Wazazi wakataa sadaka ya kuchinja iliyotolewa na Waarabu, wakidai watoto wao watatolewa kafara

Kaka wamekula siku moja wameenda toilet kesho nani atawapa tena nyama ya mbuzi? Ungekua ni msaada endelevu hata kwa miaka5 sawa.
Ukuta unakaa miaka mia kaka,hao wazazi wanawaza mbali

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Ifike wakati Sasa hata hii misaada tunayopewa.... Tuwa tuna-evaluate.... Ni kitu kinachokuwa na manufaa endelevu kwa jamii zetu au ni kitu cha siku moja .... Kesho yake unakwenda haja na habari imeishia hapo.
 
Halafu kitu kingine.... Tokea lini tukaanza kulazimishana kupokea sadaka/ misaada??

Kama walengwa wamekataa.... What's the logic ya kuanza kulazimishana kupokea sadaka za nyama ya mbuzi na ngombe🤣😂
Hapo hawajalazimishwa tu hali hii sasa wangelazimishwa hali si ingekuwa mbaya zaidi?
 
Hayo ndiyo madhara ya kupandikiza udini sasa wacha twende hivyo hivyo huku waasisi wakisifiwa kiasi cha kutaka kuabudiwa kwamba wao eti ndio wameleta umoja utafikiri wakati wakichukua madaraka toka kwa wazungu kulikuwa na vita vya kikabila na udini, sasa washajiondokea zao wametuachia sisi balaa.
 
Ifike wakati Sasa hata hii misaada tunayopewa.... Tuwa tuna-evaluate.... Ni kitu kinachokuwa na manufaa endelevu kwa jamii zetu au ni kitu cha siku moja .... Kesho yake unakwenda haja na habari imeishia hapo.
Muhimu hapo ni kutafuta cha kwako tu na sio kuanza kupanga usaidiwe nini itakuwa vichekesho.
 
Muhimu hapo ni kutafuta cha kwako tu na sio kuanza kupanga usaidiwe nini itakuwa vichekesho.
Hapa nazungumzia kwenye scenario za misaada inayotolewa kwenye jamii. Hii huwa ipo na itaendelea kuwepo.
 
Kama ni sadaka mbona ni nzuri tu kwanini wakatae
Lakini sio lazima kukubali hiyo sadaka pia ,, nadhani Kama kweli wanalengo la kutoa sadaka Basi walau wange wajengea visima vya maji , Who knows kuhusu usalama wa hizo nyama na usalama wa Afya za hao watakao pewa !?
 
Wakristo ni wehu wasile nyama hizo watakula majini
 
Wazazi vilaza
 
Kuna punguani hawana akili kabisa. Unanipa msaada ninakataa, kinachofanya upige yowe na kulazimisha niupokee ni nini?

Nini mantiki ya kula nyama siku moja au mbili. Hiyo ni chanjo dhidi ya njaa au ina maajabu gani mpaka mshupaze shingo kulazimisha watu wale
 
Msaada au sadaka ya kula siku moja ndio muusifie hivi
Shida sio nyama tuwaelewe vizuri wazazi.. ok wale leo nyama na kesho je?

Kama ni msaada kama mnavyodai basi wangezipa shule hizo mifugo wafuge watoto wanywe maziwa watapata samadi kuweka kwenye bustani za mboga au shamba la mahindi Kwa ufupi shule zitakuwa na miradi ya kujikimu.

Sasa mnashabikia eti wanakataa nyama
Ndiyo wengine wana imani zao kwa nini kudharau imani zao
Kama ni kafara je? Sadaka za kuchinja Kwa nini hawachinji kwao?

