Wauza mahindi: Hatuna mahindi tena Tanzania, yaliyopo yanatoka Zambia na Malawi

Kalime kwanza halafu ukishavuna ndio ushauri mipaka ifungwe.
 
Licha ya kwamba huyo kaongea upotoshaji ila kikubwa mahindi yapo ya kutosha swala la wapi yanatoka sio dili..

Kama Zambia na Malawi wanatulisha Basi waambie wafunge mipaka tuone Kama hatuna mahindi kwenye maghala yetu..

Huku Mkoa niliko mahindi yameshashuka Bei kwa Sasa maana mvua zinanyesha na mahindi ya mabustanini yameanza kuingia sokoni
 
Kwani Zambia huko unazani ni nini? Si GMO? au unazania GMO yana rangi tofauti?
Pia Zambia wanazalisha settlers wale waliokuwaga Zimbabwe..

Ikumbukwe kabla ya kufukuza Wazungu Zimbabwe ndio alikuwa mzalishaji namba 1 wa Mahindi Africa
 
Malawi nae kwenye mahindi hataki mchezo ashapiga ban sema yanavuka kimagendo tu sababu vichochoro vingi
Ataachaje kupiga ban wakati Hana mahindi ya kutosha?

Mahindi yaliyopo kwenye vihenge tuu vya Serikali yanatosha kuwalisha mwaka mzima.
 
Mahindi ya kuuza kutoka Tanzania ndo hakuna
Ghala la Taifa wamefunga

Zambia wananunua mahindi kwenye ghala la Taifa la Zambia

Sijui kwanini watu husema maneno nusu nusu.
 
February mahindi kutoka Bonde la ziwa y Rukwa yatakuwa yamekomaa,kwanza Disemba hii mahindi ya mabustanini yanakuwa tayari sokoni kwa Wingi maana hupandwa kiangazi.

Mkoa niliko Hakuna mwezi hatuli mahindi ya kuchoma na kande mbichi,ningekuwa misele saiz ningekupigia picha nikuoneshe mahindi mabichi sokoni..

Kwa hiyo acheni kutosha watu na mwaka huh nalima ili nije kupiga Pesa next year kwa Bei za 80,000-105,000 tulizouzia mwaka huu..

Tunaomba ukame iendelee kuwanyoosha huko mikono kwenu ili tupige pesa.Hakuna hata siku Moja Nyanda za Juu Kusini ikakosa mvua ila zinaweza pungua tuu.
 
Upo mkoa gani?
 
Mbona tunaagiza ngano haiwi issue muhimu asife mtu kwa njaa.
 
Sasa si mpaka ghala la taifa liishiwe wakala wa serikali wa ghala la taifa si ndio kazi yao kuhifadhi hicho chakula , kwa sasa wafanyabiashara wao ndio kazi yao kuuza kama ndani wamekosa lazima wakanunue nje na wakala hawezi kutoa chakula ghala la taifa mpaka nchi iwe na njaa rejea zama zile za jk Tanzania inajitosheleza haiwezi kufikia huko.
 
Mwakani basi mahindi yatakavyoshuka bei[emoji3061]

Debe la mahindi litauzwa mpaka elfu3.
 
Hatari kwakweli
 
Kwani kuna mtu amekufa kwa njaa au ameomba chakula kwa sababu ya njaa Tanzania.

kama hakuna basi nchi inajitosheleza kwa chakula
Kutoka bei ya unga shs 1000 mpaka shs 2000 unasema hakuna shida?!!!

Kuna watu hata mlo mmoja wa familia siku hizi ni mtihani,dharau na kebehi hazifai.

Price inflation ni kubwa sana kwenye kila bidhaa.

Rais Hussein Mwinyi kule Zanzibar analifanyia kazi vizuri sana hili tatizo,huku bara wafanyabiashara wanajiamulia tu na dola inawapigia makofi!!
 
Sema kaka ww ungekuwa mfanyabiashara ungecomment hivi???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…