Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
WAZALENDO SABA WALIOLALA KIMYA KWA MUDA MREFU NDANI YA SEFU YA ALLY SYKES
Hukaa kimya fikra zangu ghafla zikagutushwa na kitu nikakigeuza ndani ya kichwa changu kisha nikajiuliza ilikuwaje, nani alihusika na nini sababu yake?
‘’Nakumbuka kama jana Ally Sykes ananyoosha kidole ukutani ofisini kwake Mtaa wa Makunganya kuniambia, ‘’Nina file nyingi ndani ya sefu hapo.’’
Naangalia lakini siioni hiyo sefu ninachoona ni ukuta na kabati kubwa.
Nimeingia ofisi hiyo mara nyingi lakini hakunipitikia kuwa pale kuna sefu.
‘’Sijua ufunguo wake uko wapi lakini nitautafuta ikiwa sitaupata nitamwita fundi aje tuvunje.’’
Jumatano ilipofika nimekwenda ofisini kwa Ally Sykes.
‘’Nimeziona funguo za sefu.’’
Ally Sykes akasimama kutoka kwenye meza yake akaenda ukutani akavuta milango ya kusukuma (sliding) ya kabati akafungua sefu na kuanza kutoka mafaili.
‘’Chukua mafaili hayo yasome ukimaliza njoo tuzungumze.’’
Imekuwaje tumefika pale Ally Sykes kuitolea mafaili yake?
Joseph Kasella Bantu alikuwa ameandika makala katika gazeti ya New African akieleza masikitiko yake kwa historia ya TANU kutopewa umuhimu unaostahili.
Mimi nilimuunga mkono Kasella Bantu katika toleo lililofuata lakini nikasema kama nikutoa msaada Kasella Bantu atakuwa katoa msaada gani wa kumshinda Abdul Sykes?
Ally Sykes alipedezewa sana na majibu yangu akamtuma mwanae aniite nikamuone.
Ndipo nikamwambia kumaliza haya matatizo ya historia ya TANU bora niandike kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.
Ally Sykes akaniambia kuwa amekuwa na fikra ya kutafuta watafiti kuandika historia ya marehemu kaka yake lakini hajalifanya hilo.
Nikamuomba mimi hiyo kazi.
‘’Mohamed wewe kweli unaweza kuandika?
Hivi ndivyo ikatokea kwa Ally Sykes kunikabidhi nyaraka zile.
Kuanzia file la kwanza nilipoanza kusoma nilikuwa natoka katika miaka ya 1980 najikuta niko katika Tanganyika inayotawaliwa na Waingereza.
Nilikuwa kama mtu niliyepagawa.
Akili yangu haifikiri kitu chochote isipokuwa utafiiti uliokuwa umenikabili.
Nilimwambia Ally Sykes baada ya kupitia nyaraka chache kuwa siwezi kusubiri hadi nimalize kusoma mafaili yote.
Ally Sykes akanipangia kila Jumamosi nakwenda ofisini kwake namhoji nay eye anazungumza na mimi namrekodi kwenye cassette player.
Katika mazungumzo yetu alitoa amri kwa katibu muhtasi wake Bi. Zainab kuwa hataki simu wala hapokeI mgeni.
Ni kama vile hivi sasa Ally Sykes yuko mbele yangu anazungumza na mimi ofisi yote kimya ila kwa sauti ya kinasa sauti kikizunguka na kutoa sauti ya chini.
Leo nataka nikuwekeeni hapa picha za wazalendo saba waliolala usingizi kwa miaka mingi ndani ya sefu ya Ally Sykes hadi siku nilipowaamsha na wakaamka kutoka Dar es Salaam ile ya miaka 1920 wakajikuta wako katika Dar es Salaam nyingine kabisa ya 1980.
Watu hawa walikuwa wamelala usingizi fofofo wa zaidi ya nusu karne.
Hii kwangu ilikuwa hadithi ya Rip Van Winkle.
Kila aliyewasoma lau kama walikuwa wanawajua kwa kuwaona na wengine kwa kuwasikia walikuwa wakishangaa na kujiuliza watu hawa walikuwa wapi miaka yote hii?
Haya tunayosoma ya kweli au porojo?
Ukwei ni kuwa hawa wazalendo walikuwa ndani ya sefu ya Ally Sykes kwa miaka wakisubiri kuamshwa.
Walipotoka usingizini na kuamka niliwaomba wanipe no. za kadi zao za TANU walizokata mwaka wa 1954 baada ya TANU kuasisiwa:
1. Julius Kambarage Nyerere Kadi No. 1
2. Ally Kleist Sykes Kadi No. 2
3. Abdulwahid Kleist Sykes Kadi No. 3
4. Dossa Aziz Kadi No. 4
5. Denis Phombeah Kadi No. 5
6. Dome Okochi Budohi Kadi No 6
7. Abbas Kleist Sykes Kadi No. 7
(Kuna taarifa nyingine zinasema kuwa kadi No. 7 ni ya John Rupia)
Picha zote ingia hapo chini:
Hukaa kimya fikra zangu ghafla zikagutushwa na kitu nikakigeuza ndani ya kichwa changu kisha nikajiuliza ilikuwaje, nani alihusika na nini sababu yake?
‘’Nakumbuka kama jana Ally Sykes ananyoosha kidole ukutani ofisini kwake Mtaa wa Makunganya kuniambia, ‘’Nina file nyingi ndani ya sefu hapo.’’
Naangalia lakini siioni hiyo sefu ninachoona ni ukuta na kabati kubwa.
Nimeingia ofisi hiyo mara nyingi lakini hakunipitikia kuwa pale kuna sefu.
‘’Sijua ufunguo wake uko wapi lakini nitautafuta ikiwa sitaupata nitamwita fundi aje tuvunje.’’
Jumatano ilipofika nimekwenda ofisini kwa Ally Sykes.
‘’Nimeziona funguo za sefu.’’
Ally Sykes akasimama kutoka kwenye meza yake akaenda ukutani akavuta milango ya kusukuma (sliding) ya kabati akafungua sefu na kuanza kutoka mafaili.
‘’Chukua mafaili hayo yasome ukimaliza njoo tuzungumze.’’
Imekuwaje tumefika pale Ally Sykes kuitolea mafaili yake?
Joseph Kasella Bantu alikuwa ameandika makala katika gazeti ya New African akieleza masikitiko yake kwa historia ya TANU kutopewa umuhimu unaostahili.
Mimi nilimuunga mkono Kasella Bantu katika toleo lililofuata lakini nikasema kama nikutoa msaada Kasella Bantu atakuwa katoa msaada gani wa kumshinda Abdul Sykes?
Ally Sykes alipedezewa sana na majibu yangu akamtuma mwanae aniite nikamuone.
Ndipo nikamwambia kumaliza haya matatizo ya historia ya TANU bora niandike kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.
Ally Sykes akaniambia kuwa amekuwa na fikra ya kutafuta watafiti kuandika historia ya marehemu kaka yake lakini hajalifanya hilo.
Nikamuomba mimi hiyo kazi.
‘’Mohamed wewe kweli unaweza kuandika?
Hivi ndivyo ikatokea kwa Ally Sykes kunikabidhi nyaraka zile.
Kuanzia file la kwanza nilipoanza kusoma nilikuwa natoka katika miaka ya 1980 najikuta niko katika Tanganyika inayotawaliwa na Waingereza.
Nilikuwa kama mtu niliyepagawa.
Akili yangu haifikiri kitu chochote isipokuwa utafiiti uliokuwa umenikabili.
Nilimwambia Ally Sykes baada ya kupitia nyaraka chache kuwa siwezi kusubiri hadi nimalize kusoma mafaili yote.
Ally Sykes akanipangia kila Jumamosi nakwenda ofisini kwake namhoji nay eye anazungumza na mimi namrekodi kwenye cassette player.
Katika mazungumzo yetu alitoa amri kwa katibu muhtasi wake Bi. Zainab kuwa hataki simu wala hapokeI mgeni.
Ni kama vile hivi sasa Ally Sykes yuko mbele yangu anazungumza na mimi ofisi yote kimya ila kwa sauti ya kinasa sauti kikizunguka na kutoa sauti ya chini.
Leo nataka nikuwekeeni hapa picha za wazalendo saba waliolala usingizi kwa miaka mingi ndani ya sefu ya Ally Sykes hadi siku nilipowaamsha na wakaamka kutoka Dar es Salaam ile ya miaka 1920 wakajikuta wako katika Dar es Salaam nyingine kabisa ya 1980.
Watu hawa walikuwa wamelala usingizi fofofo wa zaidi ya nusu karne.
Hii kwangu ilikuwa hadithi ya Rip Van Winkle.
Kila aliyewasoma lau kama walikuwa wanawajua kwa kuwaona na wengine kwa kuwasikia walikuwa wakishangaa na kujiuliza watu hawa walikuwa wapi miaka yote hii?
Haya tunayosoma ya kweli au porojo?
Ukwei ni kuwa hawa wazalendo walikuwa ndani ya sefu ya Ally Sykes kwa miaka wakisubiri kuamshwa.
Walipotoka usingizini na kuamka niliwaomba wanipe no. za kadi zao za TANU walizokata mwaka wa 1954 baada ya TANU kuasisiwa:
1. Julius Kambarage Nyerere Kadi No. 1
2. Ally Kleist Sykes Kadi No. 2
3. Abdulwahid Kleist Sykes Kadi No. 3
4. Dossa Aziz Kadi No. 4
5. Denis Phombeah Kadi No. 5
6. Dome Okochi Budohi Kadi No 6
7. Abbas Kleist Sykes Kadi No. 7
(Kuna taarifa nyingine zinasema kuwa kadi No. 7 ni ya John Rupia)
Picha zote ingia hapo chini: