MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,580
Someni Biblia, muongozo jinsi ya kulea watoto wenu iko mule imetulia, hizo mbwembwe za kizungu ni kizungumkuti tu hazina msaada. Punguzeni uzungu, mtoto wa miaka 12 unamnunulia blackberry aingie facebook, tv mnaweka DSTV watoto wanaangalia makorokocha yasiyokuwa na msingi kisa mna hela za kuwawekea.
Someni Biblia, muongozo jinsi ya kulea watoto wenu iko mule imetulia, hizo mbwembwe za kizungu ni kizungumkuti tu hazina msaada. Punguzeni uzungu, mtoto wa miaka 12 unamnunulia blackberry aingie facebook, tv mnaweka DSTV watoto wanaangalia makorokocha yasiyokuwa na msingi kisa mna hela za kuwawekea.
<br />Someni Biblia, muongozo jinsi ya kulea watoto wenu iko mule imetulia, hizo mbwembwe za kizungu ni kizungumkuti tu hazina msaada. Punguzeni uzungu, mtoto wa miaka 12 unamnunulia blackberry aingie facebook, tv mnaweka DSTV watoto wanaangalia makorokocha yasiyokuwa na msingi kisa mna hela za kuwawekea.
CD shule yako imekuwa ngumu kidogo kuielewa hasa unapoongelea mtoto wa nje<br />
<br />
...kuwalinda au kuwaongoza,.mmmnnh nimeipenda hiyo...
tupo ukurasa mmoja wazazi wenzangu...
blaki woman karibu kwenye mdahalo....hii mada ni mahsusi kwa ajili ya binti chini ya miaka ishirini na moja,
lengo, nia na madhumuni yangu ni kutaka kujua upande huo ulio dhaifu kwangu, jambo ambalo kumbe pia
limeamsha hisia kwa wazazi wengine waliokuwa na maswali sawa na haya...
Leo Dada Caro kaamua kutupa mitihani shost yaani mwe!!
Sasa hapo chukua mtoto wa nje, changanya na picha kuwa mnatoka dini tofauti......................unaanzia wapi?! sijui ndo uanze kwanza kuingia darasani kujifunza dini yake ndo mkae muelewane!! Eh, nahisi leo nikimuota Caro, sitashangaa kabisa!
....lol....umeniibia password yangu wewe, nitakushtaki kwa moderator....ha hahaha...
Vunja ukimya, zungumza na mwanao.
Kusema ukweli malezi ni magumu na 'mazungumzo' kati ya mzazi/wazazi na mtoto yanapaswa kuanza mapema zaidi, Jana nilikuwa naangalia taarifa ya habari, mbabu wa miaka karibia 55, amepigwa kwa kumbaka mtoto wa miaka 9 ambaye mama yake alimtuma nyumbani kwa Mbabu huyo akaombe chumvi. Baada ya kukamatwa Mbabu anajitetea kuwa " Ni kweli nimemfanya, lakini sikumalizia!!! - meaning yeye hakufika kilele!! kwa kuwa watu walikuja kumvamia". nilishikwa na hacra na huzuni nikatamani yule mwandishi wa habari amzabe japo kibao. Nikaishia kujiuliza ina maana kuna watu leo hii hawajui kuwa hili ni kosa?
Lakini baadae nikawaza wazazi kama wazazi nafasi yetu ya kuwaandaa wenetu na hizi changamoto iko wapi? Je tumeshaweza kumfundisha mtoto 'dalili' na 'mbinu' na aina ya vishawishi ambavyo akiviona ajue hatari iliyopo mbele yake?? Sijui
Kwa hii mada ndo nachanganyikiwa kabisaaaa...........hivi sie wazazi, pamoja na 'uzoefu' wetu katika mapenzi, kweli tuna uwezo wa kuwaainishia wenetu, dalili ya mpenzi wa uwongo? tapeli? au ambaye ni likely kuja kumwuumiza huko mbele so that tumwambie awe extra care na flan kwani tunahisi si mkweli, hana mapenzi ya kweli au atamletea maumivu mbeleni??
Yaani leo kama kuniweza mmeniweza!
....,... kisha tulinganishe kwenye mazingira ya kisasa, utamvushaje binti na vishawishi hivi vya
distractions za boyfriends/girlfriends, fashionistas, facebook, twitter, sms chatting etc...
mfano; is it right to access her online accounts? accessing her phonebook calls and sms? au?
kumtumia watu wamchunguze?...