Ni upuuzi kukubali kulishwa nyama siku moja eti sadaka

Msaada wa mzungu haufanani na msaada wa mwarabu tuache unafiki
Mzungu atajenga shule hospitali vituo vya kulelea watoto
 
Hapa nazungumzia kwenye scenario za misaada inayotolewa kwenye jamii. Hii huwa ipo na itaendelea kuwepo.
Ndio hivyo maana utakuta unapewa msaada wa pesa halafu unaambiwa uitumiaje hiyo pesa yani anakupangia matumizi, bora ule msaada ambao anaulizwa kabisa uchague mwenyewe sasa ukitaka ujengewe uwanja wa mpira au msikiti hapo ni vipaumbele vyako mwenyewe.
 
Mkuu mbona waarabu wanajenga hadi visima vya maji na mambo kibao tu sasa hii sadaka ya nyama ndio iwe shida? Hawajalazimishwa kwa sababu sadaka haulazimishwi ni hiari yako uchukue au ukatae.
 
Kula nyama uingize protini mkuu halafu usizarau kuna wengine nyama hawali makwao ni kama anasa, kuna wengine maji ya kunywa ya baridi tu dili ila kwa wengine ni kitu cha kawaida, hata hivyo watu walielimishwa na wengine wakachukua nyama wameenda kujenga shavu na ukuta watajengewa pia.
 
Mkuu hakuna kitu kibaya kama kukosa akili au upumbavu... Nimesikiliza kipindi cha Leo tena clouds media mpaka nikashika kichwa jinsi baadhi ya jamii zetu ilivyojaa ujinga...
 
Ni sahihi kabisa. Huo msaada upelekwe huko magerezani na kwenye vituo vya watoto yatima.
Hawa jamaa wao wamekijika kwenye kuinua ubora wa elimu mashuleni na moja ya program zao ni kusaidia chakula mashuleni kwa sababu wamebaini ni tatizo kubwa kwa wanafunzi kukaa shuleni tokea saa moja asubuhi mpaka saa kumi bila kula... So hawawezi kwenda kwenye Magereza coz it's not targeted people..
 
Hahah naona asimiaa kubwa bado sana hajawaza nje ya Box !! ...... Mimi binafsi nimewaza hivi ! Hawa watu bhanaa wanajifanya watoa msaada saiv lakin hilo sio lengo lao kuna kitu wanatafuta sio kwa wanafunzi bali hata katika jamii au serikali au hata nje ya mipaka yetu sio bure !! Kuna hadithi nyingi sana tumekuwa wafadhili wa hawa alshabaab pasipo sisi wenyewe kujuaa !! Wanaweza kufanya wanayofanya saiv lakin lengo lao sio hilo !! Wanaweza kuanza kwa misaada ili wafikie target yao wanayoitaka !! Cha msingi zaidi usalama wa nchi inabidi waangalie Source of fund kwa hawa jamaa !! .. Na ni nan kiongozi wao hawa jamaa !! Waangalie 2 years before kuanzishwa kwa misada hii .. je hawa viongozi wa sasa walishawahi kusafiri kwenda nje ya nchi ?? Kama ikitokea mmoja wapo alishawahi kuingia kenya au mombasa , au somaliaa basi mjuee ufadhili uko kule !! Kichaka cha kutengeneza genge la wahalifu !! Fuatilieni Procedure zote wanazopitia CIA kung’oa mizizi ya OSAMA BIN LADEN !! MTANZANIA AMKA !! HAYA NI MAWAZO YANGU NIMEWAZA NJE YA BOX !!
 
Nyama ya siku moja inaongeza shavu? Hii nchi umaskini umezidi kipimo, yani mtu serious karne ya 21 nchi ina miaka 60 imepata uhuru analilia nyama za siku moja aongeze shavu.

Alafu aliyewaambia nyama ni lazima sana mwilini nani, kwani vegs hawaishi. Au protein ni lazima iwe nyama tu? Mkoa wenyewe ni Arusha kuna nyama kibao alafu wanatokea Waarabu wanalazimisha mpaka kuja kwenye vikao kuhakikisha watoto wanakula "SADAKA". Upuuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…