Wazanzibari tumemchoka Hussein Mwinyi

Falconer

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2008
Posts
891
Reaction score
541
Tangazo jipya la kuwaondosha zaidi ya familia mia tano katika mtaa wa kikwajuni kwa kuwapa wawekezaji ni kitendo kisicho kubalika kabisa.
Tangu alipoapishwa kuwa raisi, Mwinyi amekuwa ni kitendawili kwa jamii yetu. Fukwe za bahari zote zimepewa wawekezaji kwa kujenga mahoteli ya kitalii. Mitaa na wanachi wameondoshwa makwao kupisha ujenzi wa Mwinyi na watu wake. Sisi tuna uwanja wa ndege kisauni sasa kuna taarifa ya kujenga kiwanja cha ndege chengine. Hiyo nafasi iko wapi?. Hizi ardhi zetu munasema ni za serikali mbona munawapa watu wasiokuwa na hisia ya ardhi zetu. Mwinyi kweli ametimiza ambayo wenzake walishindwa kutekeleza.
Tunawaomba CCM muje muchukuwa pandikizi lenu. Sisi tumechoka nae. Yeye anajuwa kuwa hapati kura kwa hiyo CCM itambeba kwa hali yoyote ile.
 
Acha Mwinyi awanyooshe maana huwa hamkubali watu wa bara wanunue ardhi Zanzibar ila wazungu, waarab na wahindi mnawapa ardhi kama vile mnagawa njugu bila hata kuhoji
 
Njooni bara ardhi tele mje mlime huku hakuna ubivu kushinda barazani mfanye kazi.....ifakara huko mkalime mpungam...na biashara kibao bara mje acheni zbar iwe ya utaliii
 


wacha wawekezaji waibadirishe zanzibar, akina sisi tukija zanzibar hamtaki kutuuzia hata kidogo. Mwinyi mzenji kama wewe, alipo mpo na mlipo yupo.
 
subirini uchaguzi mkuu mumuondoe ni vizuri kuheshimu taratibu tulizojiwekea.
 
Tulieni kwanza nyie wazenji bomu la mungano linakaribia kuripuka
 
Nyie Mwinyi sisi huyu mama yenu hatumtaki huku bara
 
Mpaka mseme, bado saaaanaaaa
 
Na sisi ma Samia kakimbiza wa Masai na nyinyi onjeni joto la jiwe
 
Uwanja wa ndege huu anautaka kuujenga wapi kisauni au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…