Good advice tulizo, kun a dada angu pia yuko over proctective kama nini sijui, mtoto wake sasa ana miaka 19 ana boyfriend, ssa kwa kumuogopa mama yake kaamua kushare na mie, na mie sitaki kuondoa ile trust nimwambie mama yake namwacha, ila kila nikikaa nae namwambia awe rafiki na mwanae atafaidi sana, coz atakuwa anashea nae vitu vingi sanaMkuu..kuna vitu viwili vya kuzingatia. Umri wa mtoto na uhuru/Haki za mtoto.
Kumlea mtoto katika mwenendo unaokubalika na familia siyo lazima kuingilia na kumnyima uhuru wake hasa pale anapokuwa umri wa ujana (miaka 15 au 16 na kuendeleaa). Kumbuka Ku-access online email account ya mtoto wa miaka 4 siyo sawa na ku-access email account ya mtoto wa miaka 16 au 18. Hivyo basi kuna umri ambazo ni lazima kila kitu kiwe monitored kama email, internet usage etc na kuna umri ambao lazima tumpe mtoto uhuru na haki ya kujiamulia. Mfano kwa watoto wadogo hadi umri wa kati tunaweza kitu kama Kids Email | Safe Email for Kids) ambayo email za mtoto zinapitia kwa parent hadi approve ndiyo zinakuwa delivered katika inbox ya mtoto..(bila mtoto kujua). Lakini kuna umri ambao itabidi tumwache mtoto afungue email anayotaka ni umri gani? inategemea na maisha ya familia na malezi.
Kumpa uhuru na haki siyo kwamba ndio tumwache .. La hasa..ni lazima tuwe nae bega kwa bega.. Kumbuka mtoto lazima ajue maisha yake ni maisha ya familia hivyo basi furaha yake ndiyo furaha ya familia na huzuni yake ni huzuni ya familia. Binafsi, nitakuwa radhi kumruhusu binti yangu awe na rafiki ya kiume (umri ukifika) lakini kwa uangalifu sana. Kwani nikiwa mwanaume najua jinsi wanaume wanavyokuwa waharibifu. na hasa hivi vi"boyz" vinaanza uharibifu bado vi-dogo.. uharibifu siyo lazima uwe physical sex intercourse.."Broken heart" ni uharibifu tosha...Wakati tunaruhusu mabinti wetu waingie kwenye Game lazima mabinti wajue uchungu na tamu ya mapenzi.. binti lazima ajue Huzuni yake ni balaa kwa familia.. Ni jinsi gani ya kumwelekeza huko ..hapo nadhani inategemea na malezi na ukaribu wa familia husika...
In short, controls zinategemea na umri wa mtoto kadri anavyokuwa kijana kitu kinachobaki ni ku-strengthen awareness kwa mtoto kuwa chochote anafanya ni kwa ajili ya familia na wala si kwa ajili yake binafsi. Kama ataleta furaha au huzuni ni kwa ajili ya familia nzima na wala si kitu binafsi, nadhani kwa njia hii mtoto au kijana atakuwa muwazi kwa wazazi..nasi wazazi tutaendelea kuwa "baneti kwa baneti au sambamba" kama maafande wangu walivyokuwa wanasema kule JKT mafinga.
Malezi siku hizi yamekuwa magumu sana, wazazi wenyewe mnawavalisha watoto wenu wa kike kama watu wazima, utakuta katoto ka kike kanene kamevaa kasketi hadi makalio yanaonekana, jiangalieni pia upya wazazi sababu dunia ilipofikia ni pabaya sana, utakuta zee zima linabaka mtoto wa miaka saba, waepusheni watoto wenu na mabalaa kwa kukaa nao na kuwaeleza umuhimu wa kujisitiri na yanayojiri sasa hivi mtaani
Good advice tulizo, kun a dada angu pia yuko over proctective kama nini sijui, mtoto wake sasa ana miaka 19 ana boyfriend, ssa kwa kumuogopa mama yake kaamua kushare na mie, na mie sitaki kuondoa ile trust nimwambie mama yake namwacha, ila kila nikikaa nae namwambia awe rafiki na mwanae atafaidi sana, coz atakuwa anashea nae vitu vingi sana
Urudi Askofu utupe shuhuda za waumini wako.Nitarudi baadae...
MJ1 nimekumisi tu
Urudi Askofu utupe shuhuda za waumini wako.
Too bad sijaja kuungama muda mrefu Askofu. Nahisi siku nikija itabidi uwe na note book na kalamu! unawezasahau kunisamehesha mengine!