania wenye akili timamu tunajua huo ni uongo mtupu kwa sababu vyanzo vyetu vya mapato tunavijua haviwezi kama kutosha kugharamia mradi mkubwa kama ule hata kwa nusu, TUNA VIONGOZI WAPENDA SIFA TU HATA WASIPOSTAHILI
 
Watz hapa msijifanye mnajua mengi kuliko waKenya kwa ujenzi wa reli... sisi tumeshuhudia reli yetu ikijengwa hadi ilipokamilika, kwahivyo tukiwaambia reli yenu imechelewa ujenzi kidogo tunajua tunasema nini ...

Hata hivyo, sitarajii kuona reli imelazwa anytime soon huko Tz. labda tu ile temporary rail hulazwa kutoka kwa kiwanda cha kokoto au saruji hadi pale reli inajengwa... hii ni kwasababu reli ya Tz ni continuous, kwahivyo reli haiwezi ikalazwa nusu nusu, itawabidi wangojee hadi kila kitu kingine kiwe tayari kabla ya kuanza kulaza reli...

lakini hata hivyo, bado nilitarajia baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa, tz sgr ingekua imeliga hatua kubwa sana! especially vile mlitangaza mnajenga usiku na mchana... kama unataka kujua ni nini nilitarajia muwe mmefanya, pitia ukurasa wa kwanza wa hii mada hapa ujione Kenya sgr ilikua imefika wapi mwaka mmoja baada ya ujenzi

Kenya: The Standard Gauge Railway Takes Shape
 
Hahaha kichapo watanzania wanachowagawia chadomo huko kwenye kata ni lazima muwawewesekee wakenya unfortunately hawawezi kuwapigia kura 2020

Kwahiyo kichapo cha mbwa koko kipo pale pale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…