Wazanzibari bado wanataka OIC, Watanganyika tubariki tuyaone maendeleo

Wazanzibari bado wanataka OIC, Watanganyika tubariki tuyaone maendeleo

Kasema hawataki kuletewa pundamilia...

kumbe Tanganyika wanagawa mpaka maliasili kwa Zanzibar...

Hakuna watu mazuzu duniani kama Watanganyika

Julius Nyerere, Baba wa Taifa la mazezeta, vizazi vya mbele vinavyosoma shule binafsi, na vyenye access ya tehama ya kuwafumbua upeo kama watu wengine duniani, watakuja kusema alivyokuwa na uelewa wa Chifu Mangungo
Kwani hukuona kwenye tamasha la Kizimkazi walipelekwa wanyama mbalimbali hadi simba aliyepewa jina la Tundu Lissu?
 
Labda kama hukuwepo wakati ule, watu walikuwa wanatoa maoni kwa uhuru kabisa na wala hakukuwa na questionnaire ya kujaza!
Hakuna uhuru wa kutoa maoni kama kujadili kuvunja muungano ni kosa la uhaini.

Hilo kosa linatakiwa kuondolewa kwanza kabla ya wewe kuweza kusema kwamba watu walitoa maoni kwa uhuru.

Ukisikia Wazanzibari wanasema wanataka serikali tatu au wanataka serikali ya mkataba, hiyo ni uephemism.

Euphemism ni neno la Kiingereza, maana yake ni kutumia neno au dhana isiyo na makali sana, wakati unamaanisha jambo lenye makali zaidi.

Kwa mfano, mtu anaenda chooni, lakini hasemi anaenda chooni, anasema anaenda "uani".

Nafikiri kwa Kiswahili euphemism inaitwa tafsida.

Sasa Wazanzibari wengi wakisema wanataka muungano wa serikali tatu, muungano wa mkataba etc, hiyo mara nyingi ni euphemism, wanasema wanaenda uani wakati wanamaanisha wanaenda chooni.

Wengine wanataka kuuvunja muungano, ila wanaanza polepole kwanza.

Wapewe nafasi tu kupiga kura katika kura ya maoni ya huru na haki.

Kura hii itakuwa na faida mbiki.

Kama Wazanzibari wengi wanautaka muungano, tutalijua hilo na muungano utaimarika, wasioutaka watajulikana kuwa ni wachache.

Na ikiwa Wazanzibari wengi hawautaki muungano, kura hii itawapa nafasi ya kuondoka kwenye muungano na kuanzisha nchi yao wenyewe tuondokane na kelele za kila mara kuhusu muungano.
 
Hapa Kuna mradi umekamilika hata mmoja?
 
Katiba ni ngumu sana kwa walio wengi, kwa vile Zanzibar ina uhuru wa mambo yake ya ndani yasiyo ya muungano, hivyo wakadhani wanaweza kujiunga tuu, hivyo wakajiunga.

Kumbe Zanzibar sio nchi, OIC ni ya nchi. Ilipofika Bungeni wabunge wakachamaa ikalazimishwa kujitoa kwa ahadi ya Tanzania kujiunga.
Kitendo hicho ni kuionea Zanzibar kama tunavyowaonea Waislamu kuwanyima mahakama ya kadhi.

Zanzibar waachwe wajiunge OIC.
Mwisho unapomkosea mtu kwa kumtukana bila kosa lolote, akikuuliza kwanini umemtukana, usikae kimya as if you did nothing wrong!, jifunze kusema sorry!.

P
Sorry
Idu.
 
Joining OIC is about Foreign relations, which falls under Union matters. So as long as sisi Watanganyika hatuna interest na hicho kikundi cha magaidi, the other side of the Union can not join. Waachane na hili suala. Hata enzi za Mzee wa Ruksa , wenzetu wa Visiwani walishataka kuanza hizi chokochoko, ila bahati nzuri Mchonga ( RIP) alikuwa bado active na aliwakemea kwa nguvu zake zote wakaufyata na huyo mzee Ruksa wao. Sasa ngoja tumpime na huyu kwa hili.

hamuna interest na kikundi cha magaidi, lakini bandari mumesha wakabidhi
 
Bro una akili kweli ila leo umeboronga .....uganda ilijiunga oic sababu ya idi amini sio waganda walipenda ........ Tanzania wakiristo 50% waislam 32% ....why tujiunge na oic wakati nchi hii siyo kiislam.....

kwanini hao Uganda hawajajitoa mpaka leo? au wanalazimishwa?
 
Kuna msukumo mkubwa wa Wazanzibari ukichagizwa na uislam kwa Rais Samia na Rais Mwinyi kutaka Serikali ya Zanzibar kujiunga na OIC ili vijana wa Zanzibar wapate ajira na ujenzi wa bandari kubwa kisiwani Unguja.

Hilo ni jambo jema kwa maendeleo kama yatapatikana kweli. Changamoto iliyopo ni maendeleo hayo kunasibishwa na uislam na waislam ambapo unaweza ukazaliwa ubaguzi mbaya sana wa kidini.

Angalizo kwa wale wanaotaka Zanzibar kujiunga na OIC ni kuwa kuna nchi nyingi za Kiafrika ambazo zilijiunga na Jumuiya hiyo kwa matumaini ya kupata maendeleo makubwa na ya haraka, lakini badala yake yakuzaliwa makundi ya magaidi wa kiislam ambayo yamekuwa hatari kwa serikali za nchi hizo na hakuna maendeleo yaliyokusudiwa. Mfano ni jirani yetu Uganda ambayo ni mwanachama wa OIC na walichovuna ni kuzuka kwa kikundi cha kigaidi kinachoisumbua serikali ya Museveni na hakuna mchango wo wote wa maendeleo ambao Uganda inapata!

View attachment 3112979
Uganda hakuna kikundi Cha Waasai Cha Kiislamu.
 
Kwani hukuona kwenye tamasha la Kizimkazi walipelekwa wanyama mbalimbali hadi simba aliyepewa jina la Tundu Lissu?
Aanhaaa....kumbe Tundu Lissu ni jina la simba aliyepelekwa Zanzibar ?

Duuu.... walifanya utani utani wa majina ya Simba ili kuwapumbaza Watanganyika kwamba anahamishia wanyama Zanzibar ?

Julius Nyerere, with this inexplicably boneheaded union, did worse than Chifu Mangungo of Unyanyembe.

Mangungo, an illiterate tribal Chief in 19th Century Africa, was fooled by people a thousand times better educated than him.

Nyerere was an alumni of the Fabian Society Think Tank of Edinburg, and willingly entered an unspeakably foolish contract with peers in Zanzibar who could barely read and write.
 
Kwanza naunga mkono hoja Wazanzibari sio tuu waruhusiwe kujiunga OIC, bali Tanzania tujiunge na OIC kwaajili ya Wazanzibari!

Kila nchi inaweza kufaidika kwa fursa zake, hivyo failures ya Uganda kufaidika na OIC is not an excuse Zanzibar isifaidike!. Kuahidiwa Mahakama ya Kadhi, kujiunga na OIC kumeleta mshikamano na serikali? na Kumbe CCM na Ikulu ndio inaratibu Tanzania kuwa nchi ya Kiislam
P
Huwa unaongea sarcastically, lakini wengine huku huwa hatujui kuwa hiyo ni sarcasm, tunachojua na kuamini ni hilo 'Boko' ulilotoa na Wala siyo hiyo hidden meaning.

Ushauri wangu Kwa kuwa JF ni jukwaa la wengi wenye uwezo tofauti tofauti, siyo wote wanaweza ku- decipher hidden meaning; basi jitahidi kuwa more genuine na direct kwenye maandiko yako. Mwiko uite tu mwiko siyo kusema kijiko kikubwa Cha mti au kasia ndogo ya ugali.
 
Kuna msukumo mkubwa wa Wazanzibari ukichagizwa na uislam kwa Rais Samia na Rais Mwinyi kutaka Serikali ya Zanzibar kujiunga na OIC ili vijana wa Zanzibar wapate ajira na ujenzi wa bandari kubwa kisiwani Unguja.

Hilo ni jambo jema kwa maendeleo kama yatapatikana kweli. Changamoto iliyopo ni maendeleo hayo kunasibishwa na uislam na waislam ambapo unaweza ukazaliwa ubaguzi mbaya sana wa kidini.

Angalizo kwa wale wanaotaka Zanzibar kujiunga na OIC ni kuwa kuna nchi nyingi za Kiafrika ambazo zilijiunga na Jumuiya hiyo kwa matumaini ya kupata maendeleo makubwa na ya haraka, lakini badala yake yakuzaliwa makundi ya magaidi wa kiislam ambayo yamekuwa hatari kwa serikali za nchi hizo na hakuna maendeleo yaliyokusudiwa. Mfano ni jirani yetu Uganda ambayo ni mwanachama wa OIC na walichovuna ni kuzuka kwa kikundi cha kigaidi kinachoisumbua serikali ya Museveni na hakuna mchango wo wote wa maendeleo ambao Uganda inapata!

View attachment 3112979

si mtuachie nchi yetu kwani huko Tanganyika tunapata kitu gani zaidi ya kuuliwa wakati wa uchaguzi na kuwekwa vibaraka vyenu ??
 
si mtuachie nchi yetu kwani huko Tanganyika tunapata kitu gani zaidi ya kuuliwa wakati wa uchaguzi na kuwekwa vibaraka vyenu ??
Kawaulize Wapemba pale Kariakoo wanapata faida gani?
 
Kawaulize Wapemba pale Kariakoo wanapata faida gani?

Wapemba wako Mombasa , Mogadisho , Oman , Dubai London, Marekani , Canada ukiwauliza wanataka nini nchini kwao ? Watakwambia wanataka mamlaka kamili ya nchi yao
 
Tatizo si Wazanzibari kujiunga na OIC.

Tatizo ni udini na na Uzanzibari aliousema Mzee. Kwamba Samia Muislam, Mwinyi Muislam, Kombo Muislam, Masauni Muislam, wote Wazanzibari, wajiunge na OIC haraka, asije rais Mkristo akaharibu mambo.

Hii ni kauli ya kubagua Watanzania kidini, kinyume na katiba za Tanzania, Zanzibar na CHADEMA.
SI UNAONA WALIOTAJWA WOTE WALIVYONYAMAZA KIMYAAAAA, HUKU WAKITABASAMU KWA MBAAAALI, INA MAANA WAMEBARIKI HILO SWALA.
 
SI UNAONA WALIOTAJWA WOTE WALIVYONYAMAZA KIMYAAAAA, HUKU WAKITABASAMU KWA MBAAAALI, INA MAANA WAMEBARIKI HILO SWALA.
Wanataka watu wengi zaidi wajitokeze kupaza sauti!
 
SI UNAONA WALIOTAJWA WOTE WALIVYONYAMAZA KIMYAAAAA, HUKU WAKITABASAMU KWA MBAAAALI, INA MAANA WAMEBARIKI HILO SWALA.
Hivi kwa nini serikaki ya Muungano ya Tanzania ni vigumu sana kuwapa Wazanzibari kura ya maoni waamue kama wanataka kubaki kwenye Muungano ama la, iwe ya haki na huru, tujue moja onve and for all.

Wakisema wanautaka Muungano waamue ni wa serikali moja, mbiki au tatu.

Wakikubali tuendelee nao kwenye Muungano na yeyote atakayeuhoni tumshughulikie kama mchochezi, kwa sababu Muungano umeshakubakika na watu.

Wakikataa tuwaachie waende na nchi yao.

Maana kwa sasa Wazanzibari ni kama wamelazimishwa kuwa kwenye Muungano.

Come to think of it, hii kura inahitajika Tanzania nzima.

Maana hakuna siku yoyote ambayo Mtanzania wa kawaida aliulizwa kuhusu Muungano huu kabka haujaundwa.
 
Nisiwachoshe wanajukwaa hapo chini nimeattach link mukaisome ili wale wenye mawazo kama ya yule mzee wa CDM aliyeropoka kwamba OIC what? sijui OIC itasaidia? Enewei, tusipende vya bure no free lunch

 
Back
Top Bottom