Wazanzibari na Imani yao kwa Allah

Wazanzibari na Imani yao kwa Allah

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WAZANZIBARI NA IMANI YAO KWA ALLAH

Rais Hussein Mwinyi kafungua msikiti uliopewa jina lake.

Jina la msikiti huo litabaki siku zote kuwa Masjid Hussein jina la mjukuu wa Mtume SAW.

Rais Mwinyi akaombewa dua na Waislam na yeye akashukuru kwa hilo.

Hawa ndiyo Wazanzibari walioutanguliza mbele Uislam wao na kuupokea mwito wa Allah kuwa Waislam ni ndugu.

Naamini bila ya chembe ya shaka kuwa Rais Hussein Mwinyi anajua uzito wa dua hizi anazoombewa na yeye akiwa kasimama kibla kanyanyua mikono anaitika Amin pamoja na Waislam.

Naamini Rais Hussein Mwinyi anatambua dhima anayobeba mbele ya Allah na mbele ya nduguze Wazanzibar wanaomkaribisha katika misikiti yao wakanyanyua mikono yao juu kwa Allah kumuombea yeye dua na kuiombea Zanzibar salama.

Wazanzibari hawategemei baada ya haya yote damu ya Mzanzibari itakuja mwagika bila haki kwa sababu yoyote ile na yeye yupo madarakani.

Utakuwa msiba mkubwa.

Hakika Wazanzibari kwa dua zao hizi mbele ya Allah wamemtwisha rais wao mzigo mkubwa sana.

 
..subirini wakati wa uchaguzi muone atakachowafanya.

..sijui kwanini mnawaamini CCM mpaka leo pamoja na yote waliyowatenda.

..Rest in Peace Aboubakar Khamis Bakari.
 
..subirini wakati wa uchaguzi muone atakachowafanya.

..sijui kwanini mnawaamini CCM mpaka leo pamoja na yote waliyowatenda.

..Rest in Peace Aboubakar Khamis Bakari.
JK,
Uchaguzi ujao ni mtihani mkubwa sana.
 
Zikifika time za Jecha hapo mnatafutana kama sio nyote waislam
 
JK,
Uchaguzi ujao ni mtihani mkubwa sana.
Vipi na wale wahanga wa operesheni tokomeza iliyokafanyika na ostaadh jakaya mrisho kikwete nao umewasahau au kisa sio waislamu? Au kisa yalifanyika na muislamu huku wahanga wakiwa sio waislamu? Wewe jamaa ni mtu hatari mno kwa usalama wa nchi
 
Vipi na wale wahanga wa operesheni tokomeza iliyokafanyika na ostaadh jakaya mrisho kikwete nao umewasahau au kisa sio waislamu? Au kisa yalifanyika na muislamu huku wahanga wakiwa sio waislamu? Wewe jamaa ni mtu hatari mno kwa usalama wa nchi
Mnachihangu,
Mimi napenda mijadala yenye adabu na heshima ili jamii inufaike kutokana na hoja kinzani.

Ikiwa mjadala una kejeli mimi hunitoa hamu ya kushiriki.
Mathalan ''Ostaadh Mrisho Kikwete,'' kejeli hii ina faida gani katika hoja yako?
 
Mnachihangu,
Mimi napenda mijadala yenye adabu na heshima ili jamii inufaike kutokana na hoja kinzani.

Ikiwa mjadala una kejeli mimi hunitoa hamu ya kushiriki.
Mathalan ''Ostaadh Mrisho Kikwete,'' kejeli hii ina faida gani katika hoja yako?
Adabu ipi unaihitaji umesahau kuwa profesa Lipumba mwaka 2010 alimpigania Kikwete kwasababu ya padre Slaa alikuwa anamshambulia sana ? Umesahau ni Lipumba aliekihimiza waislamu wamuunge mkono Kikwete kwakuwa ni muislamu?
 
Mnachihangu,
Mimi napenda mijadala yenye adabu na heshima ili jamii inufaike kutokana na hoja kinzani.

Ikiwa mjadala una kejeli mimi hunitoa hamu ya kushiriki.
Mathalan ''Ostaadh Mrisho Kikwete,'' kejeli hii ina faida gani katika hoja yako?
msamehe bure ndugu yangu hawa ndiyo vijana wanaoitwa taifa la kesho
 
Adabu ipi unaihitaji umesahau kuwa profesa lipumba mwaka 2010 alimpigania kikwete kwasababu ya padre slaa alikuwa anamshambulia sana ? Umesahau ni lipumba aliekihimiza waislamu wamuunge mkono kikwete kwakuwa ni muislamu?
Mnachi...
Hayo unayosema hayana shida.
Kukosa uungwana ni kule kumtaja Kikwete kwa kumkejeli.
 
Mnachi...
Hayo unayosema hayana shida.
Kukosa uungwana ni kule kumtaja Kikwete kwa kumkejeli.
Kumkejeli kivipi kwani kikwete sio muislamu? Tunaweka kumbukumbu sawa yasije kutokea yale ya majemedari wa vita vya majimaji
 
Kumbe Hussein ni jina la mjukuu wa mtume?
Watoto wake mtume walikuwa kina nani?

Halafu mkuu majina kama Hamis, Juma, Jumanne, Abdallah, mbona hatuyaoni kwa waarabu? Mnayatoaga kwenye dini au?
 
Eti waislam ni ndugu, kisa wote mnashobokea utamaduni wa kiarabu? mkienda kule Madina kufanya kazi za ndani waarabu watawafanya ndugu zenu wala hamtabugudhiwa.

Sent from my BBF100-6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